mchajikobe
JF-Expert Member
- Aug 14, 2009
- 2,652
- 1,238
Hii imenifanya niamini kuwa hapa Tanzania hakuna umuhimu wa elimu,sababu wengi waliobarikiwa kuipata hawaitumii matokeo yake wanayoyafanya ni aibu na dharau kwa taifa kwaujumla.Embu fikirieni wana JF katika mitaa ya kinondoni kuna baadhi ya watu walikuwa wanauza maji kwa watu wa mikokoteni,baada ya kampeni ya DAWASCO ya kutupatia maji wakazi wote wa jijini,kweli maji tuliyapata na tulishukuru kwa hilo,lakini kinachoshangaza ni kwamba hawa DAWSCO badala ya kuwadhibiti hawa wanaouza maji bila vibali,walichokifanya ki kukatisha huduma ya maji kwa wananchi wote wa maeneo haya,sasa huu kama sio ukichaa ni nini?Wanatakiwa wajue kuwa watu wanalipia ankara zao hivyo wanastahili huduma hii!!