Hivi ukiwa dereva wa Noah, lazima uwe mpuuzi?

Hivi ukiwa dereva wa Noah, lazima uwe mpuuzi?

mambomoto

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2011
Posts
326
Reaction score
238
Jamani tumekaa mjini na vijijini na magari tumeyamiliki na barabara tunazotumia hi hizi hizi ila kinachonishangaza ni hawa wenzetu wenye kutumia magari aina ya Noah.

Yaani ni kero kwa uendeshaji wao utafikiri wamelogwa. Uendeshaji wa hovyo usiokuwa makini speed hazina umakini wowote ili mradi tu anakimbia.

Yaani naona madereva wote wa magari ya Noah ni wapuuzi watupu ile mjini au mkoani tabia zinafanana.
 
Kiufupi Noah ni daladala fujo za daladala ndio sawa na fujo za Noah
 
Sijui wanajiona wako kwenye mabasi ya mkoa..., wanaendesha kama wamerogwa vile..
 
Mkuu kama ulikuwepo mida ya mchana leo mwenye NOAH kanirushia maji machafu mimi nilikuwa napita kando ya barabara ya mtaani.
 
Mimi nina noah na ninaendesha vizuri ila kinachonisikitisha ni kusimamishwa na mateja ili kupakia abiria. ... Yaani ni kama masichana mzuri kila akipita hupigiwa miluzi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom