Hizi ndio dalili za serikali ya Magufuli kushindwa? Au tuendelee kuwapa muda?Nimeamka asubuhi natoka

Judi wa Kishua

JF-Expert Member
Apr 15, 2012
1,066
1,047
Nimeamka asubuhi natoka kuelekea kazini. Nimefika kituoni nikakuta daladala imesimama inapakia abiria huku ikiwa tayari imejaa, nikaitwa nipande nikakumbuka AMRI ya serikali kwamba ni marufuku kusimamisha abiria.

Sikupanda nikasubiria nyingine nikazunguka nayo ndani ya daladala abiria tumejaa watu wamesimama hakuna ata pa kuweka mguu. Tunapita barabarani askari wa barabarani wanatutazama tofauti na nilivyohofu kwamba nikikutwa nimesimama nitapigwa faini na wala sioni anayejali.

Nafika ofisini nakuta magazeti tayari yameshafika naona vichwa vya habari waganga wa tiba asili wameigomea serikali na wanamkanya Waziri wa serikali aache kutaka sifa so hawapo tayari kutekeleza amri ya serikali, nikapekua habari iliyoandikwa ukurasa wa juu ya gazeti la mwananchi inaonyesha namna awa waganga wanavyotapeli wananchi..

Kwa habari hiyo ya uchunguzi inaonyesha kifaa ambacho kinatiliwa shaka kinauwezo wa kuchunguza mwili wa binadamu bila kuchukua damu wala kitu chochote mwilini na kutoa majibu ndani ya dakika tatu. Mwandishi kama sehemu ya uchunguzi anaonekana ana tatizo la ugumba ilihali ana watoto tayari alikuwa anawajaribu.

Nilishikwa na ganzi baada ya kusoma hiyo habari nikabaki najiuliza huu ujasiri wa kuigomea serikali wanautoa wapi? Na wanafanya utapeli kama huu bila woga?

Muda wa kazi ukafika tukaanza kufanya kazi ghafla nikakumbuka AMRI ya Waziri wa kazi kwa wafanyakazi wanaofanya bila vibali baada ya kumuona mfanyakazi mwenzangu kutoka Kenya akiendelea na kazi bila wasiwasi wowote na ukweli ni kwamba anafanya kazi bila ya vibali kuangalia around ofisi yote nakuta wale wakenya waliokuwa wanafanya kazi bila vibali bado wapo na hawana uoga wowote na boss wala hashtuki kuwatafutia vibali wapo zaidi ya ishirini(kumbuka deadline ya serikali imeshapita) .

Ndipo nikaanza kupatwa na hofu inamaana awa mawaziri wanapotoa matamko na maelekezo mbona yanapuuzwa? Wasiposikilizwa leo ni lini watasikilizwa? Tatizo ni maagizo hayatekelezeki au watanzania hawapo tayari kwa changes? Au mawaziri hawakujipanga kusimamia utekelezaji? Au Magufuli yupo ahead of time ambapo watanzania awako tayari kufika kwa sasa bado wanataka kufurahia comfort zone?

Sina mashaka kabisa na Magufuli katika kusimamia mambo yake sababu ana historia hiyo ila nimeanza kupata mashaka na mawaziri kama haya mambo ya kusimamia taratibu wataweza au wanajilazimisha ila hawawezi.

Ni hayo tu, kazi njema!
 
Hata mimi nashangaa wahindi wanakula bata kama hamna tamko lolote limetolewa!!!

Halafu hawa uhamiaji waache unafiki!!! Wenyewe ndio wamewapa vibali then wanatuambia tuwapelekee taarifa:confused:

Uhamiaji ni jipu!!!:rolleyes:
 
CCM NI ILE ILE OOOH NI ILE ILEEE...... Naimba tu nipo out of topic.

But wat i kno iz busines as usual
 
Ni kweli mkuu wangu leo nimepita Serena waKenya wamejana utadhani tuko Kibera,nikachomokea Sopa waHindi Kenya wamejaaa tele kauli ya waziri ilikuwa kick ya kutokea haina mashiko hata kidogo wafanyakazi wageni wamehjana Tanzania utadhani nchi hii haina mwenyewe.
 
