Hivi dini inanafasi gani katika mapenzi?

Hivi dini inanafasi gani katika mapenzi?

Perry

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2011
Posts
10,082
Reaction score
2,358
Kuna mtu kitambo flani alinitosa bila sababu.Sasa juzi ameanza kurudisha mawasiliano nikamdadisi sababu za kunitosa kipindi kile akadai eti ni vile mimi sio msabato mwenzake najiuliza hivi dini nayo ina matter katika mahusiano ya kimapenzi.

Naomba kufahamishwa
 
Mapenzi yana uhusiano mkubwa ktk mapenzi. Nafasi ya dini ni makubaliano yenu, ila wasabato huwa wanataka wenzao ili kuondoa utata wa ndoa
 
Mapenzi yana uhusiano mkubwa ktk mapenzi. Nafasi ya dini ni makubaliano yenu, ila wasabato huwa wanataka wenzao ili kuondoa utata wa ndoa

Na hawa mashahidi wa jehova.Ila kama mtu kakupenda kwa dhati huwa anaenda kinyume na matarajio.It needs a very deep love ili uoe mtu wa dini tofauti.
Wengi wanatumia iyo sababu kukupiga chini hata tofauti vya dhehebu huwa inakuzwa.
 
Nafas ya Dini katka mapenz inategemea na makubaliano kat yen na wazaz wenu
 
Nikikwisha kusema sitaoa ukistu wala uisilamu bali nitaoa binti ambaye sifa kubwa nitahakikisha ni mwanamke...nimesimama katika hili! Kwamba wanangu watalelewa katika misingi gani nitalijua mbele kwa mbele muhimu nitafanya kila linalowezekana wapate elimu...elimu dunia!
 
Dini roho yako tu bhanaa!sikuhizi watu wamepata pakujificha utasikia wakimtaja Mungu but mmmmh!ndoa na dini/dhehebu si sababu labda kama hajakupenda
 
Sioni kama kuna uhusiano wowote . mtu akikuacha eti kwasabb din haziendan uyo nimchawi wamapenzi
 
Dini ni ya muhimu sana katika ndoa au mahusiano... Na sio dini tu.. Mila na mengineyo... Why dini? Kwasababu ya imani na mafundisho, mafundisho ya dini... Mfano dini yangu inasema pombe sio kosa.. Yako yasema pombe ni kosa.. Hapo mtafika?

Dini yako yasema mke na mume mmoja mwenzio anasema wake wanne... Mtafika... Kujena familia mkiamini sehemu moja ina faida kwa watoto.. Fikiria mtoto amekuwa akienda church na mama.. Baadae Mungu anamchukua.. Baba anaanza mpeleka kwingine hy inakuwaje?
 
Dini ina nafasi kubwa katika mahusiano hasa kama mnampango wa kuoana mnaweza kua mna imani za chini pindi mnapokua mnaanza mahusiano yenu na vile vile mkaamua kuishi wote kila mtu na imani yake.

Lakini inapokuja kutokea mmoja wenu au nyote mkaamua kumrudia mungu wake hapo lazima matatizo yaanze labda mmoja amue kumfuata mwenzie na ukizingatia kila mtu anajiona imani yake ni bora kuliko mwenzie lazima tu mtagombana na watoto mtawachanganya.

Kwa hiyo kabla hajafikiria kuishi wote lazima mkubaliane mmoja awe tayari kumfuata mwenzie sivyo mtaendelea kuishi maisha ya kuzini maana yake hamna ndoa ya Dini tofauti
 
Back
Top Bottom