Hivi kwanini wenye magari binafsi hushambuliwa na watembea na miguu au bodaboda?

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,295
21,438
Wapendwa,

Naomba leo kujadili swala la chuki za kisaikolojia zilizopo baina watembea kwa mguu/Bodaboda na wenye magari binafsi, swala hili linaonekana sasa kuwa changamoto kwakweli kama vipi mamlaka na police wafanye kampeni kuelimisha watu waache kujichukulia sheria mkononi,

HISTORIA YA MATUKIO

Kwa mda sasa imekuwa kama kasumba, nimeshuhudia ajali kadhaa kwa magari ya watu binafsi inapotokea labda kwa bahati mbaya wanagongana na Bodaboda ama mtembea kwa miguu-Mara nyingi mwenye gari huonekana ana makosa au hata kupigwa na raia ama gari yake kuumizwa kwa fujo na kuharibiwa ama kuibiwa mali zake.mfano;

1. Historia inaonesha chanzo cha wa-machinga kuondolewa Kariakoo, ilikuwa ni tukio moja la mwenye gari ndogo binafsi alimgusa mtembea kwa miguu yaani kama kumpush,sasa kutokana na ule msongamano watu walimshambulia mwenye ile gari hadi wakamuua kabisa.

2. Kuna jamaa mmoja alikuwa mgeni njia moja halafu mvua ilikuwa imenyesha kukawa na madimbwi, sasa kwakuwa hakuijuwa njia ile vizuri ikabidi awaulize watembea kwa miguu wanaishi maeneo hayo, wakamwambia pita tu pafupi- mwenye gari alipopita akazama kulikuwa na bonge la shimo.

3. Kawaida gari na mtembea kwa miguu mnatakiwa kila mmoja ampishe mwenzake, tena ni vizuri mtembea kwa miguu ndiye haswa ampishe mwenye gari, lakini utashangaa inapotokea mtembea kwa miguu /boda kupushiwa…huwa wanakuja juu sana ama kununa na kumchungulia dreva wa gari sielewi lawama ni za nini.

4. Kuna ajali iliwahi kutokea maeneo ya Mbagala jamaa mwenye gari ndogo alichomekewa na Bodaboda jamaa akawa kamgonga, ila kwa usitaarabu alisimama ili kutaka muafaka, baada ya mda mfupi bodaboda kibao zilimshambulia jamaa kwa mawe kiasi kwamba hadi jamaa akachomoa bastola akamchapa mmoja, walipoona mmoja kafa –wengine wakatawanyika jamaa akachomoa mchuma mpaka kituoni kwenda kuripoti ( trafiki kesi na shambulizi)

5. Mwendesha bodaboda alijigonga/aliligonga kwa nyuma gari la taka akafa palepale, wenzake wakashambulia liel gari.

6. Magari madogo huvunjiwa sidemirror na waendesha bodaboda kwa chuki binafsi ambayo haijulikani.
7. Kuna jamaa yangu alipata ajali maeneo ya Ubungo, watu badala ya kumsaidia badala, wakamwambia ebu fungua boneti harakaharaka gari inaungua, jamaa kubinua tu, wakachomoa betri fasta, na kumwambiwa fungua buti la nyuma tuweke, ile kufungua wakachukua vitu kule kwenye buti na kuanza mbio, alipowafukuzia wengine wakachomoa radio n.k

Sasa naomba tuambizane hapa, hii tabia ya watu kujichukilia sheria mkononi kumshambulia mwenye gari ndogo pindi ajari inapotokea itokomezwe vipi? Maana sasa hivi imekuwa ni bora ukimbie na gari hadi police kujisalimisha kuepuka hawa raia wanapotokea mara nyingi wamekuwa wakishambulia mwenye gari kwasababu ambazo mi naona ni kama chuki binafsi iliyojengeka akilini mwa watu. (mimi natembea na bastora lakini bado naona si busara kuitumia cha msingingi ni maelewano na sheria ifatwe)
MIFANO HIYO INAONYESHA VILE MWENYE GARI ANACHUKIWA NA WATEMBEA KWA MIGUU
Je wadau jambo hili mnalitazamaje? Watu kushambulia magari yanapopata ajari na bodaboda ama kumgonga mtu? NINI KIFANYIKE? maana kama halitafanyiwa kazi ipo siku mwenye gari ataangamiza raia kwa bastola ili kujihami.
 

