Hivi inakuwaje mtu aliyetamani matajiri waishi kama mashetani leo hii atamani aache mabilionea wasiopungua 100 hadi kipindi chake kitakapoisha?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Tumemsikia wenyewe wakati anahutubia wafanyibiashara aliowaalika Ikulu hivi karibuni akiwaambia kuwa anatamani, kipindi anatoka madarakani awaache wafanyibiashara mabilionea wakiongezeka nchini, ikiwezekana awaache mabilionea wasiopungua 100, wakati anaondoka madarakani mwaka 2025!

Nimekuwa nikijiuliza sana, si ndiyo huyu huyu mtu, ambaye siku za nyuma, aliwahi kutamka kuwa anatamani wafanyibiashara matajiri, waliokuwa wakiishi kama malaika, waishi kama mashetani, katika awamu yake?

Hivi so ndiyo huyu huyu aliyesema, yuko tayari kuona anapokea meli moja bandarini, inayoweza kulipa kodi, kuliko kuona meli 100, zisizolipa kodi??

Katika kikao hicho cha wafanyibiashara, walieleza kero zao nyingi kuhusiana na namna wanavyonyanyaswa na hao tumaoambiwa ni wakadiriaji kodi, watu wa TRA, ambao walidaiwa kuwa hawana ubinadamu hata kidogo wakati wa ukadiriaji wao kodi

Waliendelea kueleza wafanyibiashara hao kuwa hao TRA wamekuwa wanyama zaidi ya "Israel" kwa namna wanavyokadiria kodi kubwa, kiasi kilichofanya wafanyibiashara wengi wafunge biashara zao

Najua kuwa unyama huo wa watu wa TRA ulikuwa na "full blessings" za Mkuu, lakini nimeshangaa majuzi akiwaruka maili 100, hao TRA, kuwa eti ni wao wenyewe wanaojipangia kodi kubwa zisizoweza kulipika!

Akaendelea kueleza kuwa hakuna Taifa lolote lililopata maendeleo duniani, bila kutegemea sekta binafsi

Pengine tuseme kuwa Mkulu ameona pato la Taifa linazidi "kukauka" kwenye hazina ya Taifa, kutokana na hizi kauli za kinyama za hao watu wa TRA kuwa lipa kodi au funga biashara..........

Hao wafanyibiashara waliona hawana "option" nyingine zaidi ya kufunga biashara zao kwa kuwa hizo kodi walizokadiriwa nazo hazilipiki!

Hebu tembelea eneo maarufu kwa biashara nchi hii eneo la Kariakoo uone namna wafanyibiashara kwa maelfu, namna wanavyofunga biashara zao, kutokana na makadirio ya kodi ya "kinyama" za hao watoza ushuru

Ni hayo tu maoni yangu
 
One word Mkuu KULA

Tumemsikia wenyewe wakati anahutubia wafanyibiashara aliowaalika Ikulu hivi karibuni akiwaambia kuwa anatamani, kipindi anatoka madarakani awaache wafanyibiashara mabilionea wakiongezeka nchini, ikiwezekana awaache mabilionea wasiopungua 100, wakati anaondoka madarakani, mwaka 2025

Nimekuwa nikijiuliza sana, so nduyu huyu huyu mtu, ambaye siku za nyuma, aliwahi kutamka kuwa anatamani wafanyibiashara matajiri, waliokuwa wakiishi kama malaika, waishi kama mashetani, katika awamu yake?

Hivi so ndiyo huyu huyu aliyesema, yuko tayari kuona anapokea meli moja bandarini, inayoweza kulipa kodi, kuliko kuona meli 100, zisizolipa kodi??

