Johnny Sack
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 9,144
- 19,690
Ok mimi sio mwanachama wa CHADEMA, ila Mbowe alikaa muda mrefu sana gerezani hata kama alitoka.. Yaania alipokamatwa CHADEMA wangetakiwa kuonyesha reaction kubwa sana sio mtandaoni tu bali na mtaaniSipingi utetezi wako boss, na tunajua uchochezi wanaofanya sukuma gang ili kumfanya Magufuli abaki relevant. Je Mbowe hakutamka maneno ya watu kuandamana tena katika hali ya kuonyesha kutokukubaliana nayo? Ni mara moja au mbili Mbowe aliwahi kuhamasisha watu kuandamana huko nyuma?
Unataka watu waandamane kisa Mbowe kukamatwa, au kila mtu ahudhurie kesi ya Mbowe. Kwani kila mfuasi wa CDM aliyekamatwa Mbowe aliandamana au kuhudhuria kesi zao? Alipokuwa anatumia gari la umma na kupata mshahara wa ubunge na KUB, watu walikuwa wanamfuata na kufaidi alichofaidi? Walioweza kuhudhuria kesi ya Mbowe walihudhuria kutokana na nafasi zao, na mahali kesi ilipokuwa ikiendeshwa. Labda kama ulitaka wafuasi wote wa CDM waende hapo mahakamani.
Wote tunajua Samia ni tofauti na Magufuli, ila anachofanya Mbowe sasa ni kujiweka upande wa kujinyenyekeza zaidi kuliko kukaa eneo la kupata haki. Kuna mazingira makubwa Samia akamtumia sasa ili kutawala kwenye kipindi chake bila pressure kubwa. Lakini akitoka mambo yakaendelea vile vile. Tunachokataa ni Mbowe kutaka kujionyesha kwa serikali kuwa yeye ni mnyenyekevu, lakini wafuasi wa CDM ndio wenye tatizo. Kwa sasa Mbowe ushawishi wake uko chini, ni vyema akaacha wengine waongee kwani bado tuna imani nao. Mbowe ale alichopewa sio kulazimisha kuburuza watu huko atakako.
Kesi yake ilipokuwa inaendeshwa wangekuwa wanahudhuria hata watu 10,000 tu kushinikiza aachiwe na hata kama polisi wangewazingua wasingeweza kukabiliana nao, Mbowe asingemaliza hata mwezi gerezani angeachiwa, Polisi hawawezi kuua watu 10,000 wala kuwapeleka mahabusu, maana hazitatosha. na wangewajaribu kukabiliana nao hiyo ingekuwa ni aibu klubwa sana kwa Samia na angemuachia tu
Na sio lazima kiongozi aitishe maandamano, wanachama wanaojiongeza wakiona kiongozi wao au mwanchama wa kawaida tu anafanyiwa injustice wanajiongeza wenyewe kushinikiza hiyo injustice ikome haraka iwezekanavyo
Sasa unaposema na yeye kwani wanachama wanapokamatwa hakuhudhurii kesi zao, mbona anahudhuria nyingi tu, Sugu alipokamatwa, Mdude alipokamatwa, Lema na wanachama wengine Mbowe alikuwa akiwatembelea gerezani.
Alipokamatwa kama watu wangekuwa wakitia pressure aachiwe pale mahakamani ile kesi wala isingeedelea kwa muda mrefu ville
Unaposema mshahara wake sijui na gari lake alilopewa akiwa KUB hamkugawa, hapa ndio nakuona empty set tu, sasa Mbowe alikuwa hachangii chama? Mbowe amepoteza biashara zake kiasi gani kutokana na msimamo wake wa kisiasa? Hakuharibiwa mashamba yake kule Hai? hakubomolewa jengo la Bilcnas Dar? Account zake za benki hazikufungwa? yaani haya hayatoshi inatakiwa tena awe anawagawia mshahara? Na ni kiongozi wa chama gani ambaye anagawa gari na mshahara kwa wanachama?
Hivi jamaa angeamua kuungana na CCM na kutumia connection hizo kuomba favour kwa biashara zake kwani kuliko kutegemea huo mshahara wa KUB na gari ni ipi ingekuwa bora zaidi kwake kifedha?