JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 625
- 938
Pneumonia Ni Nini?
Pneumonia ni ugonjwa unaoshambulia vifuko vya hewa kwenye pafu moja au yote mawili. Vifuko hivi huweza kujaa maji au usaha na kusababibisha kikohozi kinachotoa uchafu unaotoka kwenye mapafu, homa na kupata shida katika kupumua. Vijidudu wa aina nyingi wanaweza kuhusika katika ushambuliaji wa mapafu hayo. Mara nyingi pneumonia hutokana na mashambulizi ya bacteria, virusi, fangasi (fungi) au vijiumbe wengine tegemezi (parasites).
Mtu anapovuta hewa yenye wadudu hawa wadogo (germs) wanaosababisha maradhi, wadudu hawa huingia kwenye mapafu na
kama kinga za mwili za mtu huyu zitashindwa kuwazuia, wadudu hawa hukaa kwenye vifuko vidogo (alveoli) vya kwenye mapafu na kuanza kuzaliana. Mwili utakapopeleka chembechembe nyeupe za damu kupambana na wadudu hawa, vifuko hivi hujaa majimaji na usaha na kusababisha pneumonia.