Hivi hii ya Waziri Mkuu imekaaje?

Hivi hii ya Waziri Mkuu imekaaje?

Sizinga

Platinum Member
Joined
Oct 30, 2007
Posts
9,540
Reaction score
7,371
Spika anataka kufuta kabisa utaratibu wa maswali ya papo hapo kwa Waziri Mkuu bungeni, kigezo tu eti maswali mengi yanamdhalilisha PM.
Huu utaratibu alianza nao EL na yy ni mwanadamu maswali atakayoyaweza atajibu atayohitaji data hatajibu hapo, Pinda
akaikuta hiyo system nae akaikubali kwa kusema haina shinda. Sasa huyu Muh Makinda anataka kuifuta kabisa.
Swali: Kwani PM si yupo pale kwa ajili ya wananchi, na kwani wote wenye maswali ya papo hapo wana lengo la kumdhalilisha spika??au PM Pinda uwezo wake ni mdogo sana wa kutungua maswali ya papo hapo??kazoea kudesa??

Hii imekaaje wazee??
 
Wanaogopa maswali kutoka vichwa vya CDM maana ni magumu kwa kuwa yana uhalisia.
 
Pinda si mwanasiasa,pinda ni mtendaji,jambo hili litamtesa sana kwenye siasa za tanzania,ndio maana huwa anashindwa kutafuna maneno na kujikuta anaropoka,chukulia mfano wa kusema zanzibar si nchi,ni yeye aliyethubutu kusema vile maana wanasiasa wanaogopa ila yeye amelelewa katika kuwa mtendaji zaid ya kuwa mwanasiasa,na si pinda hata mawaziri wake wakiulizwa maswali ya NYONGEZA si mnawasikia majibu wanayoyatoaaaaaa.........
 
Kwa chama na serikali iliyokosa mwelekeo hawawezi kuendelea kukubali kuulizwa maswali kwani hawana majibu ya maswali yua watz..............jiulize ,km rais anaulizwa kwa nini watz ni masikini pamoja na kuwa na =rasilimali lukuki anajibu kuwa naye anashangaa huku anawalinda mafisadi unadhani w/mkuu atajibu nini hapo..............ukiona chama tawala na serikali yake hawapo tayari kushindanisshwa kwa hoja wakati wa uchaguzi ni kwa sababu hawana majibu ya matatizo ya watz...........dawa moja tu kuwatimua kikwete, mafisadi wenzake, vimbelembele na wasema uongo km makinda,pinda na wengine , kuwakamata na kuwafilisi mafisadi wote kwa kuanzia na kikwete, lowasa,rostam,change........
 
gafai hata utendaji labda kutumwa!

Pinda si mwanasiasa,pinda ni mtendaji,jambo hili litamtesa sana kwenye siasa za tanzania,ndio maana huwa anashindwa kutafuna maneno na kujikuta anaropoka,chukulia mfano wa kusema zanzibar si nchi,ni yeye aliyethubutu kusema vile maana wanasiasa wanaogopa ila yeye amelelewa katika kuwa mtendaji zaid ya kuwa mwanasiasa,na si pinda hata mawaziri wake wakiulizwa maswali ya NYONGEZA si mnawasikia majibu wanayoyatoaaaaaa.........
 
Spika wa Bunge ambaye kwa asilimia 99.9 anaitetea serikali kwa nini asifute utaratibu huo si ajabu na tulijua hilo linakuja
 
Spika wa Bunge ambaye kwa asilimia 99.9 anaitetea serikali kwa nini asifute utaratibu huo si ajabu na tulijua hilo linakuja
Huyo sio spika ni DIKTETA asiye na huruma na watanzania,kazi yake ni kuwalinda wanyonyaji.
 
Spika ameona hawana majibu ya kuridhisha umma, so anatumia kila mbinu kuiokoa serikali!
 
Hiyo ni attempt to block democracy. watanzania tuna haki ya kuhoji na sio mbunge anayehoji bali yeye katumwa na wananchi.
tuna haki ya kuelewa kila kitu katika taifa letu. vitu gani wanavyovificha tusivielewe. ina maana serikali ya magamba ina ufisadi
mkubwa na mambo ya uvunjaji wa haki za binadam wanaondelea kuufanya. hilo alikubaliki wanajaribu kuleta fantasy katika siasa.
 
