Hivi Congo ina bahari au haina bahari

Hivi Congo ina bahari au haina bahari

Kuna nchi mbili tofauti zinazotumia jina la Congo,

Kuna Congo DRC- Kinshasa ambayo haina bahari ( landlocked) ingawa Kuna eneo dogo inapakana Moja kwa Moja na bahari ya Atlantic.

Pili Ni Congo Brazaville ambayo inapakana na bahari ya Atlantic.

Ipi unayoulizia?


Unaitaje nchi iliyo na access ya bahari landlocked
 
Huo ni mkondo tu wa bahari ,bahari ipo Angola kama wanayo bahari kwann hawana bandari waje kushusha bidhaa bandari ya Dar


Bidhaa itoke India kwenda DRC, mfano Goma mashariki ya Congo ipitie Bahari ya Atlantic???!!, kwa gharama gani??, kwanini isipitie Bahari ya hindi na ama ishuke Mombasa, Tanga au Dar kisha isafrishwe kwa Treni (Reli ya kati hadi kigoma) au isafirishwe kwa Malori hadi Goma au isafirishwe kwa meli (liemba) kwenda sehemu zingine za DRC, kifupi ni suala la upembuzi yakinifu wa kibiashara kujua faida ipo wapi.

Hebu soma hii "screen shot" uangalie, je DRC inapakana na Bahari ya Atlantic au laa!!. na angalia pameandika maneno haya:- "the country has a 25miles (40 km) Coastline on the Atlantic ocean"
Screenshot_20200809-150102.png
 
Na kama inabahari , imekuwaje wakose bandari ya kupokelea mizigo hadi watumie bandari yetu?
 
Na kama inabahari , imekuwaje wakose bandari ya kupokelea mizigo hadi watumie bandari yetu?


DRC nadhani ni nchi kubwa ya pili au ya kwanza katika Africa, Tz nadhani inaingia mara 3 ndani ya DRC, mtu akitoka Kinshasa kwenda Goma anatembea km nyingi kuliko mtu akitoka Dar kwenda kigoma. Sasa itakuwa ni ujinga wa kibiashara (biashara kichaa) Mtu wa Goma aagize mzigo kutoka China au India atumie bandari yao iliyopo Bahari ya Atlantic na aache bandari za Africa ya mashariki zilizopo Bahari ya Hindi!!!.
 
DRC nadhani ni nchi kubwa ya pili au ya kwanza katika Africa, Tz nadhani inaingia mara 3 ndani ya DRC, mtu akitoka Kinshasa kwenda Goma anatembea km nyingi kuliko mtu akitoka Dar kwenda kigoma. Sasa itakuwa ni ujinga wa kibiashara (biashara kichaa) Mtu wa Goma aagize mzigo kutoka China au India atumie bandari yao iliyopo Bahari ya Atlantic na aache bandari za Africa ya mashariki zilizopo Bahari ya Hindi!!!.
Najaribu kukuelewa lakini akili inakataa. Kwahyo huko Goma wanakabandari angalao kwa kuhudumia maeneo ya karibu au pia wanatumia bandari yetu?
 
Congo DRC wana bandari ndogo sana. Siyo kubwa. Hata bandari ya Congo Brazzaville inaizidi ya DRC. Lakini kama anataka kujua kama wana bahari, aende Google maps, siyo kuuliza JF.
Ni kama swali la kijinga lakini lina mantiki kubwa, cha kuongeza je kama ina bahari bandari wanayo? Na kama bandari wanayo ni kwa nini wategemee bandari zetu?
 
Nakaa hapa mimi. Bandari yao ni ndogo sana. Isitoshe, mizigo inayopita Dar/Mombasa ni ile inaypokwenda mashariki mwa nchi - Goma, Kivu, Lubumbashi nk. Haiendi Kinshasa. Kuna shida ya usalama pia kwenye nchi yao. Kuna vita nk. Kuupitisha mzigo toka Kinshasa hadi Goma, mashariki karibu na mpaka na Rwanda, siyo salama.
Na kama inabahari , imekuwaje wakose bandari ya kupokelea mizigo hadi watumie bandari yetu?
 
