Hivi ni kweli CCM hakuna kiongozi mzuri?

Hivi ni kweli CCM hakuna kiongozi mzuri?

Ndani ya ccm kuna viongozi wengi wazuri, tatizo ni mfumo wao wa chama kwanza.. hakuna mawazo huru utayasikia yakitolewa isipokuwa kwa maslahi ya chama
 
kwa nilivyopitia comment zote nimeona tatizo hapa sio viongozi tatizo ni ccm kwa maana ukiwa msafi lakini hupo ndani ya ccm ni sawa na hakuna kitu.Kwamaana hiyo hakuna kiongozi ndani ya ccm atakayeleta mabadiliko sababu ya mfumo jinsi ulivyo mi naona tupambane kuiondoa ccm kwa kwa ujasiri wa kuindoa ccm madarakani ndo utakuwa ujasiri wa kukiondoa chama kingine chochote ambacho kitavurunda japokuwa uongozi sio swala la kujaribu lakini ccm kwa hali jinsi ilivyofika hatuna budi kuiondoa haraka iwezekavyo 2015 hata daktari hubadilisha dozi ikibidi
 
Nimekuwa nikipitia mijadala mbali mbali kwenye jukwaa la siasa tatizo kubwa nililoliona watu wamekuwa na ushabiki mkubwa wa vyama vya siasa.

Kwa mtazamo wangu tuna haja ya kwenda mbali zaidi tukaacha ushabiki wa vyama tukawapima viongozi kwa ufanisi wao na sio kwa vyama vyao, ninaposema viongozi namaanisha kuanzia ngazi za chini mpaka ngazi za juu.

Naomba kuwasilisha tujadili bila ya ushabiki wa vyama karibuni.


Sent from my iPhone using JamiiForums mobile app



Ngoja nikuulize wewe, kwa akili yako kuna kiongozi gani wa CCM ambaye wewe unaona anafaa kuongoza nchi? Najuwa hauna jibu. Umenipata mpaka hapo?
 
Ngoja nikuulize wewe, kwa akili yako kuna kiongozi gani wa CCM ambaye wewe unaona anafaa kuongoza nchi? Najuwa hauna jibu. Umenipata mpaka hapo?

Viongozi wapo wengi tena wazuri sana tatizo ni mfumo wa CCM ndio mbovu, hata ww sasa hivi ukiingia huko utafanya kama wanavyofanya, hiyo haihitaji degree kulijua hilo.


Sent from my iPhone using JamiiForums mobile app
 
Mkuu hapo nakuunga mkono kuwa kuna haja ya kupitishwa sheria ya kuwa na mgombea binafsi itawaondolea viongozi wetu ukiritimba wa vyama vya siasa.


Sent from my iPhone using JamiiForums mobile app
tatizo hizo kura za mgombea binafsi nani atasimamia mikoa yoyote mpango mzima ni chadema ndo mkombozi wa watanzania
 
Tuache ushabiki nafasi ya uraisi !
(1).Kambi ya wazee ni EDWARD LOWASA
(2)Kambi ya vijana ni Ridhiwani Kikwete !
Asante.
 
Ccm hakuna kiongozi anaefaa huyo lowassa mwizi mkubwa mwl nyerere alisema mapema lakini ubishi Wa mkapa na kikwete wakampa madaraka akaileta Richmond name Hugo ridhiwan ndio kabisa afadhali hats lyatonga ccm hakuna MTU we I watupu
 
Nimekuwa nikipitia mijadala mbali mbali kwenye jukwaa la siasa tatizo kubwa nililoliona watu wamekuwa na ushabiki mkubwa wa vyama vya siasa.

Kwa mtazamo wangu tuna haja ya kwenda mbali zaidi tukaacha ushabiki wa vyama tukawapima viongozi kwa ufanisi wao na sio kwa vyama vyao, ninaposema viongozi namaanisha kuanzia ngazi za chini mpaka ngazi za juu.

Naomba kuwasilisha tujadili bila ya ushabiki wa vyama karibuni.


Sent from my iPhone using JamiiForums mobile app

Tatizo ni MFUMO. Mfumo ulioasisiwa na CCM hauruhusu kumpata KIONGOZI MZURI, Na hata pale itakapotokea kwa bahati mbaya kiongozi mzuri akapenya kwenye mfumo huo wa CCM, basi MFUMO utam reject, hata kama amefikia ngazi ya juu.
 
Back
Top Bottom