Hivi ndivyo wanaofurahia uzinzi, ulevi na dhambi nyingine watakavyoteseka milele

Hivi ndivyo wanaofurahia uzinzi, ulevi na dhambi nyingine watakavyoteseka milele

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
5,527
Reaction score
7,121
Loo, wanacheka, wanarukaruka, wanacheza wakifurahia uzinzi, ulevi, ulaghai, wizi, na anasa za dunia. Wanadhani maisha hayo hayana tatizo. Lakini Biblia iko wazi kabisa: maisha ya dhambi yana mwisho mbaya mno. Ni mateso ya milele na milele. Tafadhali, fuatana nami leo tuitafakari habari ya tajiri na Lazaro iliyoandikwa katika Luka 16:19–31, pamoja na maandiko mengine, tuone kwa undani mateso yanayowasubiri wanaoendelea kufurahia dhambi na kukataa kuokoka:

1. Watu hao wakifa tu, wanaingia moja kwa moja mahali penye mateso. Biblia inasema tajiri aliyekuwa akifurahia maisha ya anasa alikufa na mara moja akaingia katika mateso:
“Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso...akalia” (Luka 16:22–23)

Hii ni tahadhari kwa wale wanaoishi katika dhambi: kifo sio mwisho wa maisha, ni mwanzo wa mateso ya milele kwa wasiotubu.

2. Wanateseka katika moto mkali usiozimika. Tajiri aliyezoea starehe, alijikuta akililia tone la maji kwa sababu ya mateso:
“Akalia, akasema, Ee baba Abrahamu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, aupoze ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.” (Luka 16:24)

Wale wanaoishi maisha ya ulevi, uasherati na dhambi nyingine hawatapata tena faraja wala kicheko, bali mateso makali yasiyo na mwisho:
“Nao watatupwa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.” (Mathayo 13:42)

3. Wanajuta sana, lakini majuto ya marehemu hayana faida. Tajiri alitamani ndugu zake waambiwe ili wasiende mahali alipo kwenye mateso, lakini alikuwa amechelewa:
“Basi, nakuomba, baba, umtume Lazaro... awashuhudie.” (Luka 16:27–28)

Majuto hayo yatawapata wote wanaodharau habari njema za Yesu Kristo. Ni heri ujute sasa na kuacha dhambi zako kuliko kujuta milele bila msaada.

4. Watahukumiwa na kisha kutupwa katika ziwa la moto. Kuzimu ni hatua ya kwanza tu. Baada ya hukumu kuu ya mwisho, watenda dhambi wote watatupwa kwenye ziwa la moto la milele:
“Na iwapo mtu yeyote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.” (Ufunuo 20:15)

Hii ndiyo hatima ya mwisho ya wale wanaoendelea kufurahia dhambi bila kutubu. Jehanam ni mahali penye maumivu, upweke, huzuni, hofu, na mateso ndani ya moto usiozimika, milele na milele.

Ndugu yangu usipoteze bure fursa ya kuingia mbinguni. Kama tulivyoona, wenye dhambi wanapokufa bila kutubu, hawana tena nafasi ya kubadilisha hatima yao. Tajiri alimwona Lazaro akiwa kifuani mwa Ibrahimu, lakini hakuweza kufika huko (Luka 16:26).

Furaha ya dhambi ni ya muda mfupi, lakini athari yake ni ya milele. Mtu akiikataa neema sasa, ataukosa uzima wa milele baadaye.

Bado nafasi ipo. Leo ni siku yako mwafaka ya kuacha dhambi na kumrudia Mungu, na kumpokea Yesu awe Bwana wa maisha yako. Usingoje hadi uwe mfu ndio ujue uzinzi na ulevi vilikuwa mtego wa ibilisi.

Naamini umenielewa na utafanya uamuzi wa kuokoka sasa hivi. Kumbuka, hakuna aijuaye siku ya kuondoka duniani. Kwa sababu hiyo, usiupuuze ujumbe huu, vinginevyo ukifa kabla hujatubu na kuokoka, utaingia kwenye mateso hayo ya milele.
“Tazama, sasa ni wakati uliokubalika; tazama, sasa ni siku ya wokovu.”
(2 Wakorintho 6:2)

cc: Binti wa zamani Mallerina Lamomy I feel good leo dada
 
The Legacy labda wewe uje kusoma utaelewa!

