Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 14,176
- 25,919
Ningependa sana kujua kama huu umati ambao ulisimamisha uwanja wa ndege na Da es Salaam ulipewa kibali cha maandamano na polisi. Na je, Polisi walifanya intelijensia kujiridhisha kwamba wanachama wa Simba labda wasingefanya vurugu?
Nimetafakari juu ya hili kwa sababu Chadema au ACT Wazalendo wakisema wanataka kuandamana kwa amani, Polisi wanakuja na kila namna ya visingizio kuwakatalia. Utakuta wanatoa sababu kama mtavuruga shughuli za watu, mara intelijensia inasema kutakuwa na fujo na ujinga mwingine kama huo.
Na maandamano ya Yanga je, yalikuwa na kibali? Kiliombwa muda wa kutosha kabla ya kufanyika?
Hili la maandamano ya Yanga linaonyesha wazi kuwa Polisi mna mambo ya kujipendekeza sana kwa chama tawala. Kuna siku itawatokea puani. Wahedi Wahedi kabisa nyie.