GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,426
- 120,778
Huko nyuma ulikuwa ukijua tu unasafiri na ATCL ( zamani ATC ) kwenda Mikoani au nchi za jirani halafu katika Ndege unayoipanda ama yupo Captain Mapunda au Captain Mazula au wapo Wote wawili ilikuwa ni burudani na uhakika tosha wa safari yako kwani walikuwa na vitu vingi sana vya ziada ambavyo ni nadra mno kuviona kwa Marubani wa sasa waliopo ATCL.
Walikuwa ni Marubani wachangamfu sana na ambao walikuwa siyo tu wanaijua Kazi yao bali walikuwa wanaipenda sana Kazi yao ya Urubani na ndiyo maana haishangazi mpaka hivi leo wanasifika na kukumbukwa mno na Wadau.
ATCL nawapongezeni kwa kuwa na Marubani wenu wa sasa ila nisiwaficheni kwa kuwaambia kuwa sijui ni aina ya Ndege zenu au ni Wao wenyewe labda wanaogopa kuziharibu mwishoni Dereva wa Lori akawasweka Jela / Lupango kwani wanaendesha Ndege hizo kwa mwendo siyo wa Kasi vile halafu muda ambao huwa wanatutangazia kuwa tutafika tuendako huwa hauwi huo na badala yake lazima tu mtachelewa kati ya dakika 15 hadi 30 na hata wakiwachelewesheni hivyo hawawaombi radhi na badala yake mkiwa mnashuka na kukutana pale Mlangoni au chini wanabaki tu kuwatoleeni tabasamu zao za kulazimisha na kuwaulizeni safari ilikuwaje.
Je tatizo ni nini hasa? Mbona akina Captain Mapunda na mwenzake Captain Mazula wao Dar to Kilimanjaro walikuwa wanatumia dakika 55 hadi 60 badala ya dakika zinazotakiwa 75? Hao hao tena Dar to Mwanza walikuwa wanatumia dakika 80 badala ya dakika 90 hadi 105?
Kwa hili ndiyo maana nadiriki kusema kuwa ATCL hata mje na Ndege zenu za kila aina ila jitahidini hawa Marubani wenu waige ule umahiri hasa wa kurusha Ndege wa Marubani wenzao Waandamizi kabisa akina Mzee Mapunda na aliyekuwa Brazameni enzi hizo Uncle Mazula kwani hata uwepo tu wa Marubani ambao wanawahi kuwafikisha Abiria waendako huongeza idadi ya Abiria na kuwapeni Sifa kubwa kitu ambacho ni faida kubwa mno katika biashara yenu hiyo ya Usafiri wa anga ambao ni wa muhimu na tegemezi kwa Watu wanaojielewa.
Nawasilisha.
Walikuwa ni Marubani wachangamfu sana na ambao walikuwa siyo tu wanaijua Kazi yao bali walikuwa wanaipenda sana Kazi yao ya Urubani na ndiyo maana haishangazi mpaka hivi leo wanasifika na kukumbukwa mno na Wadau.
ATCL nawapongezeni kwa kuwa na Marubani wenu wa sasa ila nisiwaficheni kwa kuwaambia kuwa sijui ni aina ya Ndege zenu au ni Wao wenyewe labda wanaogopa kuziharibu mwishoni Dereva wa Lori akawasweka Jela / Lupango kwani wanaendesha Ndege hizo kwa mwendo siyo wa Kasi vile halafu muda ambao huwa wanatutangazia kuwa tutafika tuendako huwa hauwi huo na badala yake lazima tu mtachelewa kati ya dakika 15 hadi 30 na hata wakiwachelewesheni hivyo hawawaombi radhi na badala yake mkiwa mnashuka na kukutana pale Mlangoni au chini wanabaki tu kuwatoleeni tabasamu zao za kulazimisha na kuwaulizeni safari ilikuwaje.
Je tatizo ni nini hasa? Mbona akina Captain Mapunda na mwenzake Captain Mazula wao Dar to Kilimanjaro walikuwa wanatumia dakika 55 hadi 60 badala ya dakika zinazotakiwa 75? Hao hao tena Dar to Mwanza walikuwa wanatumia dakika 80 badala ya dakika 90 hadi 105?
Kwa hili ndiyo maana nadiriki kusema kuwa ATCL hata mje na Ndege zenu za kila aina ila jitahidini hawa Marubani wenu waige ule umahiri hasa wa kurusha Ndege wa Marubani wenzao Waandamizi kabisa akina Mzee Mapunda na aliyekuwa Brazameni enzi hizo Uncle Mazula kwani hata uwepo tu wa Marubani ambao wanawahi kuwafikisha Abiria waendako huongeza idadi ya Abiria na kuwapeni Sifa kubwa kitu ambacho ni faida kubwa mno katika biashara yenu hiyo ya Usafiri wa anga ambao ni wa muhimu na tegemezi kwa Watu wanaojielewa.
Nawasilisha.