Hivi kukopa fedha nyingi na kutumia fedha hizo kugharamia miradi, huko mikopo hiyo ikilipwa na walalahoi, ndio kuchapa kazi?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,372
Hivi mtu kuingia ofisini na kukuta nchi inakopesheka na yeye kuamua kuendelea kukopa mpaka kuanza kuonywa juu ya ukopaji huo kuwa kuna hatari kwa nchi, na kutumia fedha hizo kugharamia miradi michache huku watakaolipa fedha hizo ni wananchi masikini. Je, huku ndio kuchapa kazi kwa kiongozi?

Yaani wewe unaingia ofisini, na kabla hujafanya jitihada za kuongeza uzalishaji katika nchi yako ili kuongeza mapato ya Serikali, unaanza kukopa halafu wafuasi wako wanatuambia unachapa kazi. Hivi huu sio uongo wa mchana kweupe?

Cha ajabu, baadhi ya miradi unayotekeleza ilibuniwa na Serikali iliyopita au ni ilani ya chama chako. Sasa wewe kukopa kutekeleza hiyo miradi huku watakaolipa fedha hizo ni wananchi masikini wa nchi yako. Je, huo ndio uchapa kazi?

Kama huu ndio uchapakazi. Je, wale viongozi wanaoingia madarakani na kukuta nchi ina hali mbaya kiuchumi na kuja na mipango na mikakati na kuisimamia kuhakikisha uchumi wa nchi na maisha watu wake vinaboreka, viongozi wa aina sasa nao watasemaje?

Na wale ambao nchi zao zinazalisha kutosheleza soko la ndani na hata kuuza bidhaa nje, viongozi hawa na wafuasi wao nao watasemaje?

Tanzagiza inanishangaza sana!!!
 
Tena mpaka tunahamishia vote 20 ili tu isikaguliwe!!!
Kitendo cha kuhamishia fedha vote 20 bila kufuata utaratibu nao in sawa na wizi tuu kama ule wa kuhamisha kivuko kupeleka jeshini ili kuua mjadala na uchunguzi wa tuhuma za ufisadi katika manunuzi yake kwani kivuko hicho kinapewa hadhi ya vifaru au ndege za kivita zisizohojiwa.
 
Kitendo cha kuhamishia fedha vote 20 bila kufuata utaratibu nao in sawa na wizi tuu kama ule wa kuhamisha kivuko kupeleka jeshini ili kuua mjadala na uchunguzi wa tuhuma za ufisadi katika manunuzi yake kwani kivuko hicho kinapewa hadhi ya vifaru au ndege za kivita zisizohojiwa.
Wakitoka ofisini, wakija wengine, watakuja kuchunguza mambo haya ya kuchapa kazi.
 
Cha msingi kukopa na kuitumia kwenye maendeleo endelevu na sio kukopa hela za kuzunguka huko na huko ili kula bata.

Hakuna nchi imeendelea bila kukopa. Na kila nchi inakopa. Malekani wanakopa. China wanakopa.

Hata matajiri wanamadeni ya kufa mtu.

Umuhimu wa kukopa
1. Kufanya uwekezaji mkubwa bila kuathiri uwekezaji ulipo.
2. Kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ili kukabiliana na ongezeko la watu
3. Kusogeza huduma za jamii kwa wananchi kwa mda mfupi. Mfano.. maji, dawa, n.k
4. Kuongeza uwezo wa kuzarisha kwa kutengeneza miundombinu.
5. Kushindana na mataifa katika kukusanya mapato.. mfano Kenya tunashindana nao kwenye upitishaji wa mizigo bandarini kuelekea nchi jirani.

Unahitaji elimu zaidi? Salary Slip
 
Cha msingi kukopa na kuitumia kwenye maendeleo endelevu na sio kukopa hela za kuzunguka huko na huko ili kula bata.

Hakuna nchi imeendelea bila kukopa. Na kila nchi inakopa. Malekani wanakopa. China wanakopa.

