Jacobus
JF-Expert Member
- Mar 29, 2011
- 4,681
- 1,698
Wakuu, nimetoka kuangalia kipindi cha 'chetu ni chetu' kilichorushwa na ITV mchana huu.
Japo sikukiangalia tokea mwanzo, maana nilikuwa sehemu, kipindi hicho kilikuwa kikitukumbusha historia ya chifu Mkwawa.
Kilichonifadhaisha ni pale mtangazaji alipoelezea mavazi ya asili ya kabila la Wahehe. Alieleza kwa uzuri kabisa kuwa wanaume walivaa vazi la mgolole na akina mama nguo nyeusi.
Baadae mtangazaji akaeleza kuwa kwa sasa akina mama wanavaa vazi la kistaarabu la kanga, hapo ndo alinichefua na kuanza kujiuliza maswali mengi kuhusu dhumuni la hicho kipindi ni nini!
Ni vema tukavithamini vile wazee wetu walikuwa wakivitumia kwani vilikuwa na maana kiasili yetu.
Japo sikukiangalia tokea mwanzo, maana nilikuwa sehemu, kipindi hicho kilikuwa kikitukumbusha historia ya chifu Mkwawa.
Kilichonifadhaisha ni pale mtangazaji alipoelezea mavazi ya asili ya kabila la Wahehe. Alieleza kwa uzuri kabisa kuwa wanaume walivaa vazi la mgolole na akina mama nguo nyeusi.
Baadae mtangazaji akaeleza kuwa kwa sasa akina mama wanavaa vazi la kistaarabu la kanga, hapo ndo alinichefua na kuanza kujiuliza maswali mengi kuhusu dhumuni la hicho kipindi ni nini!
Ni vema tukavithamini vile wazee wetu walikuwa wakivitumia kwani vilikuwa na maana kiasili yetu.