Mh! Kazi kweli kweli makinda kapata uspika kwa sifa ya jinsia yake na woga kwa CCM yake hana sifa za uspika kwani sio "great thinker".
 
..maswali ya nyongeza hutokana na maswali ya msingi.

..kama umefanya/umesoma research kuhusu suala la msingi basi suala la nyongeza haliwezi kukushinda hata kidogo.

..maswali mengine ya nyongeza huulizwa na mbunge tofauti na yule aliyeuliza swali la msingi. kwa mtizamo wangu waziri makini will always be ahead of muuliza swali la nyongeza--especially kama siye aliyeuliza swali la msingi.

..kuna kipindi Waziri wa Fedha alikuwa na matatizo ya afya, nafasi yake ikakaimiwa na waziri mwingine. huyo Kaimu waziri[alishika wizara mbili ktk kipindi cha bunge] aliweza kujibu maswali yote ya msingi na nyongeza bila matatizo yoyote yale. Again, that was "back in the days."
 
Mheshiwa ametuasi watoto wenzake wa wakulima na ameungana na mafisadi kisha ameshika kasi ya ajabu
kuuendea uovu.
 
Pinda si mwanasiasa,pinda ni mtendaji,jambo hili litamtesa sana kwenye siasa za tanzania,ndio maana huwa anashindwa kutafuna maneno na kujikuta anaropoka,chukulia mfano wa kusema zanzibar si nchi,ni yeye aliyethubutu kusema vile maana wanasiasa wanaogopa ila yeye amelelewa katika kuwa mtendaji zaid ya kuwa mwanasiasa,na si pinda hata mawaziri wake wakiulizwa maswali ya NYONGEZA si mnawasikia majibu wanayoyatoaaaaaa.........

Sikubaliani nawe ng'o!!!!!! Pinda si mtendaji ila ni mwanasia. Mtendaji angekuwa na majibu ya maswali mengi anayoulizwa kwani mengi ni maswali ya kitendaji si ya kisiasa.
 
Pinda si mwanasiasa,pinda ni mtendaji,jambo hili litamtesa sana kwenye siasa za tanzania,ndio maana huwa anashindwa kutafuna maneno na kujikuta anaropoka,chukulia mfano wa kusema zanzibar si nchi,ni yeye aliyethubutu kusema vile maana wanasiasa wanaogopa ila yeye amelelewa katika kuwa mtendaji zaid ya kuwa mwanasiasa,na si pinda hata mawaziri wake wakiulizwa maswali ya NYONGEZA si mnawasikia majibu wanayoyatoaaaaaa.........

Sikubaliani nawe ng'o!!!!!! si mtendaji ni mwanasiasa. Mtendaji angekuwa na majibu ya maswali mengi anayoulizwa kwani mengi ni maswali ya kitendaji si ya kisiasa.
 
Makinda ni kada anaendesha Bunge kama kamati ya chama cha magamba, lakini pia wabunge wengi wa ccm hawajui wajibu wao au wanajifanya hawajui. Wamegeuka kuwa sehemu ya serikali, wakati Bunge ni mhimili unaoiangalia serikali, kuishauri na hata kuikemea pamoja na kazi ya kutunga sheria na kuridhia mikataba ya kumataifa sasa wao wanachojua ni kusema serikali hii haina shida ni sikivu lakini wanalalamika tunawaomba posho hawaoni umuhimu wa kujenga jamii ambayo si ombaomba kwa kuibana serikali ili raslimali zetu zitumike kuinua hali za wananchi. aswali kwa PM yatafutwa na Makinda ili kuilinda serikali isiyo na majibu kwa maswali ya watanzania
 
Pinda si mwanasiasa,pinda ni mtendaji,jambo hili litamtesa sana kwenye siasa za tanzania,ndio maana huwa anashindwa kutafuna maneno na kujikuta anaropoka,chukulia mfano wa kusema zanzibar si nchi,ni yeye aliyethubutu kusema vile maana wanasiasa wanaogopa ila yeye amelelewa katika kuwa mtendaji zaid ya kuwa mwanasiasa,na si pinda hata mawaziri wake wakiulizwa maswali ya NYONGEZA si mnawasikia majibu wanayoyatoaaaaaa.........

KATENDA nini?
 
Back
Top Bottom