Hoja za wanaoona lockdown haifai ni zipi? Tuelimishane

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,226
35,151
Mabibi na mabwana naomba niende moja kwa moja kwenye mada. Tumekabiliwa na ugonjwa ambao unatishia maisha yetu kama taifa. Mengi yameelezwa yakiwamo ufafanuzi wa nini maana ya lockdown na kwa nini ni muhimu katika kupambana na Corona. Imeelezwa pia, kwa nini hakuna kitu kama lockdown ya mtu mmoja mmoja.

Mifano imetolewa kuonyesha lockdown haina maana ya mtu kufungiwa chumbani au nyumbani, bali watu wote katika eneo husika kusalia majumbani. Shughuli zilizo muhimu tu ndiyo pekee huruhusiwa kuendelea.

Imeelezwa kwa mifano, tahadhari huchukuliwa kuona kuwa hakuna atakaye athirika kufikia hatua kufa kwa njaa au kukosa kabisa mahitaji muhimu kwa wakati wote wa lockdown. Hata hivyo ni kweli kuwa mtu hata kula au kupata kile ambacho 100% angependa kula au kupata katika kipindi hicho cha mapambano.

Njia hii imethibitika kuwa madhubuti kabisa katika kuivunja minyororo ya maambukizi ya Corona ambayo ni lazima ivunjwe ili kuudhibiti ugonjwa huu.

Bila ya minyororo hii ya maambukizi kuvunjwa, ugonjwa huu utaendelea kuenea kwa kasi. Watu watazidi kufa. Hakutakuwa na natumaini ya lini mashule yatafunguliwa wala ya lini tutarejea kwenye shughuli zetu zote za kawaida.

Kwisha kuweka utangulizi huu, ingependeza kufahamu wanaopinga kutumia njia hii ya lockdown kutanzua janga la ugonjwa huu unaotukabili, hoja zao hasa ni zipi na pengine wanao mbadala upi? Ni muhimu kama jamii tukawa na njia mbalimbali mezani tukijiridhisha kuwa ni ipi tunayoifuata na kwa matumaini yapi.

Ukiangalia kinachotokea Ecuador sasa ni majuto. Hivi wanajilaumu kwanini hawakuchukua hatua kali mapema.

Serikali inaomba msamaha kwa kuchelewa mno kuchukua hatua wakati mitaa tayari imejaa maiti za ugonjwa wa Corona:




Pamoja tutaushinda ugonjwa huu.

Humbly nawasilisha.
 
Setikali imeamua kila kitu kijiendeshe chenyewe.Watu wanakaa ktk migawa ya kahawa,puli, draft no.Kitakaponuka nuka ndii ndio tutajua cha kufanya.Waafrika no watu was ajabu duniani.Magari yanajaza ka kawaida.Dar ilibidi uwekwe karzntini mapema sana kabla hali gaijawa mbaya, Rwanda wamefanikuwa kushusha maambukuzi sisi tupo tupo tu.Makonda anasema watu wasijifungie ni uoga watu wachape kazi, yaaani anahusudu pesa kuliko uhai wa watu.Ni bora wachache wafe kwa njaa kuliko wengi wafe kwa mpigo kwa korona.
 
je wewe umejiweka lockdown?

"baba unahonga hawara elfu kumi,
watoto wanakufa na njaa nyumbani"
 
Hoja sio kwamba lockdown haifai, bali ni kwamba lockdown ni jambo lisilotekelezeka kwa urahisi kwa nchi maskini ambako watu wake wanategemea kutafuta mlo wa kila siku. Mtu hana akiba hata mia, hana bima ya aina yoyote na hata hajui kesho atakula mini halafu wewe unajaribu kumfungia ndani. Ni ngumu.
 
je wewe umejiweka lockdown?

"baba unahonga hawara elfu kumi,
watoto wanakufa na njaa nyumbani"

Mkuu uliweza kuiona paragraph hii kwenye mada?:

"....... Mengi yameelezwa yakiwamo ufafanuzi wa nini maana ya lockdown na kwa nini ni muhimu katika kupambana na Corona. Imeelezwa pia, kwa nini hakuna kitu kama lockdown ya mtu mmoja mmoja."

Angalia vizuri mkuu vinginevyo yatakuwa tena yale ya kudandia treni kwa mbele.
 
