Hivi kuna nchi nyingine duniani yenye salamu kama "shikamoo" na "Marahaba"?

mitale na midimu

JF-Expert Member
Aug 26, 2015
10,420
17,701
Salamu hii imekuwa ikilalamikiwa kutokana na asili na maana yake kutokuwepo kwa lugha nyingine. Lakini pia simulizi zinaonyesha ziliibuka enzi za utumwa akitoa heshima kwa Bwana wake.

Kwa lugha za asili nyingi ni halali kumwambia mtu mzima "Habari za asubuhi" kwa kilugha mfano "mwangaluka" lkn salamu hiyohiyo kwa maana hiyo hiyo ukimwambia kwa kiswahili mtu Mzima au mzee itaonekana huna adabu.

Nauliza wanagenzi na wananzuoni wa lugha adhimu ya kiswahili.
HII imekaaje?

Mfano
Hbr za asubuhi/mchana/jioni/usiku.
Kwa kiswahili kama zinavyotumika ktk lugha za asili na lugha nyingine za ulimwenguni. Je kuna sehem yenye salamu yenye sura na maana ya shikamoo marahaba! ?

Mfano chokonozi
Kwa nini wazoea na watu wenye umri mkubwa wengi wa Jiji Kong we la dar es salaam huwa hawapendi kusalimiswa shikamoo.

Je huko nchi nyingine kuna salamu za kitaifa zenye sura ya kitaifa kama hizi.?
Je tuendelee kuzienzi kama urithi wa waliotuachia waarabu japo wao hawazitumii?

Nawaza Kilughalugha

UPDATES...
Kwa Mujibu wa Mtaalam wa kiswahili na Muadhili wa Chuo kikuu cha DSM Dr Rajabu Chipila ktk kipindi cha Meza Huru ITV. Pamoja na mwananchi mdau wa Kiswahili.

1:Shikamoo ni Ishara ya Heshima. Kiini ni heshima licha ya asili yake kuhusishwa na utumwa.
2: Ingekuwa haifai, au hata wazee wetu wasingeiendeleza.
3: Ni kichocheo cha amani pia ikiwa taifa likiwa halina mfumo wa watu kuheshimiana kwa lika, umri, hata mfumo wa amani unakuwa hatarini.
4:Tuzienzi salamu hizi kwa misingi ya Kuheshimiana kizio kinachotuunganisha na sio asili ya neno lenyewe. Maneno haya yanaifanya jamii ya waswahili kuwa jamii ya watu wenye kuheshimiana.
5:Kuna sababu nyingi kwa nini watu hawapendi kutumia salamu hizi ikiwemo za kikabila, utandawazi na haijaanza leo ni tangu enzi inaanza salamu hii, lkn ni vizuri ienziwe kama miongoni mwa kiungo cha umoja na mshikamano kama taifa la watu wanaoheshimiana.
 
Mimi shikamoo hii huwa naona inasound kama tusi vile, sipendi kuisikia hata kidogo!
Kuna mzee kuzeeka Hadi anatembea mgongo umepinda ukitaka ukosane nae sio yeye tu hata bibi ambaye ni mke wake uwasalimie shikamoo. Wanasema kama wewe kuwasupport ni matusi sijui kwa nini.
Hadi watoto wa shule ya msingi darasa la kwanza B wanalazimika kumsalimia *Habari yako* au *za asubuhi mzee. ..* hapo anafurahi na kujibu kwa bashasha.
Mimi shikamoo hii huwa naona inasound kama tusi vile, sipendi kuisikia hata kidogo!
 
Kuna mzee kuzeeka Hadi anatembea mgongo umepinda ukitaka ukosane nae sio yeye tu hata bibi ambaye ni mke wake uwasalimie shikamoo. Wanasema kama wewe kuwasupport ni matusi sijui kwa nini.
Hadi watoto wa shule ya msingi darasa la kwanza B wanalazimika kumsalimia *Habari yako* au *za asubuhi mzee. ..* hapo anafurahi na kujibu kwa bashasha.
Ahahaha we unachukuliaje hiyo salamu mkurugenzi.
 
Kama shikamoo imekaa kitumwa.

Wahindi wanaoshikana miguu je?

Wale wanaosalimiana kwa kuminyana korodani?

Wanaoinamisha kichwa?

Wale wanasimama hadi elder akae au amalize kupita njia ndiyo waendelee na shughuli zao?
Aiseee.. Kati ya hzo ulizoandika hapo bora shikamoo ina ahueni
 
Kama shikamoo imekaa kitumwa.

Wahindi wanaoshikana miguu je?

Wale wanaosalimiana kwa kuminyana korodani?

Wanaoinamisha kichwa?

Wale wanasimama hadi elder akae au amalize kupita njia ndiyo waendelee na shughuli zao?
Maana vs asili ya salamu!!!!
Matendo ya heshima vs matendo yanayosukumwa na mahusiano ya kiBwana na kitumwa.

Kwa sababu watu wanasoma Hadi kuwa na PhD ya lugha hii pendwa wanaweza kukusaidia zaidi.
 
