Hivi huu mfumo wa EPICA ndio dudu gani?

Kashi

JF-Expert Member
Jan 6, 2013
897
743
Ndugu wana Jf ninashangazwa sana na hii serikali yetu kukurupuka katika matumizi ya teknolojia ambazo haina uwezo nazo.Leo ni wiki ya tatu tangu walimu na watumishi wengine wa Halmashauri waanze likizo zao lakini nauli bado hazijatolewa kisa mfumo wa EPICA umekata network.Kazi nyingi kwenye Mahalmashauri zimesimama kisa EPICA,kama imetushinda si turudie mfumo wa zamani tujipange upya? Najua hili litakuwa ni shinikizo tu la IFM kutumia madudu tusiyoyaweza.Naomba kuwasilisha.
 
Point less

EPICOR imeshawahi kunisababishia usumbufu mkubwa sana, kupata malipo yangu fulani Serikalini, maana niliambiwa pesa ipo lakini mtandao unawasumbua zaidi ya wiki tatu. Lakini wachunguzi wa masuala ya fedha za Serikali wanadai ishu siyo mtandao ishu ni kwamba Serikali ipo hoi financially kwahiyo Epicor imekuwa ni kama sababu tu, pia kuna habari kwamba mpaka sasa BOT hakuna Pesa ya Kutosha hivyo hata mishahara ya mwezi huu itachelewa ila wasemaji wameagizwa waseme mtandao unasumbua.
 
Hilo ni janga la taifa kwa kweli, kila kitu EPICA, EPICA sijui maana ya teknolojia ni nini kwani ninavyofahamu teknolojia huwa inarahisisha kazi na kufanya mambo yanakuwa haraka sana.

Kwa nchi yetu kila tunachokurupukia ni shida tupu badala ya kuleta unafuu.
 
EPICOR imeshawahi kunisababishia usumbufu mkubwa sana, kupata malipo yangu fulani Serikalini, maana niliambiwa pesa ipo lakini mtandao unawasumbua zaidi ya wiki tatu. Lakini wachunguzi wa masuala ya fedha za Serikali wanadai ishu siyo mtandao ishu ni kwamba Serikali ipo hoi financially kwahiyo Epicor imekuwa ni kama sababu tu, pia kuna habari kwamba mpaka sasa BOT hakuna Pesa ya Kutosha hivyo hata mishahara ya mwezi huu itachelewa ila wasemaji wameagizwa waseme mtandao unasumbua.

Nashangaa eti mtandao hakuna wakati tuna mkongo wa Taifa ambao tunaambiwa uko faste and efficient kwa asilimia kubwa.Sasa hivi malipo yaliyokuwa yanaandaliwa kwa siku 1 au 2 yanachukua mwezi hata zaidi.
 
Ndugu wana Jf ninashangazwa sana na hii serikali yetu kukurupuka katika matumizi ya teknolojia ambazo haina uwezo nazo.Leo ni wiki ya tatu tangu walimu na watumishi wengine wa Halmashauri waanze likizo zao lakini nauli bado hazijatolewa kisa mfumo wa EPICA umekata network.Kazi nyingi kwenye Mahalmashauri zimesimama kisa EPICA,kama imetushinda si turudie mfumo wa zamani tujipange upya? Najua hili litakuwa ni shinikizo tu la IFM kutumia madudu tusiyoyaweza.Naomba kuwasilisha.

Mkuu naamini hapo kwenye IFM ulimaanisha IMF.
 
Back
Top Bottom