JEKI
JF-Expert Member
- Aug 16, 2013
- 4,845
- 2,966
WanaJF, mwaka huu nimedhamilia kuweka kitu ndani, majiko ya kuazima yamenichosha, katika kampeni zangu za mwaka huu nimeamua kuanza kuwaandaa ndugu zangu juu ya ujio wa jiko la kisasa, jiko la mjeremani, siyo haya ya mchina. Kampeni yangu imeanzia kwa Bibi yangu ambaye kwa kweli ni moja ya watu muhimu kabisa katika maisha yangu na mtu aliyekata tamaa juu ya hatima yangu ya kuoa, nilipoonana naye nikamweleza kisha nikamwaga sifa juu ya hili jiko jipya la mjeremani, alichoniuliza ni hiki, umewahi kuniletea wengine ukawamwagia sifa lakini baadae ukaja kusema siyo, huyu naye si yatakuwa hayo hayo? Niliinamisha kichwa tu nisipate cha kujibu, kwa kuchechemea sana nikajibu, kwa kulinganisha na hao wa nyuma huyu naona ni bora zaidi.