Attachments

  • moto bunju.jpg
    moto bunju.jpg
    30.8 KB · Views: 35
Kwa bodaboda nawezasema ni ulimbukeni maana bodaboda wanaendesha rafu sana ila akikosea ukamgonga wanakushukia wote na usipoweza kukimbia kifo kinaweza kukukuta. Wao wanajiona wana haki sana kuliko wengine wanaotumia barabara
 
Hawa jamaa kama una chamoto wakikusogelea we walipue tu maana ukichelewa na akili zao fyatu wanakutanguliza wewe. Hawana akili kabisa hawa jamaa
 
Jana Kituo Cha Fire Kwenye Taa Kwenda Muhimbili
Bodaboda Na Ujanja Wa Zamani
Askari Karuhusu Gari Kwenda Njia Ya Muhimbili Akachomeka Kwa Mbele Akagongwa Akaanguka Akiwa Mzima Tatizo Gari Bumper Limeng'oka.

Bodaboda Kanyanyuka Na Kuanza Kukimbia Kwa Kukokota Bodaboda Maana Iligoma Kuwaka.
Haya Mambo Kuna Wakati Bodaboda Wanatumia Ubabe
 
Watu wanaassociate kua na gari ni utajiri na pia unaringa,una dharau,majivuno na hujali watu wengine nk!ile negativity inatriger kuchukiwa na mwisho wake ndio hayo majanga yanatokea!social economic inequality pia inachangia cz TZ mtu akimiliki gari anaonekana anajiweza hata km gari yenyewe ni dola 500 Fob tena toyota,ni ulimbukeni na ujinga uliopitiliza kutoheshimiana barabarani mwisho wake ndio hizi chuku zisizo na msingi!police na vyombo vya habari waelimishe jamii juu ya hili jambo.
 
Uelewa mdogo ukichangia umaskini wengi wakiona tu gari wanajua MTU tajiri anajishau so kukupiga ni njia ya kupunguza machungu ya shida zao. Hawa watu wanahitaji elimu
 
Uelewa hawana hakuna mtu anayetoka nyumbani na gari lake akiwa na dhumni la kwenda kugonga mtu au chombo cha mtu ila inapotokea bahati mbaya wengi wao hawana staha wala busara
 
Madereva wengine wa magari dawa yao ni kichapo maana wanasababisha ajali kwa uzembe wao. Alama barabarani inaonyesha hapa speed 30km/hr lakini dereva wa gari anaendesha speed 80km/hr na zaidi, unategemea nini? dawa yenu yao ni kipigo tu hadi tuheshimiane. tena kama dereva wa daladala ndo vichaa kabisa,
 
Upeo mdogo kwa jamii zetu juu ya kuwa na gari. Ukiwa na gari unachukuliwa kama tajiri hivyo kuonekana unajidai au unadharau nk na hivyo kumfanya huyo mwenye gari awe anajipendekeza pendeza kwao ndo wanakuona sawa vingnevyo n shda. Mfano chukulia mbunge akiwa kwenye gari hata kama ana safari zake itamlazimu tu apunge punge mikono na tabasamu za hapa na pale vingnevyo atachukuliwa anajidai. Kwa kifupi africa bado tuna safari ndefu
 
Wapendwa,

Naomba leo kujadili swala la chuki za kisaikolojia zilizopo baina watembea kwa mguu/Bodaboda na wenye magari binafsi, swala hili linaonekana sasa kuwa changamoto kwakweli kama vipi mamlaka na police wafanye kampeni kuelimisha watu waache kujichukulia sheria mkononi,

HISTORIA YA MATUKIO

Kwa mda sasa imekuwa kama kasumba, nimeshuhudia ajali kadhaa kwa magari ya watu binafsi inapotokea labda kwa bahati mbaya wanagongana na Bodaboda ama mtembea kwa miguu-Mara nyingi mwenye gari huonekana ana makosa au hata kupigwa na raia ama gari yake kuumizwa kwa fujo na kuharibiwa ama kuibiwa mali zake.mfano;

1. Historia inaonesha chanzo cha wa-machinga kuondolewa Kariakoo, ilikuwa ni tukio moja la mwenye gari ndogo binafsi alimgusa mtembea kwa miguu yaani kama kumpush,sasa kutokana na ule msongamano watu walimshambulia mwenye ile gari hadi wakamuua kabisa.

