kyagata
JF-Expert Member
- Oct 18, 2016
- 6,568
- 12,669
Hapo ni kwako au kwa mama ntilie?Aisee,
Imenitokea usiku huu,mda huu wakuu.
Nmetoka kazn na njaa sana, wife akanambia msosi tayari ila nianze na starter ya supu ya kuku kabisa, Kisha ndo nifate wali.
Nikamwambia Safi Sana,
Niwekee supu ya firigisi Kabisa.
Unajua mwnyw nnavoipenda Sana.
Kweli nmepakuliwa nmekula fresh.
Katikati Nmeshakula tayari, Wife ndo ananambia kua kuku (tetea) aliechinjwa ndo yule ambae kifaranga wake alikufa kwa kung'atwa na nyoka jana usiku, aliponipigia sim kunijulisha leo asbh kua Kuna kifaranga kang'atwa na nyoka kafariki.
Jana jioni shemej yangu (mdg wake wife) Akifata mkaa stoo,ile anafunua kiroba cha mkaa, nyoka mweusi kadondoka pembeni na Katoka mbio na kukimbilia Banda la kuku, wakaogopa kumfata,ukzingatia Giza lishaingia. (Banda la kuku na stoo ya mkaa vimetenganishwa na mabanzi TU)
Anasema asbh kulipokucha wamewafungulia kuku, nyoka hawajamuona bandani, ila kifaranga mmoja wamekuta kafariki, wakamtoa na kumtupa.
MDA mfupi tena baadae mama ake kifaranga aliefariki (tetea), wakaona Kama nae kanyong'onyea sn hachangamki,Wakihisi nae keshang'atwa tayari, anaweza kufariki MDA wowote ule.
Kwahiyo ikabidi achinjwe haraka sana kabla hajafariki na kumpika.
Sasa wakuu,
Hapa sio Siri Moyo wangu umeenda mbio Sana, nmejawa na woga sana.
wataalam na wazoefu kwenye hili,
Naombeni ufafanuzi wenu tafadhali
View attachment 2641976