Mwanongwa
JF-Expert Member
- Feb 15, 2023
- 866
- 805
Habari ndugu zangu, hivi huu utaratibu wa kuwaweka kambi Wanafunzi waliyokwenye Vidato vya mitihani nani ameuleta?
Maana umekuwa ni mradi kwa baadhi ya Walimu wa Shule hasa za Serikali.
Kuna shule moja Jijini Mbeya inaitwa ITIJI SECONDARY inapatikana Kata ya ITIJI ni Shule ya Kata imekuwa na utaratibu mbaya kwa Wanafunzi wa vidato vya mitihani, yaani mahitaji kwa mwezi ni mengi balaa.
Mfano Mtoto anatakiwa kila mwezi kupeleka vitu vifuatavyo:
1. Debe Moja la mahindi
2. Shilingi 48,000
3. Sukari kilo Moja
4. Ndonya saba za maharage
5. Ndonya nne za mchele
6. Pakiti moja ya chumvi
Jambo la kushangaza hayo mahitaji ni kila mwezi na hiyo Shilingi 48,000 wanadai ni kwa ajili ya Mbogamboga na matunda lakini Wanafunzi hawapati hizo mboga na hayo matunda.
Pia, wali wanakula mara moja kwa wiki, sasa je, kuna Mwanafunzi anayepewa ndonya moja kwa mlo mmoja?
Wanadai pesa ya maji na umeme, inamaana shule haina bajeti ya maji na umeme kutoka Serikalini hadi walipe Wanafunzi?
Hii imekuwa kero sana kwa Wazazi na Walezi.
Pia soma ~ Wanafunzi madarasa ya mitihani (Bukoba Vijijini) wanaacha shule kwa kukosa michango ya kambi ya maandalizi
Maana umekuwa ni mradi kwa baadhi ya Walimu wa Shule hasa za Serikali.
Kuna shule moja Jijini Mbeya inaitwa ITIJI SECONDARY inapatikana Kata ya ITIJI ni Shule ya Kata imekuwa na utaratibu mbaya kwa Wanafunzi wa vidato vya mitihani, yaani mahitaji kwa mwezi ni mengi balaa.
Mfano Mtoto anatakiwa kila mwezi kupeleka vitu vifuatavyo:
1. Debe Moja la mahindi
2. Shilingi 48,000
3. Sukari kilo Moja
4. Ndonya saba za maharage
5. Ndonya nne za mchele
6. Pakiti moja ya chumvi
Jambo la kushangaza hayo mahitaji ni kila mwezi na hiyo Shilingi 48,000 wanadai ni kwa ajili ya Mbogamboga na matunda lakini Wanafunzi hawapati hizo mboga na hayo matunda.
Pia, wali wanakula mara moja kwa wiki, sasa je, kuna Mwanafunzi anayepewa ndonya moja kwa mlo mmoja?
Wanadai pesa ya maji na umeme, inamaana shule haina bajeti ya maji na umeme kutoka Serikalini hadi walipe Wanafunzi?
Hii imekuwa kero sana kwa Wazazi na Walezi.
Pia soma ~ Wanafunzi madarasa ya mitihani (Bukoba Vijijini) wanaacha shule kwa kukosa michango ya kambi ya maandalizi