Wahusika wamekuwa wakitengeneza hadithi mbalimbali kuuhadaa umma, lakini ukweli ni kwamba watawala wana hofu ya nchi kuwekewa vikwazo vya kuuza dhahabu nje kutokana na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu unaofanywa na utawala wa Samia.
Kwa kuwa madini ya Dhahabu na Almasi, kutokana na kuwa na thamani kubwa, na kuwa yamekuwa yakitumika kujenga kiburi cha serikali nyingi za kidikteta Duniani, vikwazo vinavyozuia ununuzi wa madini kutoka mataifa yenye ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu, mara nyingi imetumika kama nyundo ya kwanza kwa tawala za kidikteta.
1. Huko Afrika ya Kati, nchi iliwekwa kwenye vikwazo vya kutokuuza almasi nje kwa miaka 11, vimeondolewa mwaka 2024.
2. Huko Sierra Leone, kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe, mwaka 2000 Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa liliweka vikwazo vya mataifa yote kutonunua almasi ya Sierra Leone.
3. Liberia, mwaka 2001, Umoja wa Mataifa uliweka vikwazo vya kuzuia almasi ya Liberia kuuzwa mahali popote Duniani, baada ya kuthibitika kuwa Liberia ilikuwa inasavidia vikundi vya waasi nchini Sierra Leone.
4. Hapo Angola, mwaka 1998, Umoja wa Mataifa uliwekea vikwazo almasi za Angola kwa sababu ya uwepo wa kundi la UNITA.
5. Pia almasi ya Ivory Coast iliwahi kuwekewa vikwazo tangu mwaka 2005 mpaka 2014.
6. Venezuela, mwaka 2018, Marekani iliweka vikwazo vya kuzuia mauzo ya dhahabu kutoka Venezuela kutokana na utawala wa Maduro kugandamiza haki za wananchi.
7. Nicaragua, mwaka 2022, utawala wa Ortega Murillo uliwekewa vikwazo vya kutokuuza dhahabu yake nje kutokana na serikali yake kukiuka haki za binadamu.
Ikumbukwe kuwa Jumuia ya Madola iliipa Serikali ya Tanzania mpaka mwezi wa March 2026, iwe imetoa ushirikiano kwa Jumuia ya Madola kuunda tume huru kuchunguza mauaji yaliyofanywa na utawala wa Samia Oct 29, mwaka 2025. Jumuia ya Madola ilimteua Rais mstaafu wa Malawi kuwa mwenyekiti wa Tume hiyo, lakini utawala wa Samia, bila ya kutoa kauli, lakini kivitendo, uliigomea Tume hiyo. Na Jumuia ya Madola ikasema inaupa utawala wa Samia muda mpaka mwezi wa Machi 2026. Na kama utawala wa kidikteta wa Tanzania utakuwa bado umekaza shingo, kikao cha Jumuia ya Madola kitakachofanyika March 2026, kitatoa Azimio dhidi ya utawala wa Samia.
Bila ya kuweka wazi, utawala wa Samia umeamua kuuza haraka akiba ya dhahabu ili kuepuka dhahabu hiyo kuwa mawe yasiyo na msaada, kama vikwazo vitakavyowekwa vitahusisha kuzuia mauzo ya dhahabu yetu nje ya nchi.
Na kama itatokea tukawekewa vikwazo vya mauzo ya dhahabu nje, tumekwisha. Baada ya utalii kudorora, chanzo kikuu pekee cha pesa ya kigeni kilichobakia ni mauzo ya dhahabu.
Hofu ha kuwekewa vikwazo na mataifa ya Ulaya, vimemfanya Kombo kuhamia Ulaya, akijaribu kutumia kila mbinu anazofikiria zinaweza kuiokoa Serikali ya Muuaji. Huku kuna ICC inayoenda na mtazamo wa kisheria, kwa uoande mwingine kuna mataifa yanayojipanga kuvhukua hatua za kuudhibiti utawala hafamu kwa diplomasia ya siasana uchumi.
Hapa anachofanya Kombo ni kutaka kuzuia mti ambao majani yake yanakauka kwa kuyapaka maji majani wakati ardhi ni kavu kabisa, haina maji. Kwenye hili, Watanzania ndiyo ardhi na ndiyo shina la mti unaokauka. Anahangaika nje(majani), huku nyumbani (udongo na shina), wenzake wanaendelea kuteka watu, kubambikia watu kesi, na kuendelea kuwatesa watu magerezani wasio na hatia! Lazima uwe mjinga mzoefu kuamini kuwa atafanikiwa anayoyafanya kupitia hizo mbinu mfu.
