Hivi ni sawa kwa Chombo cha Habari kufungiwa kutoa huduma?

Ibumalo

JF-Expert Member
Mar 19, 2017
462
491
Hili ni swali fikirishi. Tumeshuhudia mara kadhaa Vyombo vya Dola (TCRA, SERIKALI) vikitoa adhabu ya kuvifungia kutoa huduma vyombo vya habari pale vinapokiuka taratibu hata pengine sheria. Tumeshuhudia hivyo kwa gazeti la Mwananchi, gazeti la Tanzania Daima na hivi majuzi kituo cha TV cha Wasafi.

Swali la kujiuliza ni mamlaka zinapofanya hivyo zinamlenga nani na na anaumia katika kutoa hiyo adhabu. Kanuni moja ya msingi ni kuwa adhabu itolewe na kumwathiri aliyetenda kosa. Chombo cha habari kinapofungiwa kutoa huduma anayeathirika siyo mmiliki wa chombo pekee.

Wafanyikazi, familia zao watoa matangazo na wapata huduma mbalimbali. Hao wote wanaadhibiwa kwa kosa ambalo hawakuhusika moja kwa moja. Napendekeza mamlaka zibuni adhabu zitakazomuathiri mtenda kosa bila kuwagusa wasio na hatia.

Nawakilisha.
 
Wewe chukulia mfano kwa wale wengin waliofungiwa hap awal akiona mwenzie hajafungiwa unaona itakua haki.etyy
 
Wewe ni mjinga, kuwa chombo cha habari haina maana kuwa unajiamulia unalotaka.

Kuna kanuni na miongozo ya kuendesha chombo chako, ukikiuka hiyo miongozo utafungiwa tu.
 
Wewe ni mjinga, kuwa chombo cha habari haina maana kuwa unajiamulia unalotaka.

Kuna kanuni na miongozo ya kuendesha chombo chako, ukikiuka hiyo miongozo utafungiwa tu.
Jibu hoja hapa anaeumia ni nani mwenye chombo na wahariri wake au wafanyikazi wa ngazi za chini pamoja na waandishi wa habari ambao hawakushiriki kwenye kuandaa na kurusha habari iliyosababisha chombo kiadhibiwe?
 
Back
Top Bottom