Asha Abdala
JF-Expert Member
- Mar 21, 2007
- 1,130
- 44
Katika tamko la CHADEMA kuhusu siku 100 za kikwete madarakani, tamko ambalo lilichapishwa katika gazeti hili, Mwenyekiti wa chama hicho Mheshimiwa Freeman au mtu huru kama mashabiki wake wanavyo muita siku hizi, alitoa maneno mazito! Mmaneno mazito sana kuhusu dhana nzima ya wanamtandao dhidi ya hatima ya taifa, hatima ya Tanzania!
Freeman Mbowe alionyesha wasiwasi wake, na wa chama chake dhidi ya kundi hili na kwamba upo wasiwasi kuwa serikali inaongozwa na mifumo miwili inayofanya kazi sambamba, Freeman Mbowe alisema na namnukuu Kwa upande mwingine CCM kama chama kinaelekea kusogezwa pembezoni na badala yake maamuzi ya msingi kuhusu mwelekeo wa kiutawala yanaelekea kufanywa na kundi ambalo halitambuliki linalojiita wanamtandaoambalo muundo na kanuni zake haziko bayana hali inayoelekea kuigawa serikali na inaweza kutishia mwelekeo wa usalama wa nchi ambao unapaswa kuongozwa na mifumo ya kikatiba Alisisitiza kuwa Inapofika mahala wananchi wanaelezwa kuwa nchi inaongozwa na kundi fulani lisilo fahamika agenda zake, ni hatari kwa usalama wa taifa.Haya ni maneno mazito sana ambayo kimsingi serikali makini ilipaswa kutolewa ufafanuzi, serikali ilipaswa kuyatolea tamko!
Hata hivyo, katika hali ambayo haikutarajiwa na watu makini, Tofauti na Freeman, viongozi wengine wa upinzani wanaonekana kutojali hofu hiyo, hofu ya wanamtandao! Lakini ukitumia darubini, utabaini kuwa baada ya kukatwa miguu wote wasio amini katika uwanamtandao ndani ya CCM, hapana shaka kazi ya wanamtandao itabaki moja tu! Kukata miguu vyama vya upinzani.
Na hiyo ndio Hofu ya Freeman! Hofu ya Wanamtandao!!
Habari kamili bonyeza hapa: Hofu ya Wanamtandao! Kikwete, Mbowe Roho Juu!
Asha
Freeman Mbowe alionyesha wasiwasi wake, na wa chama chake dhidi ya kundi hili na kwamba upo wasiwasi kuwa serikali inaongozwa na mifumo miwili inayofanya kazi sambamba, Freeman Mbowe alisema na namnukuu Kwa upande mwingine CCM kama chama kinaelekea kusogezwa pembezoni na badala yake maamuzi ya msingi kuhusu mwelekeo wa kiutawala yanaelekea kufanywa na kundi ambalo halitambuliki linalojiita wanamtandaoambalo muundo na kanuni zake haziko bayana hali inayoelekea kuigawa serikali na inaweza kutishia mwelekeo wa usalama wa nchi ambao unapaswa kuongozwa na mifumo ya kikatiba Alisisitiza kuwa Inapofika mahala wananchi wanaelezwa kuwa nchi inaongozwa na kundi fulani lisilo fahamika agenda zake, ni hatari kwa usalama wa taifa.Haya ni maneno mazito sana ambayo kimsingi serikali makini ilipaswa kutolewa ufafanuzi, serikali ilipaswa kuyatolea tamko!
Hata hivyo, katika hali ambayo haikutarajiwa na watu makini, Tofauti na Freeman, viongozi wengine wa upinzani wanaonekana kutojali hofu hiyo, hofu ya wanamtandao! Lakini ukitumia darubini, utabaini kuwa baada ya kukatwa miguu wote wasio amini katika uwanamtandao ndani ya CCM, hapana shaka kazi ya wanamtandao itabaki moja tu! Kukata miguu vyama vya upinzani.
Na hiyo ndio Hofu ya Freeman! Hofu ya Wanamtandao!!
Habari kamili bonyeza hapa: Hofu ya Wanamtandao! Kikwete, Mbowe Roho Juu!
Asha