Hivi kwanini watu hupenda sifa wakiongea na simu?

Trial balance

JF-Expert Member
Jun 16, 2020
202
159
Jamani hii tabia inakera hasa kwenye daladala yani utakuta mtu anaongea kwenye simu kwa sifa, utasikia eh nyama vipi ipo? Vipi ile ela yule mtu alileta? eh mara nikaangie chipsi na nyama nizikute mezani, yaani ataongea kwa kujisifu sifu atakata atampigia mtu mwingine tena hallow natoka bank hapa ule mzigo nimeambiwa upo bado kuchukua tu, yaani utakuta mmepanda daladala ni makelele hadi mwisho wa safari, mimi hii tabia siipendi.

Utashangaa akiwa na watu ni tofauti na maongezi ya peke yake. Kuna siku nilikuwa natoka mkoani naenda Dar kuna kaka alibeba radio yake akawasha tangu mwanzo wa safari wakati huo gari limewasha screen miziki inapigwa kama kawaida na movie zinaendelea na yeye kaweka sauti ya kutosha tu unasikiliza radio yake unasikiliza radio ya gari.

Tulifika kituo flani ivi watu wakamchoka wakamwambia kaka weka earphone unakera wengine. Dah! kaka alikuwa mkali hakuzima radio akagoma kwasababu zilikuwa siti za nyuma tukamwita konda aje aongee naye, akamwambia kaka zima radio akagoma akidai nyimbo anazozipenda yeye zipo kwenye radio yake hafurahishwi na nyimbo za kwenye gari.

Akaendelea kudundisha nyimbo zake hadi mwisho wa safari, kwa kweli watu tulikuwa bored sana hasa Mimi huwa sipendi makelele hata TV kwenye gari siangaliagi nakaaga tu bora ingekuwa simu inakuwa na sauti nyembamba. Hebu imagine radio zile zenye spika alafu kaweka sauti kama yote sauti ilisambaa gari zima ila tuliekaanae karibu ndo tulikelekwa zaidi sauti mbili mbili masikioni bado sauti za story za watu dah makelele na Mimi hapana aisee!
 
Huo ni wivu tu, mbona mm mwenyewe nimetoka benk kutoa mil 8 kwa ajili ya matumizi ya weekend na kuweka mafuta kwenye V8 yangu, ili niwahi kurudi nyumbani kwani nikichelewa huwa napata shida sana kupanda ghorofa ya 3 kwenye nyumba yangu ya Mil 750
 
Huo ni wivu tu, mbona mm mwenyewe nimetoka benk kutoa mil 8 kwa ajili ya matumizi ya weekend na kuweka mafuta kwenye V8 yangu.. ili niwahi kurudi nyumbani kwani nikichelewa huwa napata shida sana kupanda ghorofa ya 3 kwenye nyumba yangu ya Mil 750
Vipi na wewe hayo unaongea na simu ukiwa kwenye daladala?
 
Jamani hii tabia inakera hasa kwenye basi yani utakuta mtu anaongea kwenye simu kwa sifa utasikia eh nyama vipi ipo zile ela yule mtu alileta eh mara nikaangie chips na nyama nizikute mezani yani ataongea kwa kujisifu sifu atakata atampigia mtu mwingine tena hallow natok bank hapa ule mzigo nimeambiwa upo bado kuchukua tu yani utakuta mmepanda daladala ni makelele hadi mwisho wa safati mimi hii tabia siipendi.utashangaa akiwa na watu ni tofauti na maongezi ya peke ake.
Labda ni kweli, hawajisifii
 
Nyuma kidogo nilishuhudia mtu wa namna hiyo lakini yeye alikuwa anatoa tuhuma nadhani za mpenzi kama sio mke kwenye simu tena kwa kelele hasaa sasa mule ndani ya gari kulikuwa tulii na pia kulikuwa na Mzee Mtu Mzima alipoona jamaa kazidi akamkaripia.

"we kijana kama humalizi kuzungumza na hiyo simu yako ikate utaendelea ukishuka kuliko kutupa siri za nyumbani kwako"

Yule jamaa haikumchukua sekunde akakata simu. Na baada ya hapo hamna aliyemsemesha tena cha zaidi jamaa akabaki tu kushangaa shangaa akidhania yule mzee atayaendeleza. 😀
 
Kuna Dada mmoja kaingia kwenye daladala anajifanya Yuko busy na kicheko cha kwenye simu akiongea sauti nyonyoro
Simu ikaona sio kweli
Rahaula
Simu ikamtia aibu ikaita huku iko Sikioni.
Iyo tabia mi ninayo hasa nikipita kwenye watu wengi kama naona aibu naweka sim sikioni naanza kuongea ongea peke angu ili wajue naongea na simu inanipa confidence kupita eneo la watu wengi bila aibu nikipita natoa simu sikioni naendelea na safari yangu.
 
Nyuma kidogo nilishuhudia mtu wa namna hiyo lakini yeye alikuwa anatoa tuhuma nadhani za mpenzi kama sio mke kwenye simu tena kwa kelele hasaa sasa mule ndani ya gari kulikuwa tulii na pia kulikuwa na Mzee Mtu Mzima alipoona jamaa kazidi akamkaripia.

"we kijana kama humalizi kuzungumza na hiyo simu yako ikate utaendelea ukishuka kuliko kutupa siri za nyumbani kwako"

Yule jamaa haikumchukua sekunde akakata simu. Na baada ya hapo hamna aliyemsemesha tena cha zaidi jamaa akabaki tu kushangaa shangaa akidhania yule mzee atayaendeleza.
Hoyo mzee nae ananmawenge kwani yeye anateseka nn kwa kusikia siri za nyumban kwa jamaa na anajuaje kama hayo alkua anazungumza ni siri.
 
Ila mdogo nionavyo ni vyema atume hata SMS kunakuwa na usiri fulani ila si kupayuka.

Mana kuongea na simu kidogo kidogo mbele za watu ni kipaji nacho.
Watu hupenda sifa kwa watu au utakuta mtu anaongea kwenye gari na bebi wake analemba sauti inakuwa ndogoo kama ya kitandani anaongea kwenye gari jamani hata sio poa
 
Ila mdogo nionavyo ni vyema atume hata SMS kunakuwa na usiri fulani ila si kupayuka.

Mana kuongea na simu kidogo kidogo mbele za watu ni kipaji nacho. 😀😀
Kweli sis af me naona ni ushamba eti, kila mtu ajue umekula kuku sjui una hela.

Ni kama mmoja nliona sehem story alipigiwa simu na mkewe akaamua kuweka loud speaker abiria wenzake awarushe roho baada ya kupokea tu mke akasikika 'mbona umekunywa uji wa mtoto' 😂😂 aibu hiyo aliyopata akakata na simu
 
Kweli sis af me naona ni ushamba eti, kila mtu ajue umekula kuku sjui una hela.
Ni kama mmoja nliona sehem story alipigiwa simu na mkewe akaamua kuweka loud speaker abiria wenzake awarushe roho baada ya kupokea tu mke akasikika 'mbona umekunywa uji wa mtoto' 😂😂 aibu hiyo aliyopata akakata na simu
Haipendezi kabisaa mdogo wangu kwani Mara nyingi kelele zile huwa zinaishia kwenye kumtia mtu aibu.
 
Ukiona mtu anajisifia chips sijui nyama ujue wengi wao wametokea njaa kali sana basi anaona ni ufahari kula hvo vitu, na wengi wenye misifa ya simu kwenye daladala wengi wao unakuta wameona aidha dem mkali kwenye hyo daladala mana wengi wao huwa ni wanaume,
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Back
Top Bottom