Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,400
Duh...tehtehtehtehteh...watu mna 'roho' ngumu...tehtehtehteh...Ila ushauri wangu kwa wengi ambao hawafahamu ni kuwa wote wale wanaoishi karibu na bahari wako katika mazingira hatarishi...Ndugu yangu unakumbuka kile kilichotokea kule Indonesia nadhani mwanzoni mwa miaka ya 2000 kutokana na tsunami?/ Bahari au mawimbi yake yalikuja kwa kasi zaidi ya futi 10 juu na kuua maelfu kwa maelfu ya watu...ikitokea hapa Dar walioko Kigamboni, masaki, msasani, Kawe, mikocheni, oysterbay, kunduchi, Bunju, city centre, kariakoo nk wataipatapata..tehtehtehtehtehteh
Mkuu, Tsunami inatokana na tetemeko la ardhi kwenye huo mkanda wake ulosambaa kutoka Bangladesh, India, Malaysia, Myanmar, Thailand, Sri Lanka na Maldives.
Sisi hatupo kwenye mkanda huo.
Nimeweka kabisa kila kitu kwenye mapendekezo ya mradi wangu wa kisiwa hichi kuwa cha utalii mahali hapo.
Nasubiria majibu kutoka serikalini na wamekuwa wazito kwelikweli kurudi na majibu naona hawataki kupaachia mahali hapo.