Homa ya ATCL yawakumba Fastjet

Homa ya ATCL yawakumba Fastjet

Katika ile hali inayoonekana ya ushindani katika usafiri wa anga kufuatia ujio wa dreamliner ya Atcl,kampuni ya ndege fastjet imeanza kuruhusu abiria kusafiri na begi lisilozidi uzito wa 23kg pasipo malipo ya ziada pamoja na kugawa viburudisho mbalimbali ndani ya ndege.
Kwa hakika ushindani unaleta tija tunaomba makampuni mengine yaje ili nauli pia zishuke bei
View attachment 828667
Nauli zishuke bei? sijui kama iko sahihi!
 
Nimesoma mahala kwamba bei ya nauli imepanda.. kwa hiyo ni yale yale tu.. ila kulazimisha watu kula kwa kulipa zaidi watakimbiwa tu labda wawe na kifungua kinywa cha nguvu haswa kwa wale wasafirio asubuhi mapemaaaa ambao wakifika waendapo ni kazi tu kwanza

Ndege za Magufuli oyeeeeeeeee
Ila wasipate bichwa wawe wanajiongeza hao watumishi
Nimeangalia nauli DAR-KIA tarehe 14.08 (ATCL)=98,000 (one way) wakati Fastjet ni 227,000 akili ni nywele. Fastjet mkatafute kazi nyingine
 
Katika ile hali inayoonekana ya ushindani katika usafiri wa anga kufuatia ujio wa dreamliner ya Atcl,kampuni ya ndege fastjet imeanza kuruhusu abiria kusafiri na begi lisilozidi uzito wa 23kg pasipo malipo ya ziada pamoja na kugawa viburudisho mbalimbali ndani ya ndege.
Kwa hakika ushindani unaleta tija tunaomba makampuni mengine yaje ili nauli pia zishuke bei
View attachment 828667
Hili linatuonesha umuhimu wa upinzani ktk siasa.
 
Fastjet tunauziwa mpaka karanga! AtcL komaeni wayego. Ushindani wa kibiashara ni afya na manufaa kwa wateja.
#NogeshaJPM
 
Kama Pepsi na Coka, mpaka Coka wakashuka bei kuiga bei ya Pepsi.
Ile vita coka walikuwa wamelala! Walivoshtuka tayari Pepsi wameshapiga sana hela na sokoni wamejiimarisha zaidi!

Ile vita haijawaacha coka salama, mpaka Leo bado wanasrago"
 
Sawa mkuu ila sisi wa Tandahimba tunanufaika vipi na hiyo offer..?
Subiri mzazi wako aumwe afu #tandahimba barabara mbovu na mzazi wako anahitaji huduma ya faster muhimbili utajua maana ya offer ...
 
Nyumbani kwangu halafu nizidiwe na mgeni haiwezekani
Lazima Air Tanzania zifunike ardhi ya airport kama BA kwao
 
Subiri mzazi wako aumwe afu #tandahimba barabara mbovu na mzazi wako anahitaji huduma ya faster muhimbili utajua maana ya offer ...
Mkuu dizaini kama unaomba niuguliwe na mazazi. Tandahimba hakuna hata ramani ya uwanja wa ndege .
 
Back
Top Bottom