Hivi kuna haja ya kuendelea kuwanunulia viongozi g8?

Biz2geza

Senior Member
Oct 12, 2011
117
20
Wakati wa awamu ya Tatu wananchi walipigia kelele sana matumizi makubwa ya serikali kunulia wakubwa,Rais,mawaziri,wakuu wa idara,mashirika,wakuu wa mikoa,na wakuu wa idara mbali mbali kwa maana kwamba matumizi haya hayakuwa yenye Tija.Utetezi uliyotolewa na Rais by then ni kwamba kutokana na ukubwa wa nchi yetu na barabara zetu kuwa chakavu inawalazimu kununu hayo magari ya kifahari ilikusudi hawa viongozi wawe Confortable wanapokuwa wanasafiri ili waweze kufikiria vizuri na kutoa michango ambao ingeliletea Tija taifa letu.

Mytake:
  1. kwakuwa barabara nyingi ambazo zinaunganisha mikoa yote zimeshakuwa katika kiwango cha lami ambapo leo hii unaweza kuchimba Dar/mwanza kwa G100 ukafika upo fresh.Agenda ya ubovu wa barabara inapotea.Swali: kuna haja ya kuendelea kununua hayo magari?
  2. Baadala ya wao wanapokuwa wanasafiri na hayo magari kufikiria na kutafakari na kufikiria juu ya mustakabali wa Taifa letu wao wanakula mbonji....full kipupwe.Na haya yote yanayojitokeza mpaka watu wanajiuliza kama kweli hawa viongozi wetu huwa wanapata muda wakufikiri kabla ya kutenda.
  3. Nashauri hili swala liangaliwe upya Pesa nyingi sana zinapote kununua na kuhudumia haya magari..Hi serikali tajiri wananchi maskini ....kila toleo jipya Toyota baada ya muda mfupi unaliona na number STK....
  4. Hivi ikitokea siku tukapewa gharama za magari haya na matengenezo yake tutashika midomo yetu wakati kuna shule ya msingi inawanafunzi 500 wanatumia choo kimoja.
Naomba kuwasilisha.
 
Back
Top Bottom