Hongera kwa Mkurungenzi wa jiji la Tanga

Kikwajuni One

JF-Expert Member
Mar 18, 2013
13,142
6,947
Nilikuwa Tanga hivi karibuni,likapita gari la matangazo,kukataza wafanyabiashara kupanga vitu nje,pamoja na wanaofanyabiashara barabarani.Inakuwa vigumu sana kwa watembea wa miguu,kupata sehemu ya kupita inabidi upite barabarani,ambapo ni hatari kwa usalama.

Kwa mfano maeneo ya soko la Ngamiani mpaka kuelekea stand ya mabasi ya mikoani,kuna daladala zinapaki maeneo yale,na kuna wafanyabiashara njiani na kwenye baraza za nyumba,inabidi mtembea kwa miguu apite barabarani.

Na kuna wanaoweka vijiwe vya kahawa katika maeneo ya barazani,watu wanajaa mpaka barabarani,kiasi kuwa ni tabu kwa mpita njia.

Ningeomba isiishie kuwatangazia waondoke tu,zichukuliwe hatua za kuwaondoa.Na vyombo vingine vya dola vishirikiane kuwaondoa watu hawa.

Hawa wanaofanya bishara njiani wanakosesha mapato kwa serekali na jiji. Nampongeza sana Mkurungezi wa jiji Tanga kwa kutufikiria watembea kwa miguu.
 
Kama ni hivyo hongera zake,mimi pia nimeona mabadiliko sana Tanga inapendeza sasa si kama zamani ukipita pale mabanda ya papa ni harufu ya papa tu na nguru, lakini hivi karibuni nilikuja Tanga nimeona kumetengenezwa bustani mabanda yamevunjwa kunavutia, hata ile garden ya forodhani nimeipenda sana ila wahamishe stand ile ni ndogo sana sijui kama wana mikakati hiyo.
 
Mkurugenzi wa Tanga anajitahidi sana kutimiza majukumu yake, hongera sana, hata mikutano mingi imehama bagamoyo ipo Tanga
 
Wa sasa mji unamshinda kwa uchafu.Tanga tunaikumbuka kalembo day ilikuwa kila mwisho wa mwezi watu tunafanya usafi mpaka yakawa mapenzi yetu.
 

Attachments

  • 20170215_182552.jpg
    20170215_182552.jpg
    390.9 KB · Views: 25
  • 20170215_182542.jpg
    20170215_182542.jpg
    437.3 KB · Views: 23
  • 20161105_090936.jpg
    20161105_090936.jpg
    348.9 KB · Views: 21
Back
Top Bottom