Hongera Dr.Slaa

akashube

JF-Expert Member
Dec 24, 2009
401
23
Dr. Slaa nakupongeza sana kwa kuleta mabadiliko makubwa katika demokrasia ya nchi yetu. Umewafanya watawala wapige magoti kwa wananchi kuomba kura maana walijua wazi kuchakachua pekee kusingetosha kuwapa madaraka.

Dr. Slaa umechangia kwa kiasi kikubwa sana kuongeza idadi ya wabunge wa upinzani bungeni na siyo makosa ya CCM kama CCM wanavyojinadi. Ni wabunge wawili tu wa upinzani walioshinda kwa sababu ya makosa ya CCM ambao ni wa Iringa Mjini na Maswa Magharibi. Kwingineko kote Dr. Slaa umechangia kwa kiasi kikubwa sana.

Jimbo la karatu halijapotea, na badala yake tumeongeza Dr. Slaa wengi zaidi bungeni.

Hongera Dr. Slaa.
 
Back
Top Bottom