Maana vd asili ya salamu!!!!
Matendo ya heshima vs matendo yanayosukumwa na mahusiano ya kiBwana na kitumwa.

Kwa sababu watu wanasoma Hadi kuwa na PhD ya lugha hii pendwa wanaweza kukusaidia zaidi.
Mimi niko macho kwakua ni mlinzi hivi kuna phd atakua macho saa hii ili aje kunielewesha mbumbumbu?
 
Mimi niko macho kwakua ni mlinzi hivi kuna phd atakua macho saa hii ili aje kunielewesha mbumbumbu?
Kuna jamaa wanaitwa TATAKI mkuu na wengine TUKI nadhani kama huwa wanapita huku wanaweza kuweka kumbukumbu sawa. Hata mimi ni mpiga domo tu huku jf.
Sio lazima saa hizi za kilinzi japo hata wao wanaweza kuwa wanakula buku au wanaita desa mida hii.
 
Shikamoo ni salamu ya heshima kwa mtu aliyekuzidi umri. Huu ni utamaduni wetu Waafrika kuheshimiana. Ndio maana hata kwa hizo salamu za kikabila mara nyingi huambatana na ishara mbali mbali zinazoonesha kuwa unayemsalimia unamheshimu. Mathalini kwa baadhi ya makabila wanawake hupiga magoti wakati watoto huinama kuonesha heshima.

Viva Kiswahili
 
Salamu hii imekuwa ikilalamikiwa kutokana na asili na maana yake kutokuwepo kwa lugha nyingine. Lakini pia simulizi zinaonyesha ziliibuka enzi za utumwa akitoa heshima kwa Bwana wake.

Kwa lugha za asili nyingi ni halali kumwambia mtu mzima "Habari za asubuhi" kwa kilugha mfano "mwangaluka" lkn salamu hiyohiyo kwa maana hiyo hiyo ukimwambia kwa kiswahili mtu Mzima au mzee itaonekana huna adabu.

Nauliza wanagenzi na wananzuoni wa lugha adhimu ya kiswahili.
HII imekaaje?

Mfano
Hbr za asubuhi/mchana/jioni/usiku.
Kwa kiswahili kama zinavyotumika ktk lugha za asili na lugha nyingine za ulimwenguni. Je kuna sehem yenye salamu yenye sura na maana ya shikamoo marahaba! ?

Mfano chokonozi
Kwa nini wazoea na watu wenye umri mkubwa wengi wa Jiji Kong we la dar es salaam huwa hawapendi kusalimiswa shikamoo.

Je huko nchi nyingine kuna salamu za kitaifa zenye sura ya kitaifa kama hizi.?
Je tuendelee kuzienzi kama urithi wa waliotuachia waarabu japo wao hawazitumii?

Nawaza Kilughalugha
Hii ni salamu ya kishamba sana iliyojaa utumwa mtupu ! wanangu nishawakataza kutumia salamu hiyo kwa mtu yeyote
 
Kama shikamoo imekaa kitumwa.

Wahindi wanaoshikana miguu je?

Wale wanaosalimiana kwa kuminyana korodani?

Wanaoinamisha kichwa?

Wale wanasimama hadi elder akae au amalize kupita njia ndiyo waendelee na shughuli zao?
Aiseee""
 
Shikamoo"" na asalam alayqum ....

ni salami ambazo nimetokea kuzichukia mnooo"" huwa sitaki masikio yangu yawe yanasikia huo ujinga ...""..
 
Shikamoo ni salamu ya heshima kwa mtu aliyekuzidi umri. Huu ni utamaduni wetu Waafrika kuheshimiana. Ndio maana hata kwa hizo salamu za kikabila mara nyingi huambatana na ishara mbali mbali zinazoonesha kuwa unayemsalimia unamheshimu. Mathalini kwa baadhi ya makabila wanawake hupiga magoti wakati watoto huinama kuonesha heshima.

Viva Kiswahili
Hata wajita wanaume wanawasalimia wazee wao (wanaume) asubuhi "kampilechasugu" jioni "kampilegwasugu ".
Watulete wazima wanawake watasalimiwa na wavulana "wachamawe-mchana na asubuhi" , "lyagwamawe-jioni".
Ukifuatilia maana ni kama "za asubuhi na hbr za jioni". Au zinahusishwa na jua kuchwa na Kuzama ".
Ila heshima inakuja pale mdogo ndiye anamuanza mkubwa.

Goodmorning /goodafternoon /Goodevening naona nazo ziko bomba na zinarandana na hekima za wahenga wetu .

Vitendo sioni shida hata kama tungekuwa tunarambana miguu haina shida kama kiini ni heshima.
Tatizo hii salamu kongwe asili yake inaonekana ni heshima mzizi wake ni enzi za utumwa.
Ingekuwa hata assalam-o-alaikum ambayo inamaana ya kutakiana kheri japo imegeuzwa kuwa salamu ya kidini. Kwa nini tusingechukua salamu zenye tafsiri tija kuliko ambazo tafsiri na asili ni utatautata.

Ndio maana nawaza Kilughalugha.
 
Back
Top Bottom