Hivi ni kwanini Marekani hakuna malaria?

Hivi ni kwanini Marekani hakuna malaria?

Africa bila malaria inawezekana. Mheshimiwa Majaliwa aunde tume ya uchunguzi na majaribio juu ya matumizi, ufanisi, ubora, faida na madhara ya dawa aina ya DDT katika kupambana na mbu wa malaria
 
hicho kivuli cha pink ndio nchi za kitropical zote dunian...
Kama naona vizuri ni sehemu ndogo sana ya USA imepitiwa na hio kivuli chako cha pink sasa sijui unathibitisha nini.
 
Mbu hakai maeneo ya baridi kali barafu imetanda, kwa hiyo nchi nyingi ambazo zina snow ime-cover sehemu kubwa malaria wanasikia tu magazine na news
 
Mbu hakai maeneo ya baridi kali barafu imetanda, kwa hiyo nchi nyingi ambazo zina snow ime-cover sehemu kubwa malaria wanasikia tu magazine na news
Pamoja na hayo, malaria inaachwa Africa kwa makusudi ili kucontrol population pamoja na sababu za kiuchumi kwa western economies. Kumbuka Africa hutumia dollar billion 20 kila mwaka as the total cost + loss inayotokana na malaria kila mwaka
 
Hawa wazungu washenzi sana..yaani baada ya kuona wametatua tatizo la malaria kwao ndo wakazuia matumizi ya DDT. Halafu kwetu wanajifanya kutuletea misaada ya vyandalia na serikali zetu kuwapatia mirabaha ya kuchimba madini. Waliona kwamba wakileta DDT kwetu wangemaliza tatizo la malaria hivyo wasingekua na miradi mingine yenye migongo ya kinyonyaji kama psi . Hawa wazungu wanafiki sana na wataendelea kutunyonya mpaka basi ukuzingatia na aina ya viongozi tulio nao...inakatisha tamaa, hadi inafikia hatua natamani yule Kim Jo wa Korea kusini angekuwa mfalme wa afrika ..naamini wamarekani wasinge tugusa hata kidogo.
 
Huu ujinga ujinga wa malaria ni lazima tuachane nao.., ni ujinga sana watu kupoteza maisha kwa kitu kinazuilika kabisa..
 
Nasikia kiranja ni mtaalam wa masuala ya kemia.., vipi juu ya hii miraculous chemical?
 
Mi hapa ndio huwa nashindwa kuelewa,nakumbuka miaka ya nyuma sana kulikuwa kuna mradi wa kutokomeza malaria, walikuwa wanapulizia dawa kwenye nyumba,ulikuwa unakaa mpaka mieze 6 hujaona wala kusikia Mbu,sijui kwanini wameachana na hii mikakati ya kutokomeza malaria nchini kwetu.
DDT waliihusisha na uwezekano wa kupata kansa DDT imepigwa marufuku duniani,ila kiubishiubishi kuna baadhi ya maeneo inatumika!
 
jamani mi nimekulia dar tangu nzaliwe...nliwahi kuumwa malaria mara kwa mara nkiwa primary..bt nlipofika miaka 12 mwaka 2005 sijaumwa malaria mpaka leo hii..lakini nnaoishi nao nyumbani wanaugua malaria kila baada ya mda..hata mazingira ikifika jioni kuna mbu sana wanashambulia hatari.mda meingine najisahau bila kuchomeka neti mbu wananingata sana.
sasa nna zaid ya miaka kumi siijui hospitali wala malaria,wala typhoid wala ugonjwa wowote. nlizoea ile harufu bt now nkiingia hospital ile harufu ya madawa nkiiskia najiskia kutapika kweli.je ntakuwa na nini kwenye mwili wangu?

Kinga hiyo inafanya kazi vyema. Endelea kula mlo huo huo unaokula kwa siku usiache.
 
Back
Top Bottom