hivi mbowe anajua kiingereza?

hivi mbowe anajua kiingereza?

Status
Not open for further replies.
Leo nimeamka nimekuta maji yamekatika, nikatumia tu tussue, yaani nasikia nawashwa sana itabidi ninunue maji ya chupa, nikosa nitatumia hata soda, kishindikana tusker
 
mwaka 2005,alifanya ziara uingereza then marekani. Inawezekana umeanza kufwatilia siasa wakati wa bunge la bajeti 2013/14
 
mleta uzi yuko sahihi. kiongozi mkuu lazima ajue kiingereza. kwa mbowe naona kuongea kiingereza ni kama kumuambia abebe mlima wa Kilimanjaro. kinampa tabu sana! nashauri apelekwe ktk kozi ya kiingereza. ndugu zanguni mimi naamini kuwa uzungumzaji kiingereza kwa ufasaha ni kigezo cha usomi na uelewa mzuri wa mtu. haiwezekani ufike chuo kikuu kasha ushindwe kuongea kiingereza. ww ni bongo lala. kuna siku hamad Rashid alimtoa kamasi mbowe ktk mdahalo wa pamoja. siku hiyo ndiyo niligundua upeo na uwezo mdogo wa mbowe.
 
1)Maana sijawahi kumsikia anazungumza kiingereza 2)ndio maana hata ziara za chama nje ya nchi huwa anakwepa

1)kwa sababu hujawahi kumsikia akiongea kingereza ndio una-conclude hajui kingereza hii kali. Je ulishawahi kumsikia Jakaya anaongea kikwere? kama hujawahi maana yake hajui au?
2)Safari ipi ya nje ya nchi aliyoikwepa? Inaelekea hata hujui kuwa Mbowe huwa anasafiri mara kadhaa kwenda nje ya nchi kama kuna umuhimu wa yeye kwenda nje. Au tafsiri yako ya kusafiri ni safari lukuki kama za JK?
 
profilepic117935_1.gif


Avatar yako ipo hivi, tutegemee nini? ni kwanini humtendei haki huyo marehemu?

Kweli mkuu..Avatar hii ni udhalilishaji tu..
 
Anaweza kuwa anajua Kukuzidi, japo kiingereza ni lugha tu kama Kiswahili,

"The real communication is the massage received, not intendmassage"

Jiulize ulitaka upeleke ujumbe gani na Ujumbe wako umepokelewaje, kisha pima kama ujumbe wako unaaksi hekima yako.

 
Leo nimeamka nimekuta maji yamekatika, nikatumia tu tussue, yaani nasikia nawashwa sana itabidi ninunue maji ya chupa, nikosa nitatumia hata soda, kishindikana tusker

Kumbe sio huku tu yamekatika? Nimagiza maziwa fresh kwa ajili ya kazi kama ya kwako....
 
ndio nyie mnaoamini kuwa ukijua kiingereza ndio kuwa na akili, mnasahau kiingereza hakiendani na uwezo wa mtu wa kufikiria. pole sana. ila jua nyerere alitumia kiswahili kuwaunganisha watu ni kuikomboa nchi. na watu wengi wa kijijini hawajui kiingereza.
 
JK alikuwa Singapore juzi juzi tu, hivi anajua lugha yao?
 
mleta uzi yuko sahihi. kiongozi mkuu lazima ajue kiingereza. kwa mbowe naona kuongea kiingereza ni kama kumuambia abebe mlima wa Kilimanjaro. kinampa tabu sana! nashauri apelekwe ktk kozi ya kiingereza. ndugu zanguni mimi naamini kuwa uzungumzaji kiingereza kwa ufasaha ni kigezo cha usomi na uelewa mzuri wa mtu. haiwezekani ufike chuo kikuu kasha ushindwe kuongea kiingereza. ww ni bongo lala. kuna siku hamad Rashid alimtoa kamasi mbowe ktk mdahalo wa pamoja. siku hiyo ndiyo niligundua upeo na uwezo mdogo wa mbowe.

Mbowe kafanikiwa awe anajua lugha hiyo au la, kwani CHADEMA kailetea mafanikio makubwa.Acha kuhukumu kitabu kwa kava lake.

Lipumba na usomi wake kafanikiwa nn kwenye chama chake?

Jakaya naye je? Idadi ya wabunge chamani kwake imepungua, je hayo ndo mafanikio?
Mikataba mibovu wanasaini wote wanajua lugha husika,nao wamesaidia nn taifa zaidi ya hasara kubwa?

Achana na unafiki jenga hoja zenye kusaidia taifa na raia wake.
 
Anajua kile cha Madjs tu lakini cha kuongea mbele ya umma subutu. Hata siku moja hauwezi kumkuta anafanya mahojiano kwa lugha ya kiingereza kinampata tabu sana, ni aibu kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni hajuhi lugha ya kimataifa.

Unadhani akipata ugeni wa kimataifa ataongea nao lugha gani si aibu.
 

kwani kujua kingereza ndio
sifa ya uongozi au?tunaangalia brain bana
na uwezo wa kufikiri,kiinglish hakimati hapo!
 
Khaa!! Hivi Yesu Kristo, Mtume Muhamad na wazee wengine kama kina Archimedes, Socrates, Zera Yacob nk walijua hata neno moja la kiingereza?? Naona kabla ya kuanzisha mada hakikisha uko soba :heh:
 
mbowe kafanikiwa awe anajua lugha hiyo au la, kwani chadema kailetea mafanikio makubwa.acha kuhukumu kitabu kwa kava lake.

Lipumba na usomi wake kafanikiwa nn kwenye chama chake?

Jakaya naye je? Idadi ya wabunge chamani kwake imepungua, je hayo ndo mafanikio?
Mikataba mibovu wanasaini wote wanajua lugha husika,nao wamesaidia nn taifa zaidi ya hasara kubwa?

Achana na unafiki jenga hoja zenye kusaidia taifa na raia wake.
punguza ujuha na ukijiweni hapa. Tunazungumzia lugha. Nakiri kuwa ana mengi kayafanya. Hapa mjadala ni uwezo wake wa kuongea kiingereza. Ndiyo maana mnafeli sana mitihani. Unaulizwa hili ww unajibu lile. Badilika dogo!
 
mleta uzi yuko sahihi. kiongozi mkuu lazima ajue kiingereza. kwa mbowe naona kuongea kiingereza ni kama kumuambia abebe mlima wa Kilimanjaro. kinampa tabu sana! nashauri apelekwe ktk kozi ya kiingereza. ndugu zanguni mimi naamini kuwa uzungumzaji kiingereza kwa ufasaha ni kigezo cha usomi na uelewa mzuri wa mtu. haiwezekani ufike chuo kikuu kasha ushindwe kuongea kiingereza. ww ni bongo lala. kuna siku hamad Rashid alimtoa kamasi mbowe ktk mdahalo wa pamoja. siku hiyo ndiyo niligundua upeo na uwezo mdogo wa mbowe.
Mkuu!!!!! Hamad Rashid si yule mbunge wa mahakama?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom