Hivi mtu anakuwa katika hali gani ya akili hadi anakubali kuolewa mke wa tatu, wa nne nk?

Hivi mtu anakuwa katika hali gani ya akili hadi anakubali kuolewa mke wa tatu, wa nne nk?

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
14,176
Reaction score
25,919
Juzi hapa nilikuwa Uturuki. Ni nchi ya watu ambao dini yao inaruhusu kuwa na mke zaidi ya mmoja, lakini wanawake katakata hawakubali kuwa katika ndoa ya mke zaidi ya mmoja, na wanaume wao wanaelewa hilo. Nimewaheshimu sana wanawake wa Uturuki kwa kujitambua kwa namna hii.

Hili ni jambo ambalo siku zote nimeshindwa kuwaelewa wanawake, na wala mtu asiniambie dini yangu inaruhusu. Mwanamke anakuwa katika akili gani hadi anakubali kuolewa kama mke wa pili, au wa tatu?

Kuolewa mke wa pili bado naona kama ningekuwa mwanamke nisingekubali kamwe, sasa wa tatu? Wa nne? Kwamba unakuwa na shida sana ya kupata mwanaume wako au una hali mbaya ya kiuchumi ndio ukakubali?

Na siamini kabisa kwamba yule mwanamke unaemkuta kwa huyo mumeo anafurahia kitendo cha wewe kuja kama mke wa pili au mbaya zaidi, wa tatu au wa nne.

Kwa nini wanawake hamtaki kujikomboa katika jambo hili? Sidhani kama nitamheshimu mwanamke anaekubali kuolewa mke wa tatu au wa nne; labda kidogo wa pili nitamuelewa. Mie naona kama anaekubali kuingilia ndoa ya wengine ambayo tayari ina mke mmoja au wawili kufikiri kwake hakupo sawa.

Nadhani ni Safari Sound au Marquiz waliwahi kuimba, "kama nitakuwa mke wa pili nakubali, lakini kama ni watatu sikubali hata kidogo nasikitika"
 
Mwanaume unalalamikaje mwanamke kuolewa mke wa pili ama wa 3?

Yaani wewe unaumia wanawake kuolewa mke wa pili ama wa 3?

Kwa hiyo unaona bora aendelee kua mchepuko kuliko kua na mwanaume wa uhakika wa kumhudumia na kumstiri?
 
Wanarogwa ndio maana wanakubali lakini kikawaida hawakubali.

Hili alishaniambia shehe mmoja wa BAKWATA rafiki yangu pale Morogoro.
Nilimuuliza jirani yangu "ulirogwa ukakubali kuwa mke wa pili au ni akili zako!?"aisee alinipa sifa 1000 za jamaa yake na namna anavyompenda
Wameachana kwa vipigo mke akiwa na mimba kuuuubwa kaenda kulelewa na kaka yake nilishindwa hata kumuonea huruma
 
mara nyingi ni shida tu, wengi wanaoa wake wengi ( kwa tanzagiza) wana uwezo kifedha, hivyo kama mwanamke ana shida na anaahidiwa maisha mazuri hawezi kukataa, btw. waarabu waislamu middle class na upper class wa uae, saudia, katar & co. huoa mke mmoja tu, waislamu wa afrika ndiyo huoa wake wengi sababu polygamy ni sehemu ya utamaduni wa kiafrika, no family, watoto kila kona baba tofauti, no accountability, thats why backwardness kila mahali …
 
Umaskini tu hakuna kingine
Hata iwe umasikini. Mie mwanamke anaekubali kuwa mke wa tatu kwa mfano, naona kama hayuko sawa kichwani. Siamini kwamba anaweza kufanya maamuzi ya busara maishani. Lazima ni mtu wa kuamua kwa hisia zaidi kuliko lojiki, na ni rahisi sana kuwa influenced na watu wengine
 
Mwanaume unalalamikaje mwanamke kuolewa mke wa pili ama wa 3?

Yaani wewe unaumia wanawake kuolewa mke wa pili ama wa 3?

Kwa hiyo unaona bora aendelee kua mchepuko kuliko kua na mwanaume wa uhakika wa kumhudumia na kumstiri?
Ni afadhali mwanamke kuwa mchepuko kuliko kuwa mke wa tatu!

Tena mara nyingi hawa wake wa tatu nk wanachepushwa kirahisi sana.
 
Back
Top Bottom