demokrasia
Member
- Apr 6, 2011
- 52
- 5
Habari zenu wana JF? Hivi hii tabia ya serikali kuchelewesha mishahara ya watumishi wa umma inasababishwa na nini? Leo ni tarehe 2 lakini kila nikienda kwenye akaunti sikuti chochote. Au serikali yetu ndio inafilisika? Lakini mbona serikali imeweza kuwaongezea wabunge posho za vikao kwa asilimia 150% kutoka sh. 70,000/= hadi sh. 200,000/= kwa kila kikao? Kwa nini inashindwa kuwalipa watumishi wa Umma mishahara yao kwa muda unaotakiwa? Hivi serikali ni kwa nini inafanya maamuzi kisiasa badala ya kufanya maamuzi kwa kuzingatia utaalamu? Hii nchi mambo hayaendi vizuri kwa sababu serikali inaingiza siasa kwenye kila jambo. Wananchi tunateseka sana na hii Serikali. Maisha ni magumu sana. Hii miaka minne iliyobaki, kwa kweli cha moto tutakiona.