Hivi Dr Bashiru anajua kuwa chanzo cha watu kutojitokeza kwa uwingi kwenye vituo vya kupiga kura ni CCM wenyewe?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,156
Nimemsikia Dr Bashiru akilalamikia sana huko Morogoro kuwa watu wanaojitokeza kupiga kura hivi sasa ni wachache sana na idadi hiyo inazidi kushuka kadri siku zinavyosonga mbele

Lakini Dr Bashiru amejiuliza chanzo cha watu hao wanaopiga kura kupungua kwa kasi hiyo ya kutisha??

Ngoja mimi nimpe jibu la moja kwa moja kuwa chanzo cha kupungua huko ni CCM wenyewe.

Nitajaribu kuelezea ni kwanini CCM ndiyo adui namba moja ya kupungua wapiga kura

1. Unapoenda kwenye uchaguzi ni lazima uyakubali matokeo ya aina 2/ ambayo ni kushinda na kushindwa. Lakini kwa Bahati mbaya sana hivi sasa CCM wanaingia kwenye hizo chaguzi wakiwa na uhakika wa asilimia 100 wa kushinda chaguzi hizo!

2. Tume ya uchaguzi haiko huru katika muundo wake, kwa kuwa kuanzia Mwenyekiti hadi wajumbe wake wanateuliwa na Mwenyekiti wa CCM ambaye ndiye Rais wa nchi, ambaye chama chake ni mmoja ya washindani, jambo linalofanya wananchi wakose Imani na Tume hiyo

3. Matumizi makubwa ya vyombo vya ulinzi katika chaguzi hizo, hususani Jeshi letu la Polisi, nayo inawanyong'onyeza sana wananchi. Iweje tunafanya uchaguzi ulio huru na haki kuwe na askari wa Jeshi la Polisi walio wengi kama vile nchi iko vitani?

Hizi ndiyo sababu zangu juu za watu kutokwenda kwenye vituo vya kupigia kura na kama hatua za haraka zisipochukuliwa, tusije shangaa katika chaguzi zijazo tukawaona Wasimamizi wa uchaguzi na askari Polisi kuwa ndiyo pekee ya watu watakaoonekana kwenye vituo hivyo wakati wa kupiga kura!

Mungu ibariki Tanzania
 
Me nimewahi sit ya mbele kabisa
Umewahi siti ya mbele lakini changia mada iliyopo mezani........

Tunajaribu kuangalia nini chanzo cha kushuka kwa kasi ya kutisha kwa wapiga kura kwenye vituo vya kupigia kura??
 
Bashiru amejua rojo sana, anatia aibu.

Yeye ametoa sababu? Je anapendekeza nini?
 
Na sababu nyingine huenda ikawa ni kuitikia wito uliotolewa kabla kuwa watu wasijihusishe na siasa mpaka 2020.
Very true

Huwezi kuwaambia vyama vya upinzani kuwa umepiga marufuku shughuli zote za kisiasa hadi mwaka 2020 kwa vyama vya upinzani, wakati wanaona kila baada ya muda mfupi Tume ya Taifa ya uchaguzi mnatangaza tarehe mpya ya kufanyika chaguzi ndogo!
 
Hivi utawezaje kuwaahawishi wapiga kura wako kwenye vituo vya kupigia kura wakati wanashuhudia ukiwawapa maelekezo watendaji wako, ambao ndiyo wasimamizi wa chaguzi hizo kama ifuatavyo:-

Nimekutea wewe nakupa gari ya kifahari ya kutembelea, nyumba nzuri ya kuishi na mshahara na marupurupu manino, halafu nisikie umemtangaza mpinzani kashinda...... Mwisho wa kunukuu
 
usitegemee bunge linalojaa wabunge wanaotegemea kuiba kura au wanaohama vyama kwa hajili ubinafsi wao hili wawe na manufaa kwa taifa.Ndugu zangu watu wa aina hii ni wakuogopa maana kinachowapeleka bugeni ni tumbo sio kutetea wanyonge wanaowakilisha.Bunge liko pale kwa hajili ya ku debate na kufikia muafaka kwa manufaa ya taifa sio kusema HAPANA AU NDIOOO KWA KILA JAMBO
 
