Hivi "Ga" lina asili na Kiswahili?

Hivi "Ga" lina asili na Kiswahili?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,837
Reaction score
50,541
Mara nyingi kwenye maongezi yetu mitaani huwa tunaongeza neno "Ga" ili kuonesha kuwa sentesi husika inamaanisha wakati uliopita. Kwa mfano "unakulaga" "anakujaga" "ninasemaga" na mengine mengi tu. Hivi hili neno "ga" lina asili na Kiswahili au vipi? Na ieleweke kuwa siulizi kama lina asili ya Kiswahili.

Nachukiaga sana watu wanaopenda kuchangia kwa kusomaga kichwa cha habari tu badala ya kusoma habari nzima ndipo wachangie!!
 
jibu ni sio kiswahili hicho !!!!

hicho kama sio kihaya, kinyilamba basi ni kiha.

Kinachofanyika ni mzungumzaji wa lugha ya kiswahili kutaka kuonesha hali ya mazoea katika utendaji wake , hivyo kwa kukosea huongeza vitamkwa kama -ga, -ge na -gi.

lakini tukirudi jinsi kiswahili chenyewe kilivyo, mbadala wa hivyo viambishi ni neno/kishazi "huwa"

mfano. sipendagi = huwa sipendi
huwaga. = huwa

Akhsante.
 
jibu ni sio kiswahili hicho !!!!

hicho kama sio kihaya, kinyilamba basi ni kiha.

Kinachofanyika ni mzungumzaji wa lugha ya kiswahili kutaka kuonesha hali ya mazoea katika utendaji wake , hivyo kwa kukosea huongeza vitamkwa kama -ga, -ge na -gi.

lakini tukirudi jinsi kiswahili chenyewe kilivyo, mbadala wa hivyo viambishi ni neno/kishazi "huwa"

mfano. sipendagi = huwa sipendi
huwaga. = huwa

Akhsante.
Nimeupenda huo ufafanuzi!!
 
kwetu tunatumianga -nga sio -ga

nakubali kwamba -nga hutumiwa kumaanisha "huwa" lakini eleza neno "huwanga". haungesma "huwa huwa" kumaanisha "huwanga"...
 
kwetu tunatumianga -nga sio -ga

nakubali kwamba -nga hutumiwa kumaanisha "huwa" lakini eleza neno "huwanga". haungesma "huwa huwa" kumaanisha "huwanga"...
Nadhani hii ya kwako si mara nyingi sana!!
 
Back
Top Bottom