Habari wakuu, kuna jambo nimelisikia mara kadhaa watu wakisema, kuwa kuna baadhi ya wanyama au ndege ukiwagonga wapo ambao unashitakiwa na wapo ambao hakuna kesi ila kibinadamu unamalizana tu na mmiliki.
Kwa mfano ukigonga bata au kondoo, hapo kesi ipo na itafika mbali.
Ila kama utamgonga mbuzi hapo hamna kesi, hauwezi kushtakiwa,
Hiyo ni kweli au ni stori za vijiweni?