sababu ziko wazi ... Hivi simba ikicheza na yanga na simba ikicheza na lipuli idadi ya wanaoenda uwanjani au wanaotazama mpira inalingana? Na kwa kinachoendelea sasa hivi cha watu kujiuzulu upande A na kujiunga na upande B na kurudi tena kwa wapiga kura wale wale kuwaomba kura unafikiri kinawafurahisha sana wapiga kura? Naona sababu ziko wazi kabisa na haihitaji utafiti ... Uchaguzi wa 2015 watu wengi walijitokeza kupika kura, unafikiri ni kwanini??
 
Nadhanani Dr. Bashiru angewaomba watanzania wajifungie ndani waangalie TV siku ya uchaguzi ili amani na utulivu viweze kudumu.
Kwanini serikali ilazimike kusambaza polisi kila mahali wakati kuna njia raisi? Tutangaziwe kuwa ni uchaguzi wa CCM, hivyo wengine tuangalie TV majumbani.
 
Angalia ule uhuni uliofanyika Zanzibar..

Chini ya Mwenyekiti Jecha wa ZEC..
Sanduku la Kura haliheshimiwi,

Mambo ya kipumbavu sana , alafu anakuja kuongea nini huyu Bashiru..

Tupiganie Katiba Mpya ndiyo itakuwa suluhisho la matatizo yetu mengi kama Taifa..
 
Sidhani Kama kuna haja ya kupiga kura. Washindi walishapangwa, kutoka CCM na wasipopita uchaguzi unarudiwa.Bora kukaa ndani na kuangalia TV. Hujuma Zach CCM zinakatisha tamaa. Mara watu wasiojulikana waibe sanduku kura, mara maafisa waamuriwe kutopokea fomu baadaye CCM watangazwe kupita bila kupingwa yaani ni kero tupu hadi aibu.
Nimemsikia Dr Bashiru akilalamikia sana huko Morogoro kuwa watu wanaojitokeza kupiga kura hivi sasa ni wachache sana na idadi hiyo inazidi kushuka kadri siku zinavyosonga mbele

Lakini Dr Bashiru amejiuliza chanzo cha watu hao wanaopiga kura kupungua kwa kasi hiyo ya kutisha??

Ngoja mimi nimpe jibu la moja kwa moja kuwa chanzo cha kupungua huko ni CCM wenyewe.

Nitajaribu kuelezea ni kwanini CCM ndiyo adui namba moja ya kupungua wapiga kura

1. Unapoenda kwenye uchaguzi ni lazima uyakubali matokeo ya aina 2/ ambayo ni kushinda na kushindwa. Lakini kwa Bahati mbaya sana hivi sasa CCM wanaingia kwenye hizo chaguzi wakiwa na uhakika wa asilimia 100 wa kushinda chaguzi hizo!

2. Tume ya uchaguzi haiko huru katika muundo wake, kwa kuwa kuanzia Mwenyekiti hadi wajumbe wake wanateuliwa na Mwenyekiti wa CCM ambaye ndiye Rais wa nchi, ambaye chama chake ni mmoja ya washindani, jambo linalofanya wananchi wakose Imani na Tume hiyo

3. Matumizi makubwa ya vyombo vya ulinzi katika chaguzi hizo, hususani Jeshi letu la Polisi, nayo inawanyong'onyeza sana wananchi. Iweje tunafanya uchaguzi ulio huru na haki kuwe na askari wa Jeshi la Polisi walio wengi kama vile nchi iko vitani?

Hizi ndiyo sababu zangu juu za watu kutokwenda kwenye vituo vya kupigia kura na kama hatua za haraka zisipochukuliwa, tusije shangaa katika chaguzi zijazo tukawaona Wasimamizi wa uchaguzi na askari Polisi kuwa ndiyo pekee ya watu watakaoonekana kwenye vituo hivyo wakati wa kupiga kura!

Mungu ibariki Tanzania
 
Back
Top Bottom