Katika kikao hicho cha wafanyibiashara, walieleza kero zao nyingi kuhusiana na namna wanavyonyanyaswa na hao tumaoambiwa ni wakadiriaji kodi, watu wa TRA, ambao walidaiwa kuwa hawana ubinadamu hata kidogo wakati wa ukadiriaji wao kodi

Waliendelea kueleza wafanyibiashara hao kuwa hao TRA wamekuwa wanyama zaidi ya "Israel" kwa namna wanavyokadiria kodi kubwa, kiasi kilichofanya wafanyibiashara wengi wafunge biashara zao

Najua kuwa unyama huo wa watu wa TRA ulikuwa na "full blessings" za Mkuu, lakini nimeshangaa majuzi akiwaruka maili 100, hao TRA, kuwa eti ni wao wenyewe wanaojipangia kodi kubwa zisizoweza kulipika!

Pengine tuseme kuwa Mkulu ameona pato la Taifa linazidi "kukauka" kwenye hazina ya Taifa, kutokana na hizi kauli za kinyama za hao watu wa TRA kuwa lipa kodi au funga biashara

Hao wafanyibiashara waliona hawana "option" nyingine zaidi ya kufunga biashara zao kwa kuwa hizo kodi walizokadiriwa nazo hazilipiki!

Hebu tembelea eneo maarufu kwa biashara nchi hii eneo la Kariakoo uone namna wafanyibiashara kwa maelfu, namna wanavyofunga biashara zao, kutokana na makadirio ya kodi ya "kinyama" za hao watoza ushuru

Ni hayo tu maoni yangu
 
Hivi ukiweka mazingira yasiyo rafiki yanayosababisha wafanyibiashara wafunge biashara zao, hivi unadhani ni rahisi kuwarudisha wafanyibiashara hao kwa kauli zako za "kilaghai" kuwa eti ni hao hao TRA wenyewe ndiyo waliokuwa wanakadiria kodi kubwa zisizoweza kulipika??

Wakati watanzania wote wanajua kuwa wewe ndiyo unaowapa kiburi hao TRA ya kuwanyanyasa wafanyibiashara
 
Kiukweli ni kuwa Mkulu ameshafanya "damage" kubwa ya kutisha kutokana na maagizo yake kwa watu wake wa TRA, ambayo kwa sasa hayawezi kurekebishika kwa kauli zake nyepesi kuwa eti anatamani "kuwatengeneza" mabilionea wengi zaidi katika kipindi chake cha utawala!
 
Mystery unatumia nguvu nyingi na hiyo sumu unayoishi nayo inakumaliza kila siku

Sidhani kama kwa akili zako timamu za kuzaliwa na bimkubwa wetu mama yako mzazi kuwa unaamini pasi shaka kuwa matajiri wote wamepata utajiri kihalali kabisa bila kufisadi. Ikiwa unaamini matajiri wote nk wasafi basi ungehairishwa kuzaliwa

Lakini kama matajiri hawa wamepata utajiri kwa uhalali na wanalipa kodi TRA sidhani pia kama kuna kosa kuwainua na kuwalinda


unafikiri kati ya hizi category mbili ipi unadhani wako waliopaswa kushushwa?

ulimuuliza JPM ni wa aina ipi hao alitaka washushwe?

Alfajiri yote unaamka upate tu wa kuku support ilinmradi usikie raha, ni tatizo
 
Janga kubwa la Taifa huyo ndani ya miaka minne athari kubwa alizozifanya zipo kila kona zikiwemo uchumi na kuweka dosari kubwa kwenye amani na mshikamamo wa Watanzania. Fikiria akikaa madarakani miaka 10 ataicha nchi katika hali gani kwa speed hii kubwa ya uharibifu anoufanya.

Kiukweli ni kuwa Mkulu ameshafanya "damage" kubwa ya kutisha kutokana na maagizo yake kwa watu wake wa TRA, ambayo kwa sasa hayawezi kurekebishika kwa kauli zake nyepesi kuwa eti anatamani "kuwatengeneza" mabilionea wengi zaidi katika kipindi chake cha utawala!
 
