Hivi Majukumu ya Gerson Msigwa katika Wizara yake ni Kufurahia tu Kugawa Fedha za 'Goli la Mama' kwa Simba, Yanga na Taifa Stars?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,573
108,930
Wizara anayoiongoza kama Katibu Mkuu ni ya Sanaa, Utamaduni na Michezo ila tokea ateuliwe hapo GENTAMYCINE sijawahi kusikia akifanya lolote la maana katika Sanaa na Utamaduni zaidi ya Yeye kwa 99% kujikita katika Kutafuta Sifa na Umaarufu kupitia Fedha za Goli la Mama kwa Vilabu Vikubwa na vyenye Ushawishi mkubwa nchini vya Simba na Yanga pamoja na Timu ya Taifa ya Taifa Stars..

Namshauri Rais Samia aunde Wizara Mpya iitwe Wizara ya Kutafuta Umaarufu wa Kisiasa kwa Simba, Yanga na Taifa Stars halafu Waziri au Katibu Mkuu wake awe Gerson Msigwa na huku katika Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo ateuliwe Katibu Mkuu mwenye Akili na Uwezo wa Kuiongoza hiyo Wizara kwa Usawa na Haki wa Kisekta na siyo kuwa na Katibu Mkuu ambaye Utendaji wake unajulikana au unapimwa tu kwa Ushindi wa Vilabu vya Simba, Yanga na Taifa Stars.
 
Huwa ndivyo alivyo, uwezo wake ndipo ulipoishia kwa sasa.
 
Back
Top Bottom