Uchaguzi 2020 Hivi Dkt. Magufuli atasema amefanya nini Bukoba kwa miaka mitano yote siku ya kesho?

instanbul

JF-Expert Member
Jun 26, 2016
11,381
14,186
Nasubiri siku ya kesho kuangalia atakachoongea mheshimiwa kuhusu Yale aliyoyatekeleza miaka mitano mjini Bukoba.

Kimsingi mji huu yaani manispaa hii hakuna kitu chochote kutoka serikalini kilichotekelezwa.

Barabara za mji ni ndogo na mbovu zote wakati hata hazifiki 20 km lakini wakazi wa mji huu wanasikia maflyover na madaraja ya baharini yakijengwa huko Tanzania.

Mji huu mkongwe ulioanzishwa mwaka 1890 hauna stendi ya mabasi na daladala mpaka Leo hii. Kuna kiuchochoro flani chenye tope jekundu ndo hupaki magari. Wakati huko Tanzania hata wilaya na vimiji vidogo vina stendi kubwa Tu za kisasa.

Mji huu hauna jengo lolote la maana la serikali. Yaani hata makao makuu ya NIDA, TANESCO ni vijumba vidogo. Hata makao makuu ya CCM mkoa ni gofu flani wakati huko Tanzania kuna mikoa inajenga miji ya kiserikali kama Chato na Geita nk

Mji Una soko kuu la mabati ambalo mvua ikinyesha ni kama dampo flani la mji. Wakati huko Tanzania kuna masoko ya kisasa.

Mji huu taa zake huwa haziwaki, mji umejaa vibaka kama wote ndio maana hata 2015 watu walikuwa wanakatwa makoromeo na kuchoma makanisa. Wakati huko Tanzania kuna miji midogo Sana ina mpaka traffic lights.

Wakati NHC wakijenga maghorofa marefu huko Tanzania, Bukoba kumejaa magofu ya 1957 ambayo nayo yalinyanganywa wahindi na kuyataifishwa ambayo hayafanyiwi ukarabati hata kidogo na ndio yaliua watu wengi kipindi cha tetemeko.

Mji huu una uwanja wa mpira mzuri tu, pitch nzuri ya kuchezea, Kaitaba lakini majukwaa yake ni ya mbao na ni machache lakini huko Tanzania tunasikia viwanja vikubwa vikijengwa.

Nimeona katika tumetekeleza, Kagera wanaongelea ukarabati wa Ihungo na Nyakato sijui kituo cha afya yaani bila tetemeko hayo yasingefanyika.

Watasema meli, meli CCM hao hao ndo waliiharibu Leo wanajitapa kuirudisha

Yaan katiba ingeruhusu kuuliza maswali wagombea ingekuwa vyema Sana.
 
Wananchi wa bukoba hawana uzalendo huo. Sidhani kama watakua tayari kupokea zawadi ya senene msimu huu
 
Nasubiri siku ya kesho kuangalia atakachoongea mheshimiwa kuhusu Yale aliyoyatekeleza miaka mitano mjini Bukoba.

Kimsingi mji huu yaani manispaa hii hakuna kitu chochote kutoka serikalini kilichotekelezwa...
Atazungumzia MV Victoria tu hakuna jingine
 
Una macho lakini huoni sasa utasaidiwaje?
Umeshikiwa akiri na mbowe na Lisu hutaweza kuona kamwe.
Hebu nitajie kilichafanyika Bukoba.

Halafu hao chadema pia si walikuwa wanaiongoza bukoba kuanzia meya mpaka udiwani na wameshindwa kufanya lolote
 
Nimetamani kulia kwa haya CCM inayowafanyia watu wa Bukoba
Nimemuoa Leo akijikongoja na kuanza kuwasifia wahaya eti wanakula samaki ndo maana Wana akili. Nadhani kuna baadhi ya makabila huyaogopa Tz na yanamtisha.
 
Nasubiri siku ya kesho kuangalia atakachoongea mheshimiwa kuhusu Yale aliyoyatekeleza miaka mitano mjini Bukoba.

Kimsingi mji huu yaani manispaa hii hakuna kitu chochote kutoka serikalini kilichotekelezwa...
Wewe jamaa huwa sijui ukoje,

Hujui kwamba wahaya ni much knowing na wabinafsi mkiletewa hela za maendeleo mnazozana mpaka zinarudi zilikotoka. Je, Hapo utalaumu rais hapo?

Mbaya zaidi mnachagua upinzani ambao hata huwezi kuwaajibisha.

Madiwani wengi wa upinzani wamekwamisha
 
Wewe jamaa huwa sijui ukoje,
Hujui kwamba wahaya ni much knowing na wabinafsi mkiletewa hela za maendeleo mnazozana mpaka zinarudi zilikotoka.
Je, Hapo utalaumu rais hapo?...
CCM kwa bukoba Hesabuni maumivu
 
Wahaya msikubali kudanganywa na Magufuli eti kawaletea meli , wakati kuna mabasi kibao na mnafika BK mapema, mkataeni Magufuli na CCM yake kama ukoma, Wahaya mmedhulumiwa hela za Msaada baada ya kutokea tetemeko, Wahaya wafwa msikubali kabisa kumchagua Jiwe mkataeni huyooo
 
Wewe jamaa huwa sijui ukoje,
Hujui kwamba wahaya ni much knowing na wabinafsi mkiletewa hela za maendeleo mnazozana mpaka zinarudi zilikotoka.
Je? Hapo utalaumu rais hapo...
Hiv serikali na hao wahaya wako ni Nani mwenye nguvu na mamlaka?

Hiv serikali ilitaka kujenga stendi au soko inashindwaje kupata eneo na kujenga?

Kwa hiyo miradi Yote ya dar tuwapongeze wazaramo Kwa kutokuwa wabinafsi na much knowing

Au huko Bukoba kuna freehold land tenure system kwamba serikali haiwezi kufanya lolote bila wananchi kuridhia?
Mbona kimara nyumba zilibomolewa vzr tu na road ikajengwa?
 
Back
Top Bottom