Katika pitapita zangu club kuna usiku moja nikipata moja moto moja baridi kaunta akaja binti mmoja 'kaka naomba na mimi uninunulie moja' nikamnunulia na tukawa tunaongea,ana miaka 19 na ni yatima.Kamaliza form 4 mwaka jana hana wa kumuendeleza na rafiki yake akamshauri wajiuze.Nikasema hivi Uporoto si utakuwa umefanya jambo jema ukimsaidia huyu mtoto mmoja na kumbadili maisha kwa kumuendeleza na kumuepusha na uchangu ? Nikampa elfu 30 na kumwambia aende nyumbani kesho aje mjini,kesho yake tukakutana nikampeleka sehemu na kumwandikisha asome secretarial course na kumlipia na kumwambia kila wiki nitamtumia hela ya nauli na matumizi madogo kwa Mpesa.Ijumaa nimepita chuo na kuambiwa hajaonekana siku 10 na kwenye simu hapatikani.