Kwa kuwa madini ya Dhahabu na Almasi, kutokana na kuwa na thamani kubwa, na kuwa yamekuwa yakitumika kujenga kiburi cha serikali nyingi za kidikteta Duniani, vikwazo vinavyozuia ununuzi wa madini kutoka mataifa yenye ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu, mara nyingi imetumika kama nyundo ya kwanza kwa tawala za kidikteta.
1. Huko Afrika ya Kati, nchi iliwekwa kwenye vikwazo vya kutokuuza almasi nje kwa miaka 11, vimeondolewa mwaka 2024.
2. Huko Sierra Leone, kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe, mwaka 2000 Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa liliweka vikwazo vya mataifa yote kutonunua almasi ya Sierra Leone.
3. Liberia, mwaka 2001, Umoja wa Mataifa uliweka vikwazo vya kuzuia almasi ya Liberia kuuzwa mahali popote Duniani, baada ya kuthibitika kuwa Liberia ilikuwa inasavidia vikundi vya waasi nchini Sierra Leone.
4. Hapo Angola, mwaka 1998, Umoja wa Mataifa uliwekea vikwazo almasi za Angola kwa sababu ya uwepo wa kundi la UNITA.
5. Pia almasi ya Ivory Coast iliwahi kuwekewa vikwazo tangu mwaka 2005 mpaka 2014.
6. Venezuela, mwaka 2018, Marekani iliweka vikwazo vya kuzuia mauzo ya dhahabu kutoka Venezuela kutokana na utawala wa Maduro kugandamiza haki za wananchi.
7. Nicaragua, mwaka 2022, utawala wa Ortega Murillo uliwekewa vikwazo vya kutokuuza dhahabu yake nje kutokana na serikali yake kukiuka haki za binadamu.
Ikumbukwe kuwa Jumuia ya Madola iliipa Serikali ya Tanzania mpaka mwezi wa March 2026, iwe imetoa ushirikiano kwa Jumuia ya Madola kuunda tume huru kuchunguza mauaji yaliyofanywa na utawala wa Samia Oct 29, mwaka 2025. Jumuia ya Madola ilimteua Rais mstaafu wa Malawi kuwa mwenyekiti wa Tume hiyo, lakini utawala wa Samia, bila ya kutoa kauli, lakini kivitendo, uliigomea Tume hiyo. Na Jumuia ya Madola ikasema inaupa utawala wa Samia muda mpaka mwezi wa Machi 2026. Na kama utawala wa kidikteta wa Tanzania utakuwa bado umekaza shingo, kikao cha Jumuia ya Madola kitakachofanyika March 2026, kitatoa Azimio dhidi ya utawala wa Samia.
Bila ya kuweka wazi, utawala wa Samia umeamua kuuza haraka akiba ya dhahabu ili kuepuka dhahabu hiyo kuwa mawe yasiyo na msaada, kama vikwazo vitakavyowekwa vitahusisha kuzuia mauzo ya dhahabu yetu nje ya nchi.
Na kama itatokea tukawekewa vikwazo vya mauzo ya dhahabu nje, tumekwisha. Baada ya utalii kudorora, chanzo kikuu pekee cha pesa ya kigeni kilichobakia ni mauzo ya dhahabu.
Hofu ha kuwekewa vikwazo na mataifa ya Ulaya, vimemfanya Kombo kuhamia Ulaya, akijaribu kutumia kila mbinu anazofikiria zinaweza kuiokoa Serikali ya Muuaji. Huku kuna ICC inayoenda na mtazamo wa kisheria, kwa uoande mwingine kuna mataifa yanayojipanga kuvhukua hatua za kuudhibiti utawala hafamu kwa diplomasia ya siasana uchumi.
Hapa anachofanya Kombo ni kutaka kuzuia mti ambao majani yake yanakauka kwa kuyapaka maji majani wakati ardhi ni kavu kabisa, haina maji. Kwenye hili, Watanzania ndiyo ardhi na ndiyo shina la mti unaokauka. Anahangaika nje(majani), huku nyumbani (udongo na shina), wenzake wanaendelea kuteka watu, kubambikia watu kesi, na kuendelea kuwatesa watu magerezani wasio na hatia! Lazima uwe mjinga mzoefu kuamini kuwa atafanikiwa anayoyafanya kupitia hizo mbinu mfu.