Hata matajiri wanamadeni ya kufa mtu.

Umuhimu wa kukopa
1. Kufanya uwekezaji mkubwa bila kuathiri uwekezaji ulipo.
2. Kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ili kukabiliana na ongezeko la watu
3. Kusogeza huduma za jamii kwa wananchi kwa mda mfupi. Mfano.. maji, dawa, n.k
4. Kuongeza uwezo wa kuzarisha kwa kutengeneza miundombinu.
5. Kushindana na mataifa katika kukusanya mapato.. mfano Kenya tunashindana nao kwenye upitishaji wa mizigo bandarini kuelekea nchi jirani.

Unahitaji elimu zaidi? Salary Slip
Umejibu kipropaganda sana!!
 
Hili mtu kuingia ofisini na kukuta nchi inakopesheka na yeye kuamua kukopa mpaka kuanza kuonywa juu ya kukopa huko kuwa kuna hatari kwa nchi, na kutumia fedha hizo kugharamia miradi michache huku watakaolipa fedha hizo ni wananchi masikini,je huku ndio kuchapa kazi kwa kiongozi?

Yaani wewe unaingia ofisini, na kabla hujafanya jitihada za kuongeza uzalishaji katika nchi yako ili kuongeza mapato ya serikali,unaanza kukopa alafu wafuasi wako wanmatuambia unachapa kazi,hivi huu sio uongo wa mchana kweupe?

Cha ajabu,baadhi ya miradi unayotekeleza ilibuniwa na serikali iliyopita au ni ilani ya chama chako,sasa wewe kukopa kutekeleza hiyo miradi huku watakaolipa fedha hizo ni wananchi masikini wa nchi yako huo ndio uchapa kazi?

Kama huu ndio uchapakazi,je,na wale viongozi wanaoingia madarakani na kukuta nchi ina hali mbaya kiuchumi na kuja na mipango na mikakati na kuisimamia kuhakikisha uchumi wa nchi na watu wake vinaboreka,viongozi wa aina sasa nao watasemaje?

Na wale ambao nchi zao zinazlisha kutosheleza soko la ndani na hata kuuza bidhaa nje,viongozi hawa na wafuasi wao nao watasemaje?

Tanzagiza inanishangaza sana!!!
Kweli mkuu, mbona Leo Morogoro wameshindwa kuwajali wanyonge, hata ambulance hakuna
 
Hili mtu kuingia ofisini na kukuta nchi inakopesheka na yeye kuamua kukopa mpaka kuanza kuonywa juu ya kukopa huko kuwa kuna hatari kwa nchi, na kutumia fedha hizo kugharamia miradi michache huku watakaolipa fedha hizo ni wananchi masikini,je huku ndio kuchapa kazi kwa kiongozi?

Yaani wewe unaingia ofisini, na kabla hujafanya jitihada za kuongeza uzalishaji katika nchi yako ili kuongeza mapato ya serikali,unaanza kukopa alafu wafuasi wako wanmatuambia unachapa kazi,hivi huu sio uongo wa mchana kweupe?

Cha ajabu,baadhi ya miradi unayotekeleza ilibuniwa na serikali iliyopita au ni ilani ya chama chako,sasa wewe kukopa kutekeleza hiyo miradi huku watakaolipa fedha hizo ni wananchi masikini wa nchi yako huo ndio uchapa kazi?

Kama huu ndio uchapakazi,je,na wale viongozi wanaoingia madarakani na kukuta nchi ina hali mbaya kiuchumi na kuja na mipango na mikakati na kuisimamia kuhakikisha uchumi wa nchi na watu wake vinaboreka,viongozi wa aina sasa nao watasemaje?

Na wale ambao nchi zao zinazlisha kutosheleza soko la ndani na hata kuuza bidhaa nje,viongozi hawa na wafuasi wao nao watasemaje?

Tanzagiza inanishangaza sana!!!
leo mpumzishe kidogo baba wa watu tumefiwa
 
Back
Top Bottom