Hivi unafahamu siku moja utakufa?

Hivi unafahamu siku moja utakufa?

Mto_Ngono

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2017
Posts
686
Reaction score
589
Binadamu udongo siku moja utarudi mavumbuni wengi wetu tunavyoamini. Sitaki kuandika mambo mengi swali kwa mwana JF, Hivi unajua siku moja utakufa? Je hali hiyo ya kujua kwamba utakufa (sense of death) inakuathirije katika maisha yako? Je ungependa ufanye nini au mambo yapi kabla hujafa? Je ingelikuwa ni hiari yako ungeomba kuendelea kuishi?
 
najua siku ntakifa sababu hakuna binadamu aloandikiwa kuwa hai milele duniani

hali ya kujua kwanba siku ntakufa hainipi shida wala hainiathiri kivyovyote cz ndo utaratibu ulipo..ni must kwa kila kiumbe alichoumba muumba.

ningependa kusaidia walio katika shida...maskini wagonjwa na wajane..na watu waliotengwa na jamii na yatima.lakini sina uwezp.
ipo siku.
lasltly kumuomba muumba anisamehe nlipomkosea .na kusamehe walionikosea

kila mtu angepemda kuendelea kuishi..but kama yuko kwenye point of no return...hakuna namna.
 
Ninafaham kwamba siku yaja na muda usio na jina, nitakufa.
Lakini sitaki kufikiria kuhusu kufakufa
 
Najua kuwa ipo siku na saa nitaitwa al marhum R Mbuna na yote niliyoyafanya yatafutika katika uso wa dunia isipokuwa matendo yenye kuendelea.

Sijali hata nikifa sasa hivi naamini watoto wangu hata nikifa leo kwa uwezo wa aliyewaleta duniani wataendelea na maisha kwa kadri alivyowakadiria. Sina uwezo wa kubadilisha lolote katika maamuzi ya na siku ya kifo changu.
 
Siogopi kufa.naogopa kuoza.

Sent from my TECNO-Y4 using JamiiForums mobile app
 
Aisee huwa nawaza sana ila kila nikiwaza wanaonizunguka amani inapotea kabisa.

Ila ndio hivyo hakuna jinsi kwa sababu kifo kipo na tutakufa tu.
 
moja ya dalili ya wacha Mungu ni kukumbuka kuwa kifo kipo.ukifikilia kifo basi kuna kitu kinakuijia ndani ya nafsi je huko nakoenda nimejipanga,je nakufahamu.bila shaka utatubia, hiyo ni moja ya sign ya wacha Mungu
 
tufanye mema tu kifo kipo

Sent from my GT-I9300 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom