Hivi anayevuruga mahusano yetu ni nani?

Hivi anayevuruga mahusano yetu ni nani?

Uta Uta

JF-Expert Member
Joined
Feb 2, 2016
Posts
3,740
Reaction score
8,792
Habari wanajamvi?
Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na mitafaruku mingi ktk mahusiano. Ndoa nyingi na mahusiano mengi ya kimapenzi yanalegalega. Hakuna tena kumianiana kati ya mwanamke na mwanaume.

Kibaya zaidi wanawake wanawalaumu wanaume kuwa ndio wamesababisha uaminifu na upendo utoweke na wanaume nao wanalalamika wanawake ndio chanzo cha mapenzi ya dhati kutoweka. Sasa mi napenda kujuzwa kama wanaume hawahusiki na ufisadi wa mapenzi na wanawake nao hawahusiki pia,

Je ni nani anayetuhujumu ktk mapenzi? Anakaa sayari hii au Mars?
Hali si shwari tena mapenzi ya dhati yametoweka kama dinosoo. Naomba tutamfute mchawi anaeturoga ni nani?

Maana wanaume wanadai wao wana mapenzi ya dhati tatizo wanawake, wanawake nao wanarusha makombora upande wa pili, hapa kati kati kuna nani amejificha?
 
Anayevuruga ni mwanamke na mwanaume wote wanahusika.

1. Mke wa mtu anatongozwa anakubali ili hali anajua ana ndoa yake.

2. Mme wa mtu anatongoza wake za watu ili hali nae anajua ana mke wake wake.
KWA NN TUSISEME NOO KWA PAMOJA JAMANI NDOA NA MAPENZI YETU YADUMU ?
 
Back
Top Bottom