Mystery unatumia nguvu nyingi na hiyo sumu unayoishi nayo inakumaliza kila siku

Sidhani kama kwa akili zako timamu za kuzaliwa na bimkubwa wetu mama yako mzazi kuwa unaamini pasi shaka kuwa matajiri wote wamepata utajiri kihalali kabisa bila kufisadi. Ikiwa unaamini matajiri wote nk wasafi basi ungehairishwa kuzaliwa

Lakini kama matajiri hawa wamepata utajiri kwa uhalali na wanalipa kodi TRA sidhani pia kama kuna kosa kuwainua na kuwalinda


unafikiri kati ya hizi category mbili ipi unadhani wako waliopaswa kushushwa?

ulimuuliza JPM ni wa aina ipi hao alitaka washushwe?

Alfajiri yote unaamka upate tu wa kuku support ilinmradi usikie raha ni tatizo
Yeye mwenyewe JPM amekiri hadharani kuwa hakuna Taifa lolote lililopata maendeleo bila kutegemea sekta binafsi

Sasa ninachohoji, iwapo mkulu anaamini hivyo, alikuwa na sababu zipi za kusema katika utawala wake atahakikisha matajiri waliokuwa wakiishi kama malaika wataishi kama mashetani??

Matokeo yake ndiyo haya tunayoyaona maeneo mbalimbali nchini wa matajiri kuishi kama mashetani kwa wafanyibiashara hao kufunga biashara zao!

Ninachohoji kingine, ni kwa vipi mtu yule yule aliyekuwa "adui" wa wafanyibiashara hao, leo ajifanye rafiki yao mkubwa??

Au ni kwa kuwa maji yeshamfika shingoni kwa kuona hazina "nyeupe" kutokana na walipa kodi kufunga biashara zao??
 
Nadhani mkulu hakuna na nia kila mfanyabiashara tajiri kuishi kama shetani, isipokuwa wafanyabiashara ambao walikuwa wakwepa kodi alitaka watimize wajibu wao. Na kama tunakumbuka, mara baada ya kuingia magogoni, alitoa orodha ya wafanyabiashara ambao walikuwa wamekwepa kodi katika kipindi fulani na kiwango walichokwepa.
Mind you kuna wafanyabiashara huko nyuma walikuwa untouchable wakiwa na Inland Container Deport zao, na it was as if TRA haikuwa inahusika nao.

Ni Mkulu huyuhuyu wakati anaingia madarakani alikaa na wafanyabiashara (Confederation of Tanzania Industries) akiwataka waji-position kufanya biashara kwenye tenure yake.

Ni Mkulu huyuhuyu wakati mmoja aliwataka wahandisi na waandishi wa habari kama wanaweza kufungua kampuni za kuwa sehemu ya mnyororo wa thamani kuwa ku-supply uhitaji wa huduma na bidhaa katika majenzi ya SGR, bomba la mafuta, ujenzi wa Dodoma wakae mkao wa kula.

Ni Mkulu huyuhuyu amewahi kutoa changamoto wa wafanyabiashara kuingia katika utengenezaji wa madawa na vifaa tiba; akimtaka waziri wa Afya kuratibu zoezi hilo na kuitaka NHIF iwezeshe mikopo ya ujenzi wa viwanda wa vifaa tiba au madawa.

Swali moja tu ambalo Mkulu mpaka leo hajafanya kwa wananchi wa kawaida ikijumuisha hata wazee wenye profile za mzee Dr. Mzindakaya, ni namna gani ya kumfikia yeye pale watendaji wa chini yake wanapozingua ku-facilitate mchakato wa kuweka viwanda.

Ni namna gani hiyo mikopo ili viwanda vya madawa au vifaa tiba vianzishwe au kuanzisha quarrying projects ili kuuza kokoto kwa majenzi ya SGR, uwanja wa dodoma wa mpira, ujenzi wa mji wa serikali, ujenzi wa Stiglaz. Basically haina maana pale wachina wajenga na wakati huo huo wanakuwa na quarry zao kusaga mawe yetu. Ingkuwa busara local content itumike kwa serikali kuwezesha watu wake wauze walau kokoto, zege ili wakandarasi wageni wabaki na core function ya kusimamia mradi.

