fikirini
Senior Member
- May 24, 2011
- 114
- 22
Wana Jf, imenitokea mara kadhaa na nimekuwa nikijionea pia kwa rafiki zangu wa karibu....mwanaume ukishaanzisha tu uhusiano na mwanamke, basi mwanamke ndo anakuwa wa kwanza kutoa masharti mara oooh mimi nina wivu ole wako nikukute na mtu mwingine, oooh muda wowote nitakupigia simu na ole wako usipokee, mara oooh uko wapi, upo na nani, unafanya nini, mbona hujaniaga? yote haya ni masharti tu...........jamani kwangu mimi ni kero, hii inamaanisha wanaume hatujui mahusiano yaweje? au wanawake wa aina hii ndo wanafanya hivyo ili kujilinda na tabia zao mbaya za kutotulia na mtu mmoja? nawasilisha