Hoja sio kwamba lockdown haifai, bali ni kwamba lockdown ni jambo lisilotekelezeka kwa urahisi kwa nchi maskini ambako watu wake wanategemea kutafuta mlo wa kila siku. Mtu hana akiba hata mia, hana bima ya aina yoyote na hata hajui kesho atakula mini halafu wewe unajaribu kumfungia ndani. Ni ngumu.

Mkuu lockdown sisi siyo wa kwanza. Hali tofauti za kiuchumi za watu huzingatiwa. Inafahamika:

1. Wapo wenye kuhitaji msaada kabisa (in totality).
2. Wapo wenye kuhitaji msaada kiasi (partial).
3. Wapo wanaojitosheleza.
4. Wapo wenye ziada na hata tayari kusaidia wengine.

Serikali pia ipo.

Ni kweli kuwa haitakuwa kipindi cha starehe. Kitakuwa kipindi kigumu cha muda mfupi ambacho hata hivyo hakuna atakaye kufa kwa njaa au kukosa kabisa mahitaji muhimu katika kipindi hicho.

Mkuu kwa vile unaona pia kuwa si kuwa lockdown haifai, huoni pia kuwa kama ikibidi (kwa nyakati zingine) katika kipindi hicho kushindia uji ni heri zaidi kuliko kuja kusambaratishwa na Corona bila jitihada za kutosha?
 
Hoja sio kwamba lockdown haifai, bali ni kwamba lockdown ni jambo lisilotekelezeka kwa urahisi kwa nchi maskini ambako watu wake wanategemea kutafuta mlo wa kila siku. Mtu hana akiba hata mia, hana bima ya aina yoyote na hata hajui kesho atakula mini halafu wewe unajaribu kumfungia ndani. Ni ngumu.

Mkuu lockdown sisi siyo wa kwanza. Hali tofauti za kiuchumi za watu huzingatiwa. Inafahamika:

1. Wapo wenye kuhitaji msaada kabisa (in totality).
2. Wapo wenye kuhitaji msaada kiasi (partial).
3. Wapo wanaojitosheleza.
4. Wapo wenye ziada na hata tayari kusaidia wengine.

Serikali pia ipo.

Ni kweli kuwa haitakuwa kipindi cha starehe. Kitakuwa kipindi kigumu cha muda mfupi ambacho hata hivyo hakuna atakaye kufa kwa njaa au kukosa kabisa mahitaji muhimu katika kipindi hicho.

Mkuu kwa vile unaona pia kuwa si kuwa lockdown haifai, huoni pia kuwa kama ikibidi (kwa nyakati zingine) katika kipindi hicho kushindia uji ni heri zaidi kuliko kuja kusambaratishwa na Corona bila jitihada za kutosha?
 
Hoja sio kwamba lockdown haifai, bali ni kwamba lockdown ni jambo lisilotekelezeka kwa urahisi kwa nchi maskini ambako watu wake wanategemea kutafuta mlo wa kila siku. Mtu hana akiba hata mia, hana bima ya aina yoyote na hata hajui kesho atakula mini halafu wewe unajaribu kumfungia ndani. Ni ngumu.

Mkuu lockdown sisi siyo wa kwanza. Hali tofauti za kiuchumi za watu huzingatiwa. Inafahamika:

1. Wapo wenye kuhitaji msaada kabisa (in totality).
2. Wapo wenye kuhitaji msaada kiasi (partial).
3. Wapo wanaojitosheleza.
4. Wapo wenye ziada na hata tayari kusaidia wengine.

Serikali pia ipo.

Ni kweli kuwa haitakuwa kipindi cha starehe. Kitakuwa kipindi kigumu cha muda mfupi ambacho hata hivyo hakuna atakaye kufa kwa njaa au kukosa kabisa mahitaji muhimu katika kipindi hicho.

Mkuu kwa vile unaona pia kuwa si kuwa lockdown haifai, huoni pia kuwqa kama ikibidi (kwa nyakati zingine) katika kipindi hicho kushindia uji ni heri zaidi kuliko kuja kusambaratishwa na Corona bila jitihada za kutosha?
 
Mkuu nchi kama Rwanda si nchi ya magharibi.

Tunazo raslimali za kutosha tunaweza kujisimamia wenyewe kwa chakula kwenye hili gonjwa.

Wasiwasi wetu ni njaa mkuu?
Unazungumzia nchi yenye population ya 12 milioni Tanzania tuko takriban milioni 55
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom