Hivi kuna nini cha kuangalia mabaki ya Titanic mpaka kuhatarisha maisha?

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,199
10,935
Sasa imejulikana rasmi kuwa nyambizi ya mchongo iliyokuwa ikifanyiwa biashara na kampuni ya Ocean Gate imepasuka na abiria wote watano kufariki dunia.

Waliofariki ni pamoja na mzamiaji maarufu wa kifaransa Paul-Henri Nargeolet. Wengine ni tajiri mkubwa wa kipakistani Shahzada Dawood na mwanawe Suleiman mwenye umri wa miaka 19.

Wengine ni tajiri mkubwa wa Uiengereza na msafiri aitwaye Hamish Harding. Na wa tano ni Stockton Rush ambaye alikuwa ndiye miongoni mwa waendeshaji wa kampuni hiyo na aliyekuwa baharia mkuu katika safari hiyo ya kitalii.

Matumizi ya chombo hicho inasemekana yalikwisha kutolewa onyo na wataalamu wengi kwamba si salama miaka kadhaa iliyopita hata hivyo safari za kitalii za aina hiyo zimekuwa zikiendelea kwa malipo ya fedha nyingi .

Kampuni ya Boeng imekataa kuhusishwa na kutengeneza kinyambizi hicho. Vivyo hivyo shirika la Nasa limejitenga na chombo hicho kama kilivyofanya chuo kikuu cha Washington kilipotajwa kushiriki kukitengeneza kinyambizi hicho

Safari kubwa za chombo hicho ilikuwa ni kuchukua watalii kuwapeleka chini ya bahari takriban futi 13000 katikati ya bahari ya Atlantic ilipozama meli ya Titanic mwaka 1913 na kuua idadi kubwa karibu ya abiria wate walioingia katika meli hiyo.

Kutokana na kupitiwa na muda mrefu meli hiyo ya Titanic kwa sasa imebaki vyuma vyenye matundu matundu ambayo ni makazi ya samaki wachache wanaohimili kuishi kina kirefu cha bahari kama hicho.

Mwaka 2000 mwandishi wa masuala ya sayansi wa kituo cha CBS aliwahi kuganda kwenye Titanic aliposhuka huko kwenye nyambizi ndogo ya kirusi pale waliponasa kwenye feni la meli hiyo na hatimaye kufanikiwa kutoka baada ya saa 72.

Suali la kujiuliza ni kipi wanachokwenda kuangalia wale watalii wanaolipa kiwango kikubwa cha pesa kwa ajili ya safari hiyo ya hatari.

1687504938659.png

Mwandishi wa CBC akiwa ndani ya nyambizi iiyonaswa na feni la Titanic


1687505209718.png

Suleiman imeelezwa alionekana akiwa na hofu sana kabla ya kuingia kwenye chombo hicho ambacho huendeswa na rimoti ya michezo ya watoto kwani hakina teknolojia ya kuwasiliana na vyombo vya juu ya bahari kwani chini ya bahari kina hicho hakuna GPS wala mawasilaino mengine ya kawaida.
 
Yani 4km chini ya habari tu hapa hapa duniani kwetu watu wamesepa mazima na bado kuna watu wanaamini kua mtu amewahi kukanyaga mwezini!

Lakini mtu unawezaje kuweka rehani uhai wako kwa kupanda kile kidude? Chini ya bahari kuna mambo mengi sana.
 
Yani 4km chini ya habari tu hapa hapa duniani kwetu watu wamesepa mazima na bado kuna watu wanaamini kua mtu amewahi kukanyaga mwezini!

Lakini mtu unawezaje kuweka rehani uhai wako kwa kupanda kile kidude? Chini ya bahari kuna mambo mengi sana.
mkuu pressure /mgandamizo kwenye kina cha maji sio poa
 
Yani 4km chini ya habari tu hapa hapa duniani kwetu watu wamesepa mazima na bado kuna watu wanaamini kua mtu amewahi kukanyaga mwezini!

Lakini mtu unawezaje kuweka rehani uhai wako kwa kupanda kile kidude? Chini ya bahari kuna mambo mengi sana.
Kile kidude ni cha kitapeli sana na hakikuwa na vibali husika.Ilikuwa ni mtaji wa matapeli kupata mapesa ya matajiri. Kinaendeshwa na rimotji ya michezo ya watoto kuzama na kupinda huku na hukoj. Yawezekana kule chini hicho kirimoti alipewa Suleiman na akakizamisha chini zaidi.Pressure ikakipasua na wote pamoja.Huenda hata mifupa ilisagika.
 
Sasa imejulikana rasmi kuwa nyambizi ya mchongo iliyokuwa ikifanyiwa biashara na kampuni ya Ocean Gate imepasuka na abiria wote watano kufariki dunia.

Waliofariki ni pamoja na mzamiaji maarufu wa kifaransa Paul-Henri Nargeolet. Wengine ni tajiri mkubwa wa kipakistani Shahzada Dawood na mwanawe Suleiman mwenye umri wa miaka 19.

Wengine ni tajiri mkubwa wa Uiengereza na msafiri aitwaye Hamish Harding. Na wa tano ni Stockton Rush ambaye alikuwa ndiye miongoni mwa waendeshaji wa kampuni hiyo na aliyekuwa baharia mkuu katika safari hiyo ya kitalii.

Matumizi ya chombo hicho inasemekana yalikwisha kutolewa onyo na wataalamu wengi kwamba si salama miaka kadhaa iliyopita hata hivyo safari za kitalii za aina hiyo zimekuwa zikiendelea kwa malipo ya fedha nyingi .

Kampuni ya Boeng imekataa kuhusishwa na kutengeneza kinyambizi hicho. Vivyo hivyo shirika la Nasa limejitenga na chombo hicho kama kilivyofanya chuo kikuu cha Washington kilipotajwa kushiriki kukitengeneza kinyambizi hicho

Safari kubwa za chombo hicho ilikuwa ni kuchukua watalii kuwapeleka chini ya bahari takriban futi 13000 katikati ya bahari ya Atlantic ilipozama meli ya Titanic mwaka 1913 na kuua idadi kubwa karibu ya abiria wate walioingia katika meli hiyo.

Kutokana na kupitiwa na muda mrefu meli hiyo ya Titanic kwa sasa imebaki vyuma vyenye matundu matundu ambayo ni makazi ya samaki wachache wanaohimili kuishi kina kirefu cha bahari kama hicho.

Mwaka 2000 mwandishi wa masuala ya sayansi wa kituo cha CBS aliwahi kuganda kwenye Titanic aliposhuka huko kwenye nyambizi ndogo ya kirusi pale waliponasa kwenye feni la meli hiyo na hatimaye kufanikiwa kutoka baada ya saa 72.

Suali la kujiuliza ni kipi wanachokwenda kuangalia wale watalii wanaolipa kiwango kikubwa cha pesa kwa ajili ya safari hiyo ya hatari.

View attachment 2666140
Mwandishi wa CBC akiwa ndani ya nyambizi iiyonaswa na feni la Titanic


View attachment 2666144
Suleiman imeelezwa alionekana akiwa na hofu sana kabla ya kuingia kwenye chombo hicho ambacho huendeswa na rimoti ya michezo ya watoto kwani hakina teknolojia ya kuwasiliana na vyombo vya juu ya bahari kwani chini ya bahari kina hicho hakuna GPS wala mawasilaino mengine ya kawaida.
Ukiwa na hela lile lisilowezekana unataka liwezekane kukujengea sifa labda na history lakini ile Titainc original iliyozama ilizama na mali nyingi sana yakiwemo madhahabu na vitu vingi vya thamani, huenda mtalii unaenda kwenye ile Meli kuleta kitu amacho kitakupa sifa sana labda kukuongezea na utajiri
 
Gharama tu ya utalii wenyewe ni Tsh million 500+
inawezekana ukiwa tajiri yaani tajiri usie na wasiwasi na kesho yako basi unakua na hamu ya kujaribu kila kitu
maskin leo ukimpa 1B umwambie atoe 500M akatalii sidhan kama atakubali maana bado anakua na wasiwasi na kesho yake
 
Ukiwa na hela lile lisilowezekana unataka liwezekane kukujengea sifa labda na history lakini ile Titainc original iliyozama ilizama na mali nyingi sana yakiwemo madhahabu na vitu vingi vya thamani, huenda mtalii unaenda kwenye ile Meli kuleta kitu amacho kitakupa sifa sana labda kukuongezea na utajiri
Hamna kitu kilichobaki pale cha kufuatwa na mtoto.Kama kipo ile roboti iliyoona mabaki ingekwisha kuzileta hizo dhahabu. Na pia ingewezekana kufungwa kamba na kuvutwa juu kidogo kidogo au ikapelekwa kwenye kina kidogo cha bahari.
 
Sasa imejulikana rasmi kuwa nyambizi ya mchongo iliyokuwa ikifanyiwa biashara na kampuni ya Ocean Gate imepasuka na abiria wote watano kufariki dunia.

Waliofariki ni pamoja na mzamiaji maarufu wa kifaransa Paul-Henri Nargeolet. Wengine ni tajiri mkubwa wa kipakistani Shahzada Dawood na mwanawe Suleiman mwenye umri wa miaka 19.

Wengine ni tajiri mkubwa wa Uiengereza na msafiri aitwaye Hamish Harding. Na wa tano ni Stockton Rush ambaye alikuwa ndiye miongoni mwa waendeshaji wa kampuni hiyo na aliyekuwa baharia mkuu katika safari hiyo ya kitalii.

Matumizi ya chombo hicho inasemekana yalikwisha kutolewa onyo na wataalamu wengi kwamba si salama miaka kadhaa iliyopita hata hivyo safari za kitalii za aina hiyo zimekuwa zikiendelea kwa malipo ya fedha nyingi .

Kampuni ya Boeng imekataa kuhusishwa na kutengeneza kinyambizi hicho. Vivyo hivyo shirika la Nasa limejitenga na chombo hicho kama kilivyofanya chuo kikuu cha Washington kilipotajwa kushiriki kukitengeneza kinyambizi hicho

Safari kubwa za chombo hicho ilikuwa ni kuchukua watalii kuwapeleka chini ya bahari takriban futi 13000 katikati ya bahari ya Atlantic ilipozama meli ya Titanic mwaka 1913 na kuua idadi kubwa karibu ya abiria wate walioingia katika meli hiyo.

Kutokana na kupitiwa na muda mrefu meli hiyo ya Titanic kwa sasa imebaki vyuma vyenye matundu matundu ambayo ni makazi ya samaki wachache wanaohimili kuishi kina kirefu cha bahari kama hicho.

Mwaka 2000 mwandishi wa masuala ya sayansi wa kituo cha CBS aliwahi kuganda kwenye Titanic aliposhuka huko kwenye nyambizi ndogo ya kirusi pale waliponasa kwenye feni la meli hiyo na hatimaye kufanikiwa kutoka baada ya saa 72.

Suali la kujiuliza ni kipi wanachokwenda kuangalia wale watalii wanaolipa kiwango kikubwa cha pesa kwa ajili ya safari hiyo ya hatari.

View attachment 2666140
Mwandishi wa CBC akiwa ndani ya nyambizi iiyonaswa na feni la Titanic


View attachment 2666144
Suleiman imeelezwa alionekana akiwa na hofu sana kabla ya kuingia kwenye chombo hicho ambacho huendeswa na rimoti ya michezo ya watoto kwani hakina teknolojia ya kuwasiliana na vyombo vya juu ya bahari kwani chini ya bahari kina hicho hakuna GPS wala mawasilaino mengine ya kawaida.
Mkuu,

Inaonekana huoni umuhimu wa kufanya utalii hasa kwenye kitu kama Titanic.

Watu wanalipa gharama kwenda kutizama magofu (majengo ya kale) kilwa na sehemu zingine, sembuse Tutanic?

Ajali ni ajali tu kwani chombo hicho kimefanya safari zaid ya 50 bila hitilafu.
Japokuwa kuna taarifa zinadai kuwa siku za karibuni walipewa tahadhari kutika kwa wataalamu kuhusu mfumo wa umeme wa chombo.
 
Back
Top Bottom