2. Kuna jamaa mmoja alikuwa mgeni njia moja halafu mvua ilikuwa imenyesha kukawa na madimbwi, sasa kwakuwa hakuijuwa njia ile vizuri ikabidi awaulize watembea kwa miguu wanaishi maeneo hayo, wakamwambia pita tu pafupi- mwenye gari alipopita akazama kulikuwa na bonge la shimo.

3. Kawaida gari na mtembea kwa miguu mnatakiwa kila mmoja ampishe mwenzake, tena ni vizuri mtembea kwa miguu ndiye haswa ampishe mwenye gari, lakini utashangaa inapotokea mtembea kwa miguu /boda kupushiwa…huwa wanakuja juu sana ama kununa na kumchungulia dreva wa gari sielewi lawama ni za nini.

4. Kuna ajali iliwahi kutokea maeneo ya Mbagala jamaa mwenye gari ndogo alichomekewa na Bodaboda jamaa akawa kamgonga, ila kwa usitaarabu alisimama ili kutaka muafaka, baada ya mda mfupi bodaboda kibao zilimshambulia jamaa kwa mawe kiasi kwamba hadi jamaa akachomoa bastola akamchapa mmoja, walipoona mmoja kafa –wengine wakatawanyika jamaa akachomoa mchuma mpaka kituoni kwenda kuripoti ( trafiki kesi na shambulizi)

5. Mwendesha bodaboda alijigonga/aliligonga kwa nyuma gari la taka akafa palepale, wenzake wakashambulia liel gari.

6. Magari madogo huvunjiwa sidemirror na waendesha bodaboda kwa chuki binafsi ambayo haijulikani.
7. Kuna jamaa yangu alipata ajali maeneo ya Ubungo, watu badala ya kumsaidia badala, wakamwambia ebu fungua boneti harakaharaka gari inaungua, jamaa kubinua tu, wakachomoa betri fasta, na kumwambiwa fungua buti la nyuma tuweke, ile kufungua wakachukua vitu kule kwenye buti na kuanza mbio, alipowafukuzia wengine wakachomoa radio n.k

Sasa naomba tuambizane hapa, hii tabia ya watu kujichukilia sheria mkononi kumshambulia mwenye gari ndogo pindi ajari inapotokea itokomezwe vipi? Maana sasa hivi imekuwa ni bora ukimbie na gari hadi police kujisalimisha kuepuka hawa raia wanapotokea mara nyingi wamekuwa wakishambulia mwenye gari kwasababu ambazo mi naona ni kama chuki binafsi iliyojengeka akilini mwa watu. (mimi natembea na bastora lakini bado naona si busara kuitumia cha msingingi ni maelewano na sheria ifatwe)
MIFANO HIYO INAONYESHA VILE MWENYE GARI ANACHUKIWA NA WATEMBEA KWA MIGUU
Je wadau jambo hili mnalitazamaje? Watu kushambulia magari yanapopata ajari na bodaboda ama kumgonga mtu? NINI KIFANYIKE? maana kama halitafanyiwa kazi ipo siku mwenye gari ataangamiza raia kwa bastola ili kujihami.
Mkuu,
Mada yako inahusu maisha.
Katika maisha kuna Tabaka mbili za watu, Fukara na Matajiri tukiacha lile kundi la maskini, maana maskini hana say yoyote ni sawa mfu ndio maana hatumhesabu.
Kwa hayo makundi mawili kila kundi lina mazingira yake kimaisha.
Kwa uwezo alio nao tajiri huishi maisha yake kwa raha lakini hudharau fukara kwa Tabaka hii humnyanyasa fukara pale anapoweza kufanya hivyo.
Fukara maisha yake Shida tangu kidole cha miguu hadi utosini hivyo saa yote ana jaziba aonapo mtu anamiliki chombo kama gari itokeapo hitilafu yoyote ndogo tu, iwe kosa au iwe si kosa hutamani aliteketeze hilo gari wakose wote hiyo ndio sababu kubwa.
 
Back
Top Bottom