nuruyamnyonge
JF-Expert Member
- Mar 18, 2014
- 4,439
- 2,287
Leo asubuhi katika kipindi cha nipashe radio one nimemsikia naibu spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania na mjumbe wa bunge la katiba mh.Job Ndugai akisema, hatuwezi kupata katiba mpya kwa misimamo mikali ya kwa pande zote mbili.
Job amekwenda mbali saidi na kusema wajumbe wengi wa ccm wanamisimamo mikali kila anaye simama anapinga rasimu ya warioba hii haitasaidia badala yake amesema wakae pamoja na Ukawa ili wafanye maridhiano taifa lisonge mbele.
Ameongeza tena kuwa bunge la katiba linawatu wengi sana kitu ambacho kinachangia kila mtu kuomba muongozo na kupoteza muda, amesisitiza lazima ccm wakae chini na kuacha hiyo misimamo yao mikali kwani haitasaidia kupata katiba mpya.amemalizia kwa kushangaa ccm kusema kama takwimu za warioba siyo halali wabunge wa bunge la katiba wanafanya nini kujadili takwimu hewa!
Naomba kama kuna mchambuzi kamsikiliza vizuri nae aje hapa achangie hiyo kauli ya Job. Matusi hayatakiwi humu ndani jikite kwenye mada.karibuni kwa kuchangia.
Job amekwenda mbali saidi na kusema wajumbe wengi wa ccm wanamisimamo mikali kila anaye simama anapinga rasimu ya warioba hii haitasaidia badala yake amesema wakae pamoja na Ukawa ili wafanye maridhiano taifa lisonge mbele.
Ameongeza tena kuwa bunge la katiba linawatu wengi sana kitu ambacho kinachangia kila mtu kuomba muongozo na kupoteza muda, amesisitiza lazima ccm wakae chini na kuacha hiyo misimamo yao mikali kwani haitasaidia kupata katiba mpya.amemalizia kwa kushangaa ccm kusema kama takwimu za warioba siyo halali wabunge wa bunge la katiba wanafanya nini kujadili takwimu hewa!
Naomba kama kuna mchambuzi kamsikiliza vizuri nae aje hapa achangie hiyo kauli ya Job. Matusi hayatakiwi humu ndani jikite kwenye mada.karibuni kwa kuchangia.