Kaka Mtambuzi hata sisi wanawake huwa tunawachoka nyinyi wanaume/waume zetu, kwa sababu kubwa ni kubadilika kwa tabia zenu, pindi mnapotuchumbia, mpk ndoa mnakuwa watu wazuri sana amao mnajua kujali, kutusikiliza kwa kila kitu hata ushauri wetu mnausikiliza na kuufanyia kazi. Lakini pindi nimeshakuwa mke ndani ya nyumba basiiiiiiiiii kila kitu kinabadilika , na yeye ndiye anayekuwa msemaji wa mwisho, hataki tena ushauri, hana kujali tena, wanawake wa nje ndiyo mali kwake kuliko familia yake, anaondoka asubuhi kurudi lala salama, hadi watoto wanakuuliza " BABA KASAFIRI?"
inabidi uitikie ili kuuwa so hapo nyumbani, Sasa hali hii humpelekea mwanaumke kuwa mpweke muda mwingi na kuumia moyoni na kujuta kwa nini alikubali kuolewa na huyo mwanaume.
NINI KINAPELEKEA MWANAMKE KUTOKA NJE: Kwa kipindi hicho anapokuwa mpweke na mwenye majonzi mengi anaweza akapata mtu wa kumweleza shida zake na hisia zake na anaumia vipi moyoni mwake , sasa huyo mwanaume akimbembeleza kidogo tu, akili ya huyo mwanamke ikatulia na kumahidi kumsaidia, hata kama huyo mwanamke alikuwa mzuri na mwenye adabu vipi ni lazima atakuwa na mahusiano ya kula sakalameti takatifu na huyo mwanaume. na kama unavyojua MTAMBUZI cha nje kilivyo kitamu, basi ndipo anaponchonga mzinga.Na familia ndipo inaposambaratika kabisa. MARA NYINGI WANAOANZA NI WANAUME KUTOKA NJE YA NDOA.