Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,555
- 41,066
Kuna Watanzania ni laana kwa nchi hii. Wengine ni kutokana na ujinga na uwezo duni wa kuona mbali. Wengine ni mawakala wa maadui wa Taifa letu. Wengine ni sababu ya ubinafsi na tamaa.
Ulimwengu huu tangu uumbwe, vita vilivyopiganwa mara nyingi zaidi, ni vya kugombania maeneo/ardhi. Urusi inapigana na Ukraine kwa nia ya kuyachukua maeneo yote ya mashariki mwa Ukraine. Ukraine nayo inapambana kurudisha maeneo yaliyoporwa. Waisrael na wapalestina wanapigana kugombania maeneo. Kadhalika Spain na Morocco, Tanzania na Uganda, n.k.
Hivyo mtu yeyote mwenye kichwa kinachofanya kazi, anakuwa makini sana kwenye suala la wageni kuwapa rasilimali msingi ambazo siku moja zinaweza kumpa mgeni nafasi rahisi ya ushindi.
WAARABU
Mfalme wa Oman, miaka ya karibuni ametamka kwa uwazi kuwa lazima siku moja makao makuu ya sultani wa Oman yarudi Zanzibar.
Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar amewahi kutamka kuwa maeneo yote ya pwani ya bahari kutoka pwani ya bahari kuingia bara kilometa 20, ukanda wote toka Pangani mpaka Mtwara, ni maeneo ya Zanzibar kwa sababu maeneo hayo yalikuwa chini ya utawala wa sultani.
IGA inasema DP wanatakiwa kumilikishwa ardhi ya maeneo yote watakayowekeza. IGA ni mkataba mama, na haujabadilishwa hata nukta moja hata leo. IGA, kila mmoja mwenye uelewa aliiona, lakini HGA iliyosainiwa hakuna aliyeiona, na wanayoyanena hawa watu wasioaminika, hakuna mwenye uhakika kama yapo kwenye mkataba huo wa bandari ya Dar au ni mwendelezo ule ule wa uwongo na ulaghai wa watawala. Lakini hata kama maneno wanayoyasema ni kweli, bila mabadiliko ya IGA, siku yoyote DP wanaweza kuibuka na kudai kilichopo kwenye IGA.
LENGO LA MUDA MREFU
DP watachukua maeneo ya bandari, na maeneo mengine ya pwani ya bahari watayanunua toka kwa wananchi, ambao wengi wao ni maskini, na hawatakuwa na uwezo wa kukataa donge nono la mnunuzi mwarabu. Baada ya miaka mingi mbeleni, pwani yote ya bahari, toka Pangani mpaka Mtwara, itakaliwa na kumilikiwa na waarabu. Na kutokana na nguvu ya pesa, watajiunga CCM, (na kwa CCM ukiwa na pesa utapewa cheo chochote utakachotaka) na hivyo kuwafanya wageni hawa wawe na nguvu za kisiasa na uchumi.
Yumkini, huko mbeleni pwani yote ya bahari ya hindi itachukuliwa na waarabu, na kisha kuifanya ni sehemu ya Zanzibar. Hilo likitokea, Tanganyika itakuwa landlocked, ikibakiwa na vibandari vya kwenye maziwa, na hivyo kuzitegemea bandari za mataifa mengine. Ukamilifu wa haya unaweza usitokee miaka ya karibuni, lakini ni mpango wa muda mrefu. Baada ya migogoro mingi, Zanzibar itajitenga, na kuridhia kuwa sehemu ya Oman, na hapo ndipo makao makuu ya sultani yatahamia mji mkongwe.
Ulimwengu huu tangu uumbwe, vita vilivyopiganwa mara nyingi zaidi, ni vya kugombania maeneo/ardhi. Urusi inapigana na Ukraine kwa nia ya kuyachukua maeneo yote ya mashariki mwa Ukraine. Ukraine nayo inapambana kurudisha maeneo yaliyoporwa. Waisrael na wapalestina wanapigana kugombania maeneo. Kadhalika Spain na Morocco, Tanzania na Uganda, n.k.
Hivyo mtu yeyote mwenye kichwa kinachofanya kazi, anakuwa makini sana kwenye suala la wageni kuwapa rasilimali msingi ambazo siku moja zinaweza kumpa mgeni nafasi rahisi ya ushindi.
WAARABU
Mfalme wa Oman, miaka ya karibuni ametamka kwa uwazi kuwa lazima siku moja makao makuu ya sultani wa Oman yarudi Zanzibar.
Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar amewahi kutamka kuwa maeneo yote ya pwani ya bahari kutoka pwani ya bahari kuingia bara kilometa 20, ukanda wote toka Pangani mpaka Mtwara, ni maeneo ya Zanzibar kwa sababu maeneo hayo yalikuwa chini ya utawala wa sultani.
IGA inasema DP wanatakiwa kumilikishwa ardhi ya maeneo yote watakayowekeza. IGA ni mkataba mama, na haujabadilishwa hata nukta moja hata leo. IGA, kila mmoja mwenye uelewa aliiona, lakini HGA iliyosainiwa hakuna aliyeiona, na wanayoyanena hawa watu wasioaminika, hakuna mwenye uhakika kama yapo kwenye mkataba huo wa bandari ya Dar au ni mwendelezo ule ule wa uwongo na ulaghai wa watawala. Lakini hata kama maneno wanayoyasema ni kweli, bila mabadiliko ya IGA, siku yoyote DP wanaweza kuibuka na kudai kilichopo kwenye IGA.
LENGO LA MUDA MREFU
DP watachukua maeneo ya bandari, na maeneo mengine ya pwani ya bahari watayanunua toka kwa wananchi, ambao wengi wao ni maskini, na hawatakuwa na uwezo wa kukataa donge nono la mnunuzi mwarabu. Baada ya miaka mingi mbeleni, pwani yote ya bahari, toka Pangani mpaka Mtwara, itakaliwa na kumilikiwa na waarabu. Na kutokana na nguvu ya pesa, watajiunga CCM, (na kwa CCM ukiwa na pesa utapewa cheo chochote utakachotaka) na hivyo kuwafanya wageni hawa wawe na nguvu za kisiasa na uchumi.
Yumkini, huko mbeleni pwani yote ya bahari ya hindi itachukuliwa na waarabu, na kisha kuifanya ni sehemu ya Zanzibar. Hilo likitokea, Tanganyika itakuwa landlocked, ikibakiwa na vibandari vya kwenye maziwa, na hivyo kuzitegemea bandari za mataifa mengine. Ukamilifu wa haya unaweza usitokee miaka ya karibuni, lakini ni mpango wa muda mrefu. Baada ya migogoro mingi, Zanzibar itajitenga, na kuridhia kuwa sehemu ya Oman, na hapo ndipo makao makuu ya sultani yatahamia mji mkongwe.