Serikali sawa na mbwa koko, inabweka tu bila kung'ata. Tukianzia kwenye makontena,wakwepa kodi, wafanyakazi haramu, daladala etc. Hamna kitu hapa. Swagger tu za kwenye vyombo vya habari. Nao pia wameisha wachoka
 
Tatizo lipo kwa hawa mawaziri wanaofanya kazi kwa mtindo huu
ImageUploadedByJamiiForums1451291375.250394.jpg
 
Mwananchi we ndio WA kwanza kutekeleza...sasa kama ninyi mnapanda ukijua fika kuwa gari imejaa halafu utake polisi wajuukize?..vitu vingine ni sisi kwanza ndio maana iliomba tumuunge mkono...sasa ninyi badala ya kukataa kupanda daladala iliyojaa...mnapanda halafu mnakuja kutoa lawama kwa magufuli kweli!!!!!??...kama msomi una akili hii VP wale wenzangu na mm mule kakonko?
 
Ukis
Mwananchi we ndio WA kwanza kutekeleza...sasa kama ninyi mnapanda ukijua fika kuwa gari imejaa halafu utake polisi wajuukize?..vitu vingine ni sisi kwanza ndio maana iliomba tumuunge mkono...sasa ninyi badala ya kukataa kupanda daladala iliyojaa...mnapanda halafu mnakuja kutoa lawama kwa magufuli kweli!!!!!??...kama msomi una akili hii VP wale wenzangu na mm mule kakonko?
ukisema daladala zisisimamishe miji kama Dar ,basi watu watafika kazini saa 7 mchana na watarud kwao saa 9 alfajiri
 
Ya dala dala kusema kweli kuliko hakuna uhalisia.
Mmoja nauli inayolipwa haiwezi kuiweka gari barabarani kama haitasimamisha abiria.

Na tatizo la msingi ni foleni na maana hiyo ni kuwa Gari haiwezi kufanya safari ya kutosha kwa siku iliiweze kulipa/faida.

Pili-mahitaji /abiria ni wengine kuliko uwezo wa Daladala zilizopo na hili halinaubishi-sasa tuache kuuza sura badala yake tufanye kazi kwa kuishi kwa uhalisia.

Kwanza Ndani ya City magari ya abiria yawe ni magari ya uwezo wa abiria 65 na kuendelea!
Pili Maboresho ya Barabara yafanyike kila kona!
Tatu ilikupunguza Foleni utaratibu kama wa Boda Bora kwa Magari uanzishwe pamoja na kwamba zoezi la Boda Boda kutukufika katikati ya mji eti kuogopa ujambazi ilikuwa kichekesho na ubaguzi uliopitiza kwa wenye kipato kidogo.

Kwa hiyo namna Bora kuwe na ushuru kwa Vyombo Moto vya watu Binafsi vyote vinavyoingia i.e Kila siku 2500/= ukitaka kuingia na gari lako Mjini. kwa utartibu huu baadhi ya Watu wataacha kuja na magari yao Mjini na hivyo kupunguza Foleni.
 
Hilo dogo mengi makubwa yanakujaaa mawaziri wengi wana mbwembwe kama myweather
 
Judi wa Kishua, hii serikali inaendeshwa kwa kila mwenye dhamana kutoa amri yake bila watekelezaji kufuatilia, kwa maana askari wa kusimamia sheria, duu, usanii mtupu
 
Judi wa kishua ,jina lako mwenyewe hulitendei haki ,umeamua tu kutuonea wapanda daladala wakati wewe kazini umeenda na INFINITY QX 90 ,
 
Waingereza wao wanafanya hivyi kuondokana na tatizo la watu wanaofanya kazi bila vibali. Ushauri wangu ni kuangalia jinsi ya kuwatoza faini kubwa haya makampuni yanayokaidi agizo la wizara. Ila pia kuwepo na task force ambayo itakua inaenda kwenye maeneo ambayo wanadhani kuna wafanyakazi wanafanya kazi bila vibali. Pia kuwepo na number za simu/website ya watu kutoa taarifa za watu wanadhani wanaweza kuwa wanafanya kazi bila vibali.


Penalties for employing illegal workers


You can get a fine (also known as a civil penalty) of up to £20,000 per person for employing illegal workers.

Illegal workers include:

  • students with expired visas, or students working more hours than they’re allowed to
  • people who work on a visitor’s visa
If you’re caught employing an illegal worker
You’ll get a ‘referral notice’ to let you know that:

  • your case is being considered
  • you may get a civil penalty of up to £20,000 for each illegal worker
You won’t have to pay a civil penalty if you can show you made the correct ‘right to work’ checks.

You’ll be sent a ‘civil penalty notice’ if you’re found liable and you’ll have 28 days to respond.

The penalty notice will give you your payment options and tell you what do next. It will also tell you how to object to the civil penalty. You can then make an appeal.

Your business’s details may be published by Immigration Enforcement as a warning to other businesses not to employ illegal workers.
 
Back
Top Bottom