No Way Wtf GIF by Harlem.gif
 
Wewe mama mchungaji taratibu kwanza, kwani kuna kiumbe hakizini hapa duniani?
Au nyie mlio kwenye ndoa ndo mnataka peke yenu mlombwe? 😹😹😹

*Kuzini ni kuzini, hata mama yake Yesu alipatikana kwa midinyano. ✅

*Kulewa ntalewa sana Yesu mwenyewe aliwalewesha watu kwenye harusi kwa mvinyo uliochachuka. ✅

Hiyo mbingu haipo usitutishe, wewe uliiona? Ulifika ukaikuta?
 
Huwa natamani kusoma nyuzi zako ila naishiaga kusoma title tu ni ndefu mno
Nyuzi za uzinzi na ulevi unasoma mwanzo mpaka mwisho Part 1 mpaka Part 3 bila kuchoka. Lakini za Injili unasoma kichwa tu. Sawa, hutakuwa na la kujitetea. Maana nuru imekuja ukapenda giza. Ukiwa jehanam utatamani ungesoma nyuzi zangu mwanzo hadi mwisho, lakini utakuwa umechelewa.
 
Loo, wanacheka, wanarukaruka, wanacheza wakifurahia uzinzi, ulevi, ulaghai, wizi, na anasa za dunia. Wanadhani maisha hayo hayana tatizo. Lakini Biblia iko wazi kabisa: maisha ya dhambi yana mwisho mbaya mno. Ni mateso ya milele na milele. Tafadhali, fuatana nami leo tuitafakari habari ya tajiri na Lazaro iliyoandikwa katika Luka 16:19–31, pamoja na maandiko mengine, tuone kwa undani mateso yanayowasubiri wanaoendelea kufurahia dhambi na kukataa kuokoka:

1. Watu hao wakifa tu, wanaingia moja kwa moja mahali penye mateso. Biblia inasema tajiri aliyekuwa akifurahia maisha ya anasa alikufa na mara moja akaingia katika mateso:
“Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso...akalia” (Luka 16:22–23)

Hii ni tahadhari kwa wale wanaoishi katika dhambi: kifo sio mwisho wa maisha, ni mwanzo wa mateso ya milele kwa wasiotubu.

2. Wanateseka katika moto mkali usiozimika. Tajiri aliyezoea starehe, alijikuta akililia tone la maji kwa sababu ya mateso:
“Akalia, akasema, Ee baba Abrahamu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, aupoze ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.” (Luka 16:24)

Wale wanaoishi maisha ya ulevi, uasherati na dhambi nyingine hawatapata tena faraja wala kicheko, bali mateso makali yasiyo na mwisho:
“Nao watatupwa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.” (Mathayo 13:42)

3. Wanajuta sana, lakini majuto ya marehemu hayana faida. Tajiri alitamani ndugu zake waambiwe ili wasiende mahali alipo kwenye mateso, lakini alikuwa amechelewa:
“Basi, nakuomba, baba, umtume Lazaro... awashuhudie.” (Luka 16:27–28)

Majuto hayo yatawapata wote wanaodharau habari njema za Yesu Kristo. Ni heri ujute sasa na kuacha dhambi zako kuliko kujuta milele bila msaada.

4. Watahukumiwa na kisha kutupwa katika ziwa la moto. Kuzimu ni hatua ya kwanza tu. Baada ya hukumu kuu ya mwisho, watenda dhambi wote watatupwa kwenye ziwa la moto la milele:
“Na iwapo mtu yeyote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.” (Ufunuo 20:15)

Hii ndiyo hatima ya mwisho ya wale wanaoendelea kufurahia dhambi bila kutubu. Jehanam ni mahali penye maumivu, upweke, huzuni, hofu, na mateso ndani ya moto usiozimika, milele na milele.

Ndugu yangu usipoteze bure fursa ya kuingia mbinguni. Kama tulivyoona, wenye dhambi wanapokufa bila kutubu, hawana tena nafasi ya kubadilisha hatima yao. Tajiri alimwona Lazaro akiwa kifuani mwa Ibrahimu, lakini hakuweza kufika huko (Luka 16:26).

