HOJA Hoja kuhusu Muundo wa Uwanja wa Arusha Stadium

HOJA Hoja kuhusu Muundo wa Uwanja wa Arusha Stadium

Hoja ya Mdau inayopendekeza maboresho au mabadiliko ndani ya jamii, inayotakiwa kuangakiwa kwa mapana na Mamlaka husika
A

Anonymous

Guest
Huku Tanzania ikiendelea kujiandaa kwa ajili ya mashindano makubwa ya AFCON 2027, muundo wa Uwanja wa Arusha Stadium umeibua mjadala mzito miongoni mwa wadau na mashabiki wa soka nchini. Sababu kubwa ni uwepo wa njia kubwa ya riadha inayozunguka uwanja na kutenganisha wanja wa mchezo na majukwaa ya mashabiki.

Tukilinganisha na Uwanja wa Zanzibar Stadium unaojengwa Fumba Town, tofauti inaonekana wazi. Zanzibar Stadium imeundwa mahsusi kwa ajili ya mpira wa miguu pekee, bila njia ya riadha. Hii inaruhusu mashabiki kuwa karibu na wanja, hivyo kuleta hamasa, msisimko na shinikizo halisi la soka ambalo linahitajika wakati wa michuano mikubwa kama AFCON.
Uwanja Arusha.jpg
Uwanja Arusha1.jpg
Kwa upande mwingine, Arusha Stadium inaonekana kufuata mfumo wa Olympic Stadium kama vile vilivyo viwanja vya Benjamin Mkapa na New Amaan. Muundo huu unaweka umbali mkubwa kati ya pitch na mashabiki. Hoja inayotolewa ni kwamba uwepo wa running track ni uwekezaji wa muda mrefu ambao utasaidia michezo mingine kama riadha hata baada ya AFCON 2027.

Lakini hapa ndipo swali linatokea. Kenya ni nchi inayojulikana zaidi kwa riadha Afrika, lakini katika ujenzi wa uwanja wao mpya wa Talanta Stadium kwa ajili ya AFCON 2027, wameamua kutoa njia ya riadha. Pia tukitazama viwanja vikubwa kama vile vya Atlanta, vimejengwa maalum kwa ajili ya soka bila kuchanganya na riadha.

Hii inatufanya tujiulize, je ni sahihi kuendelea na mfumo wa viwanja vya michezo yote au ni wakati wa kuwa na viwanja mahsusi vya soka? Zaidi ya hapo, kwa nini wadau wa michezo, wataalamu na mashabiki hawakushirikishwa katika kupanga miundo hii tangu mwanzo? Tumekuwa tukiona Benjamin Mkapa ikiwa na running track, lakini ukweli ni kwamba asilimia kubwa ya watu wanaona hakuna manufaa makubwa yamepatikana kutokana na hilo kwa upande wa soka.

Kwa mtazamo wangu, tunapaswa kuweka kipaumbele kwenye soka kwanza wakati wa AFCON. Siku hizo chache za mashindano ndizo zitakazotangaza Tanzania duniani. Baada ya hapo tunaweza kujenga viwanja maalum vya riadha.

Je, wewe unaonaje? Je, viwanja vyetu vipya vya AFCON 2027 vinapaswa kuwa mahsusi kwa soka kama Zanzibar Stadium, au ni sawa tuendelee na mfumo wa michezo yote kama Arusha Stadium?
 
Umeshasahau matamasha ya viwanja vyetu 🤣🤣🤣🤣🤣

Hapo wanatega watu wa matamasha
 
Labda ni kwa sababu Arusha na Manyara ni chimbuko la wanariadha mashuhuri mfano Alfonce Simbu! Hivyo wanawaenzi kwa kuweka hizo njia kama sehemu ya kupromote huo mchezo.

Kinyume na hapo, hakukuwq na sababu uwanja wa mpira wa miguu kuwekwa hayo manjia.
 
Wapo sahihi, Arusha kuna wanariadha wengi tuu, simbu n mtu wa Singida ila amekulia Arusha na ndipo kituo chake cha mazoezi
 
Huwa nasikia uwanja wa mkwakwani Tanga ni football 100%
Nikurudi kwenye wazo lako,
Ni kweli watu wa serikalini hufanya kazi kwa mazoea sana...
Hayo maviwanja ya Olympic yamejaa nchi nzima.
Kulikuwa hakuna haja hiyo tena.
Isitoshe Riadha haina washabiki Tanzania.
Ni heri niangalie soka la wanawake kuliko riadha.
Kwa Tanzania after football, ni muziki na after music ni Boxing.
Faida nyingine ni kwamba viwanja vya football pure ni vigumu mno kwa visting teams.
 
Back
Top Bottom