Hata juzi akiwa na wafanyabiashara aliweka wazi yuko supportive hata kumwandika mtu barua yake binafsi ili awekeze kwenye kiwanda ambacho kitakuwa chanzo cha ajira, kodi na kupunguza imports kama za viatu vya majeshi.
Suala ni namna gani mkulu anapatikana kwa tabia ya watendaji wa ofisi zetu ukiandika barua huwa hawajibu. Unless angetoa backdoor channel kama kwa yule mzee wa Mbeya akiwa na wafanyabiashara alimpa simu ya mpambe wake, kama mzee atapata usumbufu ampigie Kanali moja kwa moja. Kwa mlango huohuo angetoa avenue kwa mtu mwenye very outstanding investment proposal afungue mlango ili zimfikie.

Tuna uhitaji wa tani zaidi ya laki 4 za mafuta na tuna wahindi ambao wanalangua ufuta na kuuza India wakati kumbe tungepata project financing tungezalisha mafuta ya kula kwa domestic use/export.

Tuna-korosho na kuna watu wenye interest ya kuanzisha processing industries lakini hakuna project financing kupata equipment kufanya processing na packaging ili kuuza soko la Ulaya kupata foreign currency.

Mkulu ana nia njema sana, ila kuna namna imekuwa kazi kubwa kupata ili a-facilitate mambo kwa haraka pale ambapo watendaji wake wanasuasua.
 
Nadhani mkulu hakuna na nia kila mfanyabiashara tajiri kuishi kama shetani, isipokuwa wafanyabiashara ambao walikuwa wakwepa kodi alitaka watimize wajibu wao. Na kama tunakumbuka, mara baada ya kuingia magogoni, alitoa orodha ya wafanyabiashara ambao walikuwa wamekwepa kodi katika kipindi fulani na kiwango walichokwepa.
Mind you kuna wafanyabiashara huko nyuma walikuwa untouchable wakiwa na Inland Container Deport zao, na it was as if TRA haikuwa inahusika nao.

Ni Mkulu huyuhuyu wakati anaingia madarakani alikaa na wafanyabiashara (Confederation of Tanzania Industries) akiwataka waji-position kufanya biashara kwenye tenure yake.

Ni Mkulu huyuhuyu wakati mmoja aliwataka wahandisi na waandishi wa habari kama wanaweza kufungua kampuni za kuwa sehemu ya mnyororo wa thamani kuwa ku-supply uhitaji wa huduma na bidhaa katika majenzi ya SGR, bomba la mafuta, ujenzi wa Dodoma wakae mkao wa kula.

Ni Mkulu huyuhuyu amewahi kutoa changamoto wa wafanyabiashara kuingia katika utengenezaji wa madawa na vifaa tiba; akimtaka waziri wa Afya kuratibu zoezi hilo na kuitaka NHIF iwezeshe mikopo ya ujenzi wa viwanda wa vifaa tiba au madawa.

Swali moja tu ambalo Mkulu mpaka leo hajafanya kwa wananchi wa kawaida ikijumuisha hata wazee wenye profile za mzee Dr. Mzindakaya, ni namna gani ya kumfikia yeye pale watendaji wa chini yake wanapozingua ku-facilitate mchakato wa kuweka viwanda.

Ni namna gani hiyo mikopo ili viwanda vya madawa au vifaa tiba vianzishwe au kuanzisha quarrying projects ili kuuza kokoto kwa majenzi ya SGR, uwanja wa dodoma wa mpira, ujenzi wa mji wa serikali, ujenzi wa Stiglaz. Basically haina maana pale wachina wajenga na wakati huo huo wanakuwa na quarry zao kusaga mawe yetu. Ingkuwa busara local content itumike kwa serikali kuwezesha watu wake wauze walau kokoto, zege ili wakandarasi wageni wabaki na core function ya kusimamia mradi.