Furaha ya dhambi ni ya muda mfupi, lakini athari yake ni ya milele. Mtu akiikataa neema sasa, ataukosa uzima wa milele baadaye.

Bado nafasi ipo. Leo ni siku yako mwafaka ya kuacha dhambi na kumrudia Mungu, na kumpokea Yesu awe Bwana wa maisha yako. Usingoje hadi uwe mfu ndio ujue uzinzi na ulevi vilikuwa mtego wa ibilisi.

Naamini umenielewa na utafanya uamuzi wa kuokoka sasa hivi. Kumbuka, hakuna aijuaye siku ya kuondoka duniani. Kwa sababu hiyo, usiupuuze ujumbe huu, vinginevyo ukifa kabla hujatubu na kuokoka, utaingia kwenye mateso hayo ya milele.
“Tazama, sasa ni wakati uliokubalika; tazama, sasa ni siku ya wokovu.”
(2 Wakorintho 6:2)

cc: Binti wa zamani Mallerina Lamomy I feel good leo dada
Ingawaje sijasoma nikamaliza naomba kuuliza swali

Mi nikiamua kula bata la maana kabisa hadi nizeeke labda miaka 60 ndio niokoke...... Je nikifanikiwa kutoboa hadi 60yrs halafu ndio nikaokoka nikifa nakwenda Peponi?
 
Nyuzi za uzinzi na ulevi unasoma mwanzo mpaka mwisho Part 1 mpaka Part 3 bila kuchoka. Lakini za Injili unasoma kichwa tu. Sawa, hutakuwa na la kujitetea. Maana nuru imekuja ukapenda giza. Ukiwa jehanam utatamani ungesoma nyuzi zangu mwanzo hadi mwisho, lakini utakuwa umechelewa.
Bora niangalie haya niliyo na uhakika nayo tunayaona tunayaishi ila ya mbinguni nani alienda kutembea akarudi?
 
Nyuzi za uzinzi na ulevi unasoma mwanzo mpaka mwisho Part 1 mpaka Part 3 bila kuchoka. Lakini za Injili unasoma kichwa tu. Sawa, hutakuwa na la kujitetea. Maana nuru imekuja ukapenda giza. Ukiwa jehanam utatamani ungesoma nyuzi zangu mwanzo hadi mwisho, lakini utakuwa umechelewa.
Za uzinzi zinanoga, sasa kama hii Utamu wa tunda Part 1 au Part 2 au ya jana Part 3 unaachaje kusoma mpaka mwisho ukakutana na madini ya akina makaveli10 wakiongelea "Morning Glory" 🤣 🤣 😋 😅
 
Nyuzi za uzinzi na ulevi unasoma mwanzo mpaka mwisho Part 1 mpaka Part 3 bila kuchoka. Lakini za Injili unasoma kichwa tu. Sawa, hutakuwa na la kujitetea. Maana nuru imekuja ukapenda giza. Ukiwa jehanam utatamani ungesoma nyuzi zangu mwanzo hadi mwisho, lakini utakuwa umechelewa.
Ninasikia kwamba ipo siku ya hukumu ambapo kila awaye yote atalipwa sawa na matendo yake...kama kumbe watenda maovu wanapokufa basi wanaenda moja Kwa moja kupokea adhabu ya moto...je hiyo siku ya hukumu ni ya nini? Ilhali hukumu na adhabu vimeishasetiwa moja Kwa moja?
 
“Akalia, akasema, Ee baba Abrahamu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, aupoze ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.” (Luka 16:24)
Biblia inasema tukifa, mwili unarudi kwenye udongo na roho inarudi kwa mungu. Wakati huo huo biblia hiyo hiyo inasema mtu aliekufa ana vidole na ana ulimi! Hawa watu walioandika biblia walikua wana akili kweli..? Roho ina ulimi??
“Nao watatupwa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.” (Mathayo 13:42)
Sio tu ulimi na vidole, na meno pia!

Ukisoma biblia kwa makini, utagundua watu walioiandika walikua na upeo mdogo sana wa kufikiri ndio maana ina mkanganyiko wa kila aina.

NB: Mimi ni mkristo.
 
Loo, wanacheka, wanarukaruka, wanacheza wakifurahia uzinzi, ulevi, ulaghai, wizi, na anasa za dunia. Wanadhani maisha hayo hayana tatizo. Lakini Biblia iko wazi kabisa: maisha ya dhambi yana mwisho mbaya mno. Ni mateso ya milele na milele. Tafadhali, fuatana nami leo tuitafakari habari ya tajiri na Lazaro iliyoandikwa katika Luka 16:19–31, pamoja na maandiko mengine, tuone kwa undani mateso yanayowasubiri wanaoendelea kufurahia dhambi na kukataa kuokoka:

1. Watu hao wakifa tu, wanaingia moja kwa moja mahali penye mateso. Biblia inasema tajiri aliyekuwa akifurahia maisha ya anasa alikufa na mara moja akaingia katika mateso:
“Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso...akalia” (Luka 16:22–23)

Hii ni tahadhari kwa wale wanaoishi katika dhambi: kifo sio mwisho wa maisha, ni mwanzo wa mateso ya milele kwa wasiotubu.

2. Wanateseka katika moto mkali usiozimika. Tajiri aliyezoea starehe, alijikuta akililia tone la maji kwa sababu ya mateso:
“Akalia, akasema, Ee baba Abrahamu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, aupoze ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.” (Luka 16:24)

Wale wanaoishi maisha ya ulevi, uasherati na dhambi nyingine hawatapata tena faraja wala kicheko, bali mateso makali yasiyo na mwisho:
“Nao watatupwa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.” (Mathayo 13:42)

3. Wanajuta sana, lakini majuto ya marehemu hayana faida. Tajiri alitamani ndugu zake waambiwe ili wasiende mahali alipo kwenye mateso, lakini alikuwa amechelewa:
“Basi, nakuomba, baba, umtume Lazaro... awashuhudie.” (Luka 16:27–28)

Majuto hayo yatawapata wote wanaodharau habari njema za Yesu Kristo. Ni heri ujute sasa na kuacha dhambi zako kuliko kujuta milele bila msaada.

4. Watahukumiwa na kisha kutupwa katika ziwa la moto. Kuzimu ni hatua ya kwanza tu. Baada ya hukumu kuu ya mwisho, watenda dhambi wote watatupwa kwenye ziwa la moto la milele:
“Na iwapo mtu yeyote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.” (Ufunuo 20:15)

Hii ndiyo hatima ya mwisho ya wale wanaoendelea kufurahia dhambi bila kutubu. Jehanam ni mahali penye maumivu, upweke, huzuni, hofu, na mateso ndani ya moto usiozimika, milele na milele.

Ndugu yangu usipoteze bure fursa ya kuingia mbinguni. Kama tulivyoona, wenye dhambi wanapokufa bila kutubu, hawana tena nafasi ya kubadilisha hatima yao. Tajiri alimwona Lazaro akiwa kifuani mwa Ibrahimu, lakini hakuweza kufika huko (Luka 16:26).

Furaha ya dhambi ni ya muda mfupi, lakini athari yake ni ya milele. Mtu akiikataa neema sasa, ataukosa uzima wa milele baadaye.

Bado nafasi ipo. Leo ni siku yako mwafaka ya kuacha dhambi na kumrudia Mungu, na kumpokea Yesu awe Bwana wa maisha yako. Usingoje hadi uwe mfu ndio ujue uzinzi na ulevi vilikuwa mtego wa ibilisi.

Naamini umenielewa na utafanya uamuzi wa kuokoka sasa hivi. Kumbuka, hakuna aijuaye siku ya kuondoka duniani. Kwa sababu hiyo, usiupuuze ujumbe huu, vinginevyo ukifa kabla hujatubu na kuokoka, utaingia kwenye mateso hayo ya milele.
“Tazama, sasa ni wakati uliokubalika; tazama, sasa ni siku ya wokovu.”
(2 Wakorintho 6:2)

cc: Binti wa zamani Mallerina Lamomy I feel good leo dada
UKWELI MTUPU ISIPOKUWA UKIWA DUNIANI SIO RAHISI KUELEWA KWANI UNAJIONA WEWE NI MJANJA. ILA IPO SIKU MANENO HAYA YATAKUJA KAMA MWANGWI
 
Back
Top Bottom