Nakaa hapa mimi. Bandari yao ni ndogo sana. Isitoshe, mizigo inayopita Dar/Mombasa ni ile inaypokwenda mashariki mwa nchi - Goma, Kivu, Lubumbashi nk. Haiendi Kinshasa. Kuna shida ya usamala pia kwenye nchi yao. Kuna vita nk. Kuupitisha mzigo toka Kinshasa hadi Goma, mashariki karibu na mpaka na Rwanda, siyo salama.
Nmekusoma mkuu
 
Republic Democratic of Congo inayo bahari na bandari katika bahari ya Atlantic, eneo la ukanda mdogo kusini magharibi mwa nchi hiyo. Bandari yao inaitwa Boma, ambayo ipo pembeni ya maporomoko ya mto Congo unapoporomoka kuingia baharini. Eneo la bahari na fukwe lenyewe ni dogo, hivyo inaifanya Congo ionekane kama haina bahari. Bandari ya Boma ni kubwa, ina kiwanja cha ndege pia na barabara nzuri zinazopita kwenye milima kukwepa maporomoko ya mto Congo kuelekea katika jiji la Kinshasa mji mkuu wa Congo. Mizigo yote na meli kutoka/Kwenda Afrika magharibi, Ulaya na Amerika upitia kwenye mlango wa bahari hiyo ya Boma Congo, Lakini mizigo kutoka/Kwenda Uchina, india, Japan, Afrika Mashariki, Australia na Korea upitia Afrika Mashariki(Tanzania). Eneo la bahari dogo la Kongo upakana kusini na Angola na kasikazini upakana na Cabinda(eneo huru linalotawaliwa na Angola linalopigana kujitenga). Kwahiyo Congo Kinchasa inayo bahari uko Atlantic ingawa ni Eneo dogo la Kilomètre kama 60.
 
Kuna nchi mbili tofauti zinazotumia jina la Congo,

Kuna Congo DRC- Kinshasa ambayo haina bahari ( landlocked) ingawa Kuna eneo dogo inapakana Moja kwa Moja na bahari ya Atlantic.

Pili Ni Congo Brazaville ambayo inapakana na bahari ya Atlantic.

Ipi unayoulizia?
Inabahari bana mkuu
 
Hakuna bahari.hapo unapopaona kwenye ramani kama pana bahari panaitwa Cabinda ni eneo la Angola kuna jambo lilitoka kipindi cha ukoloni wakapewa Angola
Nimefika Matadi ,nibahari ingawa mawe mengi
 
Huo ni mkondo tu wa bahari ,bahari ipo Angola kama wanayo bahari kwann hawana bandari waje kushusha bidhaa bandari ya Dar
Wako Atlantic hivyo kupitia Dar Ni distance fupi kuliko meli zizunguke Atlantic na kumbuka Atlantic ndo bahari korofi,haizoeleki,ukijifanya be mjanja utakutwa Bermuda pembetatu upotee
 
Najaribu kukuelewa lakini akili inakataa. Kwahyo huko Goma wanakabandari angalao kwa kuhudumia maeneo ya karibu au pia wanatumia bandari yetu?


Goma ni eneo la DRC linalopakana na Rwanda, ni rahisi wao kutumia bandari za Africa mashariki (Dar, Tanga na Mombasa) kuliko bandari yao huko kwao katika Bahari ya Atlantic ambako ni mbali sana ukilinganisha na umbali kutoka Dar au Mombasa, pia ndani ya Congo hakuna usalama mkubwa kusafirisha mzigo kutoka Bandari yao upite katikati ya nchi kwa lori hadi Goma, barabara zao pia ni mbovu sana.
 
Back
Top Bottom