Hata juzi akiwa na wafanyabiashara aliweka wazi yuko supportive hata kumwandika mtu barua yake binafsi ili awekeze kwenye kiwanda ambacho kitakuwa chanzo cha ajira, kodi na kupunguza imports kama za viatu vya majeshi.
Suala ni namna gani mkulu anapatikana kwa tabia ya watendaji wa ofisi zetu ukiandika barua huwa hawajibu. Unless angetoa backdoor channel kama kwa yule mzee wa Mbeya akiwa na wafanyabiashara alimpa simu ya mpambe wake, kama mzee atapata usumbufu ampigie Kanali moja kwa moja. Kwa mlango huohuo angetoa avenue kwa mtu mwenye very outstanding investment proposal afungue mlango ili zimfikie.

Tuna uhitaji wa tani zaidi ya laki 4 za mafuta na tuna wahindi ambao wanalangua ufuta na kuuza India wakati kumbe tungepata project financing tungezalisha mafuta ya kula kwa domestic use/export.

Tuna-korosho na kuna watu wenye interest ya kuanzisha processing industries lakini hakuna project financing kupata equipment kufanya processing na packaging ili kuuza soko la Ulaya kupata foreign currency.

Mkulu ana nia njema sana, ila kuna namna imekuwa kazi kubwa kupata ili a-facilitate mambo kwa haraka pale ambapo watendaji wake wanasuasua.
Obviously wafanyibiashara wengi wamepata utajiri wao kwa njia ambazo hazijanyooka

Hata hivyo kuna haja gani kujenga uhasama na kundi hilo la watu,wakati tunajua mchango wao kwa Taifa kuwa ni mkubwa sana, kwa upande wa ajira za wazawa na kodi wanazotoa kwa serikali??

Hata Yesu Kristo aliwahoji wale watu waliotaka kumpiga mawe yule mama mzinzi, kuwa yeyote kati yao ambaye hajatenda dhambi tokea kuzaliwa kwake, awe wa kwanza kumrushia mawe yule mama......

Unajua nini kilitokea??

Ni kwa mmoja baada ya mwingine, kuondoka kimya kimya, kutokana na kusutwa na nafsi zao

Turudi kwenye mada yetu, hivi ikiwa tutawa-judge hao wafanyibiashara wakubwa kutokana na matendo yao ya awali, ni nani atakayesalimika, kutokana na makosa ambayo aliyafanya hapo awali, including yeye mwenyewe Mkulu??
 
Obviously wafanyibiashara wengi wamepata utajiri wao kwa njia ambazo hazijanyooka

Hata hivyo kuna haja gani kujenga uhasama na kundi hilo la watu,wakati tunajua mchango wao kwa Taifa kuwa ni mkubwa sana, kwa upande wa ajira za wazawa na kodi wanazotoa kwa serikali??

Hata Yesu Kristo aliwahoji wale watu waliotaka kumpiga mawe yule mama mzinzi, kuwa yeyote kati yao ambaye hajatenda dhambi tokea kuzaliwa kwake, awe wa kwanza kumrushia mawe yule mama......

Unajua nini kilitokea??

Ni kwa mmoja baada ya mwingine, kuondoka kimya kimya, kutokana na kusutwa na nafsi zao

Turudi kwenye mada yetu, hivi ikiwa tutawa-judge hao wafanyibiashara wakkubwa kutokana na matendo yao ya swali, ni nani atakayesalimika??
Sidhani kama kuna kujengeana uhasama boss wangu.
Kutolipa kodi ni kosa la kisheria na nchi za wenzetu watu huwa wanafungwa jela.

Mkulu akijua watu wamekwepa, wengine wanaghushi na kuwa na vitabu viwili viwili, wengine wanaghushi na kudai VAT returns wakati hawastahili. Alichofanya ni kuwataka walipe kodi ili biashara ziendelee na kumpa list waziri mkuu wale waliokuwa wamepokea malipo ya VAT refunds bila stahili.

Kama angetumia rungu la kisheria kumtaka DPP awafikishe mahakamani kwa mujibu wa taratibu; sijui kama buz sector ingetulia. To be fair, Mkulu anataka kodi na kwa makampuni makubwa kama Airtel amekaa nao mezani kwa vikao kadhaa kuonesha wapi tumepigwa na haki yatu ilikuwa ipi.

Marekani wakwepa kodi, huwa ni suala mahakamani na kifungo ikithibitika.

Mkulu yuko fair sana tu. Na hata juzi alitoa kama angalizo, hivi akiweka mambo hadharani ya nini wafanyabiashara wanafanya kuna atakaepona kweli....

Anyway... tukubali. Sekta ya biashara Tanzania "sanaa" iko juu sana. Watu wananunua vitu mil 200, mtu anapewa risit ya mil 50...
Watu wananunua vitu mil 50, mzigo unapelekwa na gari la muuzaji kana kwamba unaelekea kwenye warehouse, kumbe jamaa wanakwepa kodi... hii ndiyo Tanzania yetu
 
Binadamu kukosea ni jambo la kawaida, juzi aliwaona hawafai leo amefunguka ameona faida yao na anawakubali.
 
Binadamu kukosea ni jambo la kawaida, juzi aliwaona hawafai leo amefunguka ameona faida yao na anawakubali.
Lakini Mkuu wa nchi unapaswa wakati wote kuwa makini sana kwa hotuba zako kwa Taifa

Siyo "kuropoka" ovyo kuwa unahitaji matajiri waishi kama mashetani na wanapoishi kama mashetani, wewe tena "unawapigia" magoti, kuwa ungependa uwaache mabilionea wengi, kipindi unaondoka madarakani
 
Ungejiulizalje aikuwa anaongelea wale ambao hawakuzipata kwa uhalali.. na ushaidi upo unazidi kuendelea.
Hivi mmekuwaje siku hizi wengi humu ni LT hadi mnaboaaaaaa.. kisa mmefungua uzi kujadili kupitia maumivu wa ufisadi na kuisoma namba. Mumtaje tu Rais ndio bonbaaa
 
Hivi ukiweka mazingira yasiyo rafiki yanayosababisha wafanyibiashara wafunge biashara zao, hivi unadhani ni rahisi kuwarudisha wafanyibiashara hao kwa kauli zako za "kilaghai" kuwa eti ni hao hao TRA wenyewe ndiyo waliokuwa wanakadiria kodi kubwa zisizoweza kulipika??
Huyo mzee inabidi tumzoee tu na kauli zake za kilaghai.
 
Mkuu umesahau tunaelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa pia na ule wa 2020?
Tumemsikia wenyewe wakati anahutubia wafanyibiashara aliowaalika Ikulu hivi karibuni akiwaambia kuwa anatamani, kipindi anatoka madarakani awaache wafanyibiashara mabilionea wakiongezeka nchini, ikiwezekana awaache mabilionea wasiopungua 100, wakati anaondoka madarakani mwaka 2025!

Nimekuwa nikijiuliza sana, si ndiyo huyu huyu mtu, ambaye siku za nyuma, aliwahi kutamka kuwa anatamani wafanyibiashara matajiri, waliokuwa wakiishi kama malaika, waishi kama mashetani, katika awamu yake?

Hivi so ndiyo huyu huyu aliyesema, yuko tayari kuona anapokea meli moja bandarini, inayoweza kulipa kodi, kuliko kuona meli 100, zisizolipa kodi??

Katika kikao hicho cha wafanyibiashara, walieleza kero zao nyingi kuhusiana na namna wanavyonyanyaswa na hao tumaoambiwa ni wakadiriaji kodi, watu wa TRA, ambao walidaiwa kuwa hawana ubinadamu hata kidogo wakati wa ukadiriaji wao kodi

Waliendelea kueleza wafanyibiashara hao kuwa hao TRA wamekuwa wanyama zaidi ya "Israel" kwa namna wanavyokadiria kodi kubwa, kiasi kilichofanya wafanyibiashara wengi wafunge biashara zao

Najua kuwa unyama huo wa watu wa TRA ulikuwa na "full blessings" za Mkuu, lakini nimeshangaa majuzi akiwaruka maili 100, hao TRA, kuwa eti ni wao wenyewe wanaojipangia kodi kubwa zisizoweza kulipika!

Akaendelea kueleza kuwa hakuna Taifa lolote lililopata maendeleo duniani, bila kutegemea sekta binafsi

Pengine tuseme kuwa Mkulu ameona pato la Taifa linazidi "kukauka" kwenye hazina ya Taifa, kutokana na hizi kauli za kinyama za hao watu wa TRA kuwa lipa kodi au funga biashara..........

Hao wafanyibiashara waliona hawana "option" nyingine zaidi ya kufunga biashara zao kwa kuwa hizo kodi walizokadiriwa nazo hazilipiki!

Hebu tembelea eneo maarufu kwa biashara nchi hii eneo la Kariakoo uone namna wafanyibiashara kwa maelfu, namna wanavyofunga biashara zao, kutokana na makadirio ya kodi ya "kinyama" za hao watoza ushuru

Ni hayo tu maoni yangu
 
Walisha zoea kuwaona watanzania ni kondooo
Hivi ukiweka mazingira yasiyo rafiki yanayosababisha wafanyibiashara wafunge biashara zao, hivi unadhani ni rahisi kuwarudisha wafanyibiashara hao kwa kauli zako za "kilaghai" kuwa eti ni hao hao TRA wenyewe ndiyo waliokuwa wanakadiria kodi kubwa zisizoweza kulipika??
 
Kiukweli ni kuwa Mkulu ameshafanya "damage" kubwa ya kutisha kutokana na maagizo yake kwa watu wake wa TRA, ambayo kwa sasa hayawezi kurekebishika kwa kauli zake nyepesi kuwa eti anatamani "kuwatengeneza" mabilionea wengi zaidi katika kipindi chake cha utawala!
Asha watengeneza masikini wengi sana na hao mabilionea labda wa kwenye ndoto
 
Serikali ya ccm hakuna aliye msafi na wataanza wamesha amua kuifuta kabisa kwenye uso wa dunia
Mystery unatumia nguvu nyingi na hiyo sumu unayoishi nayo inakumaliza kila siku

Sidhani kama kwa akili zako timamu za kuzaliwa na bimkubwa wetu mama yako mzazi kuwa unaamini pasi shaka kuwa matajiri wote wamepata utajiri kihalali kabisa bila kufisadi. Ikiwa unaamini matajiri wote nk wasafi basi ungehairishwa kuzaliwa

Lakini kama matajiri hawa wamepata utajiri kwa uhalali na wanalipa kodi TRA sidhani pia kama kuna kosa kuwainua na kuwalinda


unafikiri kati ya hizi category mbili ipi unadhani wako waliopaswa kushushwa?

ulimuuliza JPM ni wa aina ipi hao alitaka washushwe?

Alfajiri yote unaamka upate tu wa kuku support ilinmradi usikie raha, ni tatizo
 
H
Ungejiulizalje aikuwa anaongelea wale ambao hawakuzipata kwa uhalali.. na ushaidi upo unazidi kuendelea.
Hivi mmekuwaje siku hizi wengi humu ni LT hadi mnaboaaaaaa.. kisa mmefungua uzi kujadili kupitia maumivu wa ufisadi na kuisoma namba. Mumtaje tu Rais ndio bonbaaa
Hakuna utajiri wa njia ya halali.Tunadanganyana tu hapa.Jiulize tangu lini kwenye ubepari kuna utakatifu,uhalali,kukosekana kwa wizi,kukosekana kwa unyonyaji, kukosekana kwa utumwa na utwana,kukosekana kwa figisu na uchafu mwingine unaoujua?.

Utajiri hauchukuliwi kama udhanivyo.Nani hapa Tanzania ni tajiri halali?.Uhalali wake uko kwenye mtazamo upi?.Hanyonyi?,Au haibi?,Au hadhulumu?.Ni Mungu tu ndie ajuaye yale yaliyojificha juu ya matajiri.

Kwa kifupi ni kuwa, vile tutendewavyo na mfumo wa ubepari kwa kuanzia na nchi tajiri kwa maskini,ndivyo matajiri watutendeavyo sisi HAKUNA UTAJIRI HALALI
 
Back
Top Bottom