GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,694
- 109,128
Hivi kweli CCM mnataka Kutudanganya Watanzania kuwa Mapendekezo ya kuweka Tozo Umiza kwa Wananchi yaliyofanywa na Waziri wa Fedha Dk. Nchemba kwanza hayakupita Kwenu kama Chama Dola na hata kwa Mwenyekiti wenu Taifa Rais Samia Suluhu Hassan na mkayabariki?
Sasa iweje leo tena mnatuonyesha Undumilakuwili wenu wa Kujifanya nanyi mmeguswa na Machungu ya Tozo Umiza kwa Wananchi ambayo nyie nyie mliibariki na sasa kuitaka Serikali ( ambayo inaundwa na CCM ) ipitie upya hizi Tozo Umiza ili kuwapunguzia Machungu Wananchi ambao wengine ni wana CCM Wenzenu?
Na wala msianze kusema sijui GENTAMYCINE ni Mpinzani hivyo anatumika Mimi ni Shabiki Mwandamizi ( ila bado sijawa Mwanachama ) wa CCM na hiki ninachokiwasilisha hapa nakitoa katika Fikra nyingi za Watanzania ambao kutokana na Fani yangu nakutana nao 24/7 na Wanalalamika mno.
Kitendo cha leo hii CCM kujitokeza hadharani kuhoji hizi Tozo Umiza zenu wakati zilipitishwa na 99% ya Wabunge wa CCM, ikabarikiwa nanyi CCM kama Chama Dola na Kubarikiwa zaidi na Mwenyekiti wenu Taifa Rais Samia Suluhu Hassan ni Unafiki Usiovumilika kwa Sisi Watanzania wenye Upeo, Maono na Akili Kubwa kuwazidi.
Mtanichukia ila Ukweli ninawapeni!!!
Sasa iweje leo tena mnatuonyesha Undumilakuwili wenu wa Kujifanya nanyi mmeguswa na Machungu ya Tozo Umiza kwa Wananchi ambayo nyie nyie mliibariki na sasa kuitaka Serikali ( ambayo inaundwa na CCM ) ipitie upya hizi Tozo Umiza ili kuwapunguzia Machungu Wananchi ambao wengine ni wana CCM Wenzenu?
Na wala msianze kusema sijui GENTAMYCINE ni Mpinzani hivyo anatumika Mimi ni Shabiki Mwandamizi ( ila bado sijawa Mwanachama ) wa CCM na hiki ninachokiwasilisha hapa nakitoa katika Fikra nyingi za Watanzania ambao kutokana na Fani yangu nakutana nao 24/7 na Wanalalamika mno.
Kitendo cha leo hii CCM kujitokeza hadharani kuhoji hizi Tozo Umiza zenu wakati zilipitishwa na 99% ya Wabunge wa CCM, ikabarikiwa nanyi CCM kama Chama Dola na Kubarikiwa zaidi na Mwenyekiti wenu Taifa Rais Samia Suluhu Hassan ni Unafiki Usiovumilika kwa Sisi Watanzania wenye Upeo, Maono na Akili Kubwa kuwazidi.
Mtanichukia ila